Tajiri wa Magomeni
JF-Expert Member
- Aug 21, 2019
- 4,274
- 2,935
huyo jamaa gari yake ina maajabu gani hadi awe anawabeba?mkuu mbona kila mwaka kuna official drag racing mara mbili.... inaitwa destination arusha drag racing huwa tunasafiri kwenda arusha barabara imenyooka ipo quality ya hali ya juu huwa inafungwa kwa ajili ya hyo racing... ina vibari kabisa huwa wanakuja wakenya kushindana na tz
wiki ijayo inafanyika kenya inaitwa masinga TT sema hii ntaikosa majukumu yamebana ila watu wameshafiri wameweka kambi arusha kwa tuner anaitwa jason frisby na huyu ndio gari yake huwa inatubeba TZ kwenye racing na wakenya
modifications gani ukiongezea kwenye altezaa inafanya iwe nzuri/ yenye starehe zaidiSaana. Mods ni balaa, zinatumia pesa nyingi saana. Maana ni zaidi ya kununua OEM parts za gari.
inakuaje ina cc 4000 then horse power ndogo?Nafikiri ilikuwa kweli kwenye gari za kizamani na hasa za Marekani. Unakuta ina cc4000, V8, ila horsepower hazifiki 200. Ila za kisasa wamejitahidi saana. Ukihitaji performance, basi na mafuta inakunywa saana, ila ukiendesha kawaida, mafuta inatumia vizuri tuu.
yanabaugia lita ngapi kwa km 1?Zinabugia wese kwa staili ya kufa mtu kama huna kipato cha kueleweka lazma likushinde hyo ndio sababu yanauzwa bei chee
Sent using Jamii Forums mobile app
Lita moja km 8 kwa town afu high had lita moja km11yanabaugia lita ngapi kwa km 1?
altezza hakanyagi hapo sio?Lexus LS460 ya mwaka 2008. Hizo gari ni kama zimeletwa from the future.
ukiwa speed kubwa ukiyumba na kutoka nje ya line kupinduka nje njeHao jamaa hawaogopi kukaa karibu hivyo na barabara? Maana watu wengi saana huwa wanashindwa kuendesha gari kwa kasi kubwa kwenye straight line.
sure.nimekupata.altezza ipi unaikubali?Lita moja km 8 kwa town afu high had lita moja km11
Sa ka unategemea mshahara wa laki 7 kwa mwezi hyo adhabu bora ukae kwny IST unaogea lita 1 km 15 hata town trips kama mguu wako mwepesi
Yes, ile ina nguvu kweli lakini inakiu balaa. Ina engine ya 2JZ. Ila kwa Japan, nafikiri Altezza ya cc3000 ni Gita pekee. Zile saloon ni cc2000.nataka nichukue hiyo tezza yenye cc 3000 .I guess itakuwa na nguvu balaa
Kabisa yaani.ukiwa speed kubwa ukiyumba na kutoka nje ya line kupinduka nje nje
Yes, huo mnyama hatari. Japo Altezza inafurahisha zaidi kuendesha. Hilo dude ni comfortable saana. Inakuwa kama unaelea vile.altezza hakanyagi hapo sio?
Teknologia yao ilikuwa chini, sio kama ya Ulaya na Japan. Na pia mafuta kwao haikuwa gharama saana. So wanajiachia tu na ma engine makubwa yasio na ishu.inakuaje ina cc 4000 then horse power ndogo?
Aise, Altezza kwa upande wa starehe hapana. Suspension zake ni ngumu, zimekaza, na ndani imeshakuwa ya kizamani kidogo kulinganisha ni kina Brevis na Crown. Wengi huwa wanaipiga mziki wa maana, na kuongeza radio ya android, kidogo inapendeza.modifications gani ukiongezea kwenye altezaa inafanya iwe nzuri/ yenye starehe zaidi
hiyo yenye engine ya 2JZ inakula kiasi gani kwa km 1?Yes, ile ina nguvu kweli lakini inakiu balaa. Ina engine ya 2JZ. Ila kwa Japan, nafikiri Altezza ya cc3000 ni Gita pekee. Zile saloon ni cc2000.
Ile saloon ya four cylinder yenye engine ya 3S ina nguvu zaidi kuliko ya six cylinder yenye 1G. So unaweza kuchukua hiyo. Hazipishani saana nguvu na ile yenye c 3000, ila yenyewe ulaji wake wa mafuta ni mzuri. Shida yake ni kwamba hiyo engine 3S-FE Beams dual vvti iko kwenye Altezza RS200 pekee. So ikizingua inabidi uitafute hiyo hiyo ya Altezza.
unamaanisha nini unaposema altezza inafurahisha kuendesha?Yes, huo mnyama hatari. Japo Altezza inafurahisha zaidi kuendesha. Hilo dude ni comfortable saana. Inakuwa kama unaelea vile.
zile zenye uwazi kwenye bonnet ni engine gani ile?Yes, ile ina nguvu kweli lakini inakiu balaa. Ina engine ya 2JZ. Ila kwa Japan, nafikiri Altezza ya cc3000 ni Gita pekee. Zile saloon ni cc2000.
