Top TEN walipa KODI KISEKTA, No Voda, AZAM wala Lake Oil/Kobil/RIZ-One.

Top TEN walipa KODI KISEKTA, No Voda, AZAM wala Lake Oil/Kobil/RIZ-One.

Kama Bahresa na mohammed int, wanatoa ml 500 kila mmoja kwenye uchaguzi unategemea walipe kodi
 
yaani nashindwa kuelewa kampuni kama Barrick linalomiliki migodi minne n.Mara,Buzwagi,Bulyanhulu naTulawaka linazidiwa na Resolute kampuni yenye mgodi mmoja tena size ya kati halafu wakala\dealer wa voda Simba telecom anazidi makampuni mama kama vodacom,airtelna Zantel kweli hii ndiyo Tanzania
 
kodi yangu ninayolipa kupitia voda haipelekwi tra. Jamani voda, acheni kuniibia.
 
Mkuu Kibanga Ampiga Mkoloni
Kuna tofauti kati ya kuwa tax compliant na kulipa kodi kubwa. Hao waliotajwa kwenye hiyo list ni tax compliant na sio lazima wawe walipa kodi wakubwa.
Mpendwa usituchanganye, hata Kama ni tax compliant Kama unavyodai, basi bado makampuni yanayolalamikiwa yangejitokeza kuwa ni vinara. Huwezi kuwa tajiri wa kimataifa Kama BAKHRESA and then ukitafutwa kwa walipakodi wakubwa whether by compliant or by amount haupo??.

Hayo makampuni ya madini yanayoendelea kutuachia mashimo, kodi iko wapi jamani. Kodi anayolipa mfanyakazi ni balaa. Nina ndg yangu amepata redundancy akalipwa tshs. 90 mil , akakatwa kodi 30% ambayo ni 27 mil just imagine. Na bado alipokuwa kazini kila mwezi alikuwa anakatwa kodi. Hayo ni maumivu makubwa, inakuwa Kama double tax.

Halafu kaka Sesame unaleta hadithi wakati maumivu ya mfanyakazi ni makubwa. Ingekuwa wote tunalipa wala isingeuma. Mbaya zaidi waajiri wako buzy kutukata wapate hizo sifa unazosema wakati tunaumia.

Roho imeniuma sana sana na kodi kubwa kwa mfanyakazi, Wakati huko kwenye marasilimali ya nchi hakuna. Mweeeee tunaombaaa tunaombaaaa, usiku na mchana Mungu aiponye nchi yetu, hata hivyo tusikate tamaa, maana kila iitwapo leo tunaona uovu unazidi. Wale wanaoiombea nchi hii ni prayer item, tusikate tamaa, uwazi huu nao ni majibu, tungejuaje?

Mtoa mada ubarikiwe.

Queen Esther
 
Unaniangusha yani VODA, TOGO, TTCL na AItel wanzidiw ana Simba Telecom Tanzania Limited (Telecommunication) ?
Haiwezekani kamwe labda kuna kitu hatukijuhi.

Wako wapi TANESCO? SOGAS? IPTL, SYMBION watu wanalipwa over 200 Mil kw asiku ila humu hawaonekani kwa nini?


Ukweli ni kwamba it depend investment ya kampuni na asset zake zilivyo ghali... hii inasababisha kampuni isi-break even mapema zaidi... hivyo kutukuwa na net profit mapema zaidi... that is the fact... ikumbukwe kodi ni kutoka kwenye profit na haitoki kwenye revenue... only exercise na VAT tu.
 
TRA wamegawa haya makampuni ki sekta, hivyo BAKHRESA alitakiwa kuwa among walipa kodi wakubwa. Usisahau ni Kati ya matajiri wakubwa Africa, ikiwa na maana anazalisha sana pia.
Queen Esther

Utajiri wa mtu si katika uzalishaji tu, ila kuna mambo mengi. Kuna wengine ni wazalishaji wakubwa lakini hawana assert kubwa ambazo nazo zinahesabika kama pesa ambazo huongeza dau la fedha kimahesabu.