Ile saloon ya four cylinder yenye engine ya 3S ina nguvu zaidi kuliko ya six cylinder yenye 1G. So unaweza kuchukua hiyo. Hazipishani saana nguvu na ile yenye c 3000, ila yenyewe ulaji wake wa mafuta ni mzuri. Shida yake ni kwamba hiyo engine 3S-FE Beams dual vvti iko kwenye Altezza RS200 pekee. So ikizingua inabidi uitafute hiyo hiyo ya Altezza.
powerseats na seat heaters ndo nini mzee?Toyota Altezza Gita (wagon) ni moja kati ya magari mazuri na imara kuwahi kutengenezwa na kampuni ya kutengeneza magari ya Toyota kwa kipindi cha miongo kadhaa iliyopita. Gari hili liliingia sokoni mwaka 2001, miaka mitatu baada ya gari la Altezza (sedan) kupata mafanikio makubwa sokoni tangu lilipoanza kutengezwa mnamo mwaka 1998. Altezza na Altezza Gita ni magari yaliyotengenezwa kupambana na magari ya Ulaya kama BMW 3 series, Mercedes C class na Audi A4, ambayo kiutaalamu huwa yanawekwa kwenye kundi la Entry Level Compact Executive Salon/Wagon.
Kwa soko ya Ulaya na Marekani Altezza na Altezza Gita ziliuzwa kwa jina la Lexus IS, na Lexus IS SportCross.
View attachment 898986
Kuna matoleo matatu ya Altezza Gita kutokana na engine zake. Kuna AS200 yenye cc2000 ambazo ndio nyingi. Hizi zinakuja na engine ya 1G-FE, na AS300 ambayo ina engine ya 2JZ-GE yenye cc3000. Hizo engine zote ni 6 cylinder. Pia kuna models chache za Altezza Gita, RS200 zenye engine ya 3S-GE. Hii ni engine ya 4 cylinder, iliyoundwa kwa ushirikiano kati ya Toyota na Yamaha. Hii ina nguvu (200-210hp) zaidi ya ile 1G-FE, na mara nyingi inakuwa kwenye Altezza salon.
View attachment 898987
The good
The bad
- Gari hili lina muonekano mzuri na usiopitwa na wakati kirahisi (ukizingatia lina umri wa zaidi ya miaka 17). Watu wengi wanashawishika kuliita Altezza new model
- Lina features nyingi kutoka kiwandani kulinganisha na magari ya Ulaya ya kipindi hicho, hasa ukipata Limited edition (yenye seats za leather) mfano power seats kwa dereva na abiria, 6 disc CD changer, 6 airbags etc. Ukibahatisha kupata model ya Lexus ndio utafurahi zaidi. Lina mpaka seat heaters.
- Japo ni sports car, ila liko comfortable vya kutosha kwa aina ya gari, hasa kwenye barabara ya lami
- Vile ni rear wheel drive (linasukuma kwa tairi za nyuma) handling inakuwa safi sana, maana tairi za mbele zinabaki na kazi ya kuliongoza gari tuu. Kiukweli linafurahisha kuendesha, hasa kwenye barabara zenye kona.
- Hizi gari ni very reliable, yaani ni kati ya magari ambayo kiukweli hayana urafiki saana na garage. Yanavumilia shida saana. It is very well made.
Cha kuzingatia unapolinunua hilo gari likiwa limetumika
- Linakunywa mafuta zaidi ya magari ya Ulaya ya level moja, kama BMW 3 series (E46) na Mercedes C class (W203).
- Kwa kuwa ni sport car, suspension zake ni ngumu kiasi, na rims za size 17 ambazo zinakuja na gari, tairi linakuwa na low profile, hivyo haliko comfortable saana kwenye barabara za vumbi (rough roads).
- Seats za nyuma ni finyu kidogo kwa watu warefu, hasa kama dereva ni mrefu pia.
- Liko chini saana, hasa kwa barabara zetu za mtaani ambazo mara nyingi haziko kwenye hali nzuri. Hii husababisha watu wengi kuligonga sehemu za chini na kwenye bumper kama wakilitumia bila kuliinua. Na ukiliinua linakuwa bayaa, na linapoteza stability.
- Radio yake ya CD 6 huwa inaharibika kirahisi huo mfumo wa kubadilisha CD hasa inapotumiwa na watu wasio wazoefu.
Maoni yangu
- Models zote za tangu 2001 mpaka 2005 hazina tofauti kubwa, sababu gari hilo halikufanyiwa mabadiliko yeyote makubwa ndani ya kipindi hicho, zaidi ya mabadiliko madogo (facelift) mwaka kwa model ya mwaka 2003 ambapo, taa na navigation screen ndio vilibadilishwa na vitu vichache vya ndani.