Mtengeneza barabara ni magreda kama kumi hivi au 15 ni mtaji mkubwa ambao kwa miaka atazalishia. Hivyo pato lake ni kubwa kwa vila hamegeani na mwingine. Lakini Food manufacturing kuna kugawana sana pato kuanzia mkulima, mnunuzi toka kwa mkulima, warehouse, kiwandani na kisha kumfikia consumer. Utakuta mlolongo mrefu sana na pato lote hugawana wote hao. Huo ndio mwono ambao tuutazame katika viwanda vya manufacturing tofauti na secta ambazo zina vitendea kazi ambavyo ni kusalishia tu, maana yake wao ni kukinga pesa yote. Kama serikali inawapa tenda ya barabara itakayogharibu bilioni 50 basi zote zitaingia kwa huyo mtengeneza barabara tofauti kwa kipindi kifupi na wa food manufacturing kuna wengi wanaogawana.

Huyu wa Azam vitendea kazi vyake ni vingi yaani assert ambazo zinaonyesha kuwa ana mali nyingi na ni tajiri sana Tanzania, lakini si kipimo sahihi cha kuonyesha uzalishaji wenye kuleta ushindani wa kulipa kodi.

Kwa anayetaka ufafanuzi wa mapana na marefu anitonye nitaweka kwa kutohoa mifano mizuri zaidi.
 
haya ni maajabu voda,azam etc makampuni makubwa hayapo kwenye walipa kodi wazuri! inabid tra wawachunguze coz wana volume kubwa sana.badala ya kukimbizana na wauza maduka waende huko kujua kunani mbona wanaleta kodi kidogo?mbona wafanyakazi sijackia wanalipa sana PAYE nao wanastail kupongezwa
 
Hayo ni walipa kodi (soma walipa posho) wakubwa. Ni scandle kuyaona makampuni 3 yaliyokithiri kwa rushwa/hongo/ufisadi. Hayo ni Sopa Management (Hotels), Freight Forwarders (T) Ltd (Transportation) na Simba Telecom Tanzania Limited eti ni washindi. Kweli Tanzania inahujumiwa mpaka basi!

Haya 3 nina ushahidi mzito tu wa rushwa zao na ukwepaji kod (systematically). Kama haya 3 ni miongoni mwa walipa kodi wazuri nchini basi it's official HAKUNA MKWEPA KODI Tanzania.

NB: Ushahidi nitautoa tu Mahakamani tu).

 
haya ni maajabu voda,azam etc makampuni makubwa hayapo kwenye walipa kodi wazuri! inabid tra wawachunguze coz wana volume kubwa sana.badala ya kukimbizana na wauza maduka waende huko kujua kunani mbona wanaleta kodi kidogo?mbona wafanyakazi sijackia wanalipa sana PAYE nao wanastail kupongezwa

Unaona matangazo kila kukicha na udhamini kama Voda inapodhamini ligi kuu, pesa inayotumiwa ni ile net profit kusudi isilipiwe kodi, na kwa kawaida makampuni ambayo husaidia shughuli za maendeleo na huduma kitaifa pesa ile inayotumika kwa shughuli hiyo haitozwi kodi, hiyo ndio njia ya kuhalalisha msamaha wa kodi usio rasmi lakini unatambuliwa. Jambo hilo lipo po pote duniani.

Mataifa yaliyoendelea hata mtu binafsi anapotoa pesa sadaka kanisani au kutuma kusaidia vikundi au watu maskini Afrika, pesa hiyo anatakiwa kutunza kumbukumbu kwani mwisho wa mwaka anapofile tax return anarudishiwa, ni njia za kukwepa makali ya kodi. Hata watu mashuhuri toka Ulaya na Marekani individual wanapokuja kuchimba visima vya maji huko wameweka kumbukumbu hizo za matumiki zenye kuhakikika na revenue na mwishoni mwa mwaka hurudishiwa.

NB: Azam inamiliki timu ya mpira, hivyo net profit anayopata anaweza wave to the soccer team kama msaada na hivyo makali ya kodi kupungua.

Wengi wetu tuko bado kuelewa janja hiyo ila wafanyabiashara wakubwa hujua hili na serikali inajua na utaratibu unaotumika karibu na mataifa mengi duniani.
 
Hawajajificha, ni kwamba wao wanalipa moja kwa moja kwa "watawala" na "chama tawala" hivyo hesabu zao hazionekani kwenye data base ya TRA! Tafakari!!!

nimeipenda hii, ningekuwa natumia pc, ningekugongea like.
 
Mpendwa usituchanganye, hata Kama ni tax compliant Kama unavyodai, basi bado makampuni yanayolalamikiwa yangejitokeza kuwa ni vinara. Huwezi kuwa tajiri wa kimataifa Kama BAKHRESA and then ukitafutwa kwa walipakodi wakubwa whether by compliant or by amount haupo??.

Hayo makampuni ya madini yanayoendelea kutuachia mashimo, kodi iko wapi jamani. Kodi anayolipa mfanyakazi ni balaa. Nina ndg yangu amepata redundancy akalipwa tshs. 90 mil , akakatwa kodi 30% ambayo ni 27 mil just imagine. Na bado alipokuwa kazini kila mwezi alikuwa anakatwa kodi. Hayo ni maumivu makubwa, inakuwa Kama double tax.

Halafu kaka Sesame unaleta hadithi wakati maumivu ya mfanyakazi ni makubwa. Ingekuwa wote tunalipa wala isingeuma. Mbaya zaidi waajiri wako buzy kutukata wapate hizo sifa unazosema wakati tunaumia.

Roho imeniuma sana sana na kodi kubwa kwa mfanyakazi, Wakati huko kwenye marasilimali ya nchi hakuna. Mweeeee tunaombaaa tunaombaaaa, usiku na mchana Mungu aiponye nchi yetu, hata hivyo tusikate tamaa, maana kila iitwapo leo tunaona uovu unazidi. Wale wanaoiombea nchi hii ni prayer item, tusikate tamaa, uwazi huu nao ni majibu, tungejuaje?

Mtoa mada ubarikiwe.

Queen Esther

Queen Esther

Nilichosema hapo ni ukweli na sio hisia zangu. Hata mimi nina uchungu kama wewe, lakini kwenye fact siwezi kuacha hisia zangu ndio zinitawale. Jaribu kutafuta hiyo mikataba ya wawekezaji wakubwa unaowataja na uangalie vipengele vinavyohusu masuala ya kodi. Nahisi utaangua kilio. Lakini sheria zinazohusu makampuni na uwekezaji katika sekta mbalimbali zimewekwa na nani? Na bado utawalaumu wawekezaji tu. Wajinga ndio waliwao. Tuendelee kuwakumbatia viongozi wetu na wao waendelee kutuuza tu.
 
Mjadala bila kujua namna makampuni yanavyofanya kazi itakuwa upotoshaji tu... mfano usitegemee group companies kama IPP, S.S. Bakheresa, SUMARIA to be in top tens..........b'se they have several companies under them and those are the one recognized by TRA.

Mkuu Kasheshe. Watu wengi wanachangia kitu wasichokijua.
 
Home Shopping Centre hayumo, wadosi na viwanda vyao vyote hawamo labda kama wangetoa 100 bora kabla hatujatoa comment zaidi. Na huu mtindo wao wakuwa na kampuni kumi kumi na rushwa iliyokithiri miongoni mwa maofisa wa TRA. Tunakusanya kama 40% hivi nyingine.
 
yaani nashindwa kuelewa kampuni kama Barrick linalomiliki migodi minne n.Mara,Buzwagi,Bulyanhulu naTulawaka linazidiwa na Resolute kampuni yenye mgodi mmoja tena size ya kati halafu wakala\dealer wa voda Simba telecom anazidi makampuni mama kama vodacom,airtelna Zantel kweli hii ndiyo Tanzania
tatizo ni kutojua makampuni yanavyoendeshwa na aina za kodi na ipi inatolewa wakati gani???
 
bila rushwa huwezi kusurvive kwa mfanya biashara yeyote, hata USA wanatoa rushwa sembuse bongo? hasa hawa wafanya biashara wakubwa ndo wananuka rushwa sana
 
Rushwa Rushwa Rushwa Taifa La Walarusha Halikusanyi Kodi Inasikitisha Kuona Haya Makampuni Makubwa Ya Simu Voda, Tigo, Aitel Hayapo
 
Back
Top Bottom