- Ukinunua likiwa chini ya km 100,000 hakikisha unamuuliza muuzaji kama alibadilisha timing belt, maana huwa zina kawaida ya kukatika baada ya kufikisha km hizo. Na zikikatika zinaweza kuleta madhara makubwa kwenye engine. Kama ni Japan, hakikisha linabadilishwa huko huko.
- Usinunue ambalo lina dalili za kuwa modified saana kama hauna lengo la kulitumia kwenye mashindano na kupiga misele (drifting). Maana hizi gari zilipendwa saana na racer boys, walikuwa wanazitumia kwenye mashindano, hivyo zilikuwa abused saana.
- Manual transmission inafurahisha saana kuendesha. Ina gia sita. Japo kiukweli, hizi nimeziona chache saana. Automatic transmission nazo hazina shida. Kuna za gia nne, na gia tano. Ukiwa na auto, hakikisha unatumia ATF ya Toyoto TIV, kama hauwezi, basi bora usibadilishe kabisa.
- Engine ya 1G inatabia ya kuvuja oil kwenye Valve cover, hasa kama utajaza engine oil kupita kiasi wakati wa kufanya service. Hakikisha oil ya viscosity ya 5W40 au 10W40, na usizidishe lita 4.1. Mafundi wenge huwa wanashauri kuweka lita 5. Ni makosa ina haribu oil seals. Na usitumie oil filter za elfu 5, nunua genuine ππ.
- Hizi gari hasa zikiwa na km nyingi, bush za low control arms (lower wishbone) za mbele huwa zinaisha, na kusababisha gari kula tairi upande wa ndani. Usijaribu kufanya wheel alignment ukiona inakula tairi. Hilo sio tatizo la alignment. Tafuta hizo wishbone bushes ubadilishe. Hakikisha unaweka alama kwanza kabla ya kufungua wishbone, maana ukikosea kuzirudisha kwenye alignment tu unaharibu handling na litaboa kuendesha..
Hizi ni gari nzuri saana, ukizitunza unaweza kuzitumia kwa muda mrefu saana bila kukuletea shida yeyote. Na idadi yake sio kubwa, hivyo ukiwa nalo linakuwa unique kidogo. Ila kama unaishi sehemu yanye barabara mbovu, halikufai, hata kama wewe ni dereva mzuri. Utachoka kuliendesha.
Karibuni tupeane uzoefu.
ni altezza gani ina horsepower kubwa?Toyota Altezza Gita (wagon) ni moja kati ya magari mazuri na imara kuwahi kutengenezwa na kampuni ya kutengeneza magari ya Toyota kwa kipindi cha miongo kadhaa iliyopita. Gari hili liliingia sokoni mwaka 2001, miaka mitatu baada ya gari la Altezza (sedan) kupata mafanikio makubwa sokoni tangu lilipoanza kutengezwa mnamo mwaka 1998. Altezza na Altezza Gita ni magari yaliyotengenezwa kupambana na magari ya Ulaya kama BMW 3 series, Mercedes C class na Audi A4, ambayo kiutaalamu huwa yanawekwa kwenye kundi la Entry Level Compact Executive Salon/Wagon.
Kwa soko ya Ulaya na Marekani Altezza na Altezza Gita ziliuzwa kwa jina la Lexus IS, na Lexus IS SportCross.
View attachment 898986
Kuna matoleo matatu ya Altezza Gita kutokana na engine zake. Kuna AS200 yenye cc2000 ambazo ndio nyingi. Hizi zinakuja na engine ya 1G-FE, na AS300 ambayo ina engine ya 2JZ-GE yenye cc3000. Hizo engine zote ni 6 cylinder. Pia kuna models chache za Altezza Gita, RS200 zenye engine ya 3S-GE. Hii ni engine ya 4 cylinder, iliyoundwa kwa ushirikiano kati ya Toyota na Yamaha. Hii ina nguvu (200-210hp) zaidi ya ile 1G-FE, na mara nyingi inakuwa kwenye Altezza salon.
View attachment 898987
The good
The bad
- Gari hili lina muonekano mzuri na usiopitwa na wakati kirahisi (ukizingatia lina umri wa zaidi ya miaka 17). Watu wengi wanashawishika kuliita Altezza new model
- Lina features nyingi kutoka kiwandani kulinganisha na magari ya Ulaya ya kipindi hicho, hasa ukipata Limited edition (yenye seats za leather) mfano power seats kwa dereva na abiria, 6 disc CD changer, 6 airbags etc. Ukibahatisha kupata model ya Lexus ndio utafurahi zaidi. Lina mpaka seat heaters.
- Japo ni sports car, ila liko comfortable vya kutosha kwa aina ya gari, hasa kwenye barabara ya lami
- Vile ni rear wheel drive (linasukuma kwa tairi za nyuma) handling inakuwa safi sana, maana tairi za mbele zinabaki na kazi ya kuliongoza gari tuu. Kiukweli linafurahisha kuendesha, hasa kwenye barabara zenye kona.
- Hizi gari ni very reliable, yaani ni kati ya magari ambayo kiukweli hayana urafiki saana na garage. Yanavumilia shida saana. It is very well made.
Cha kuzingatia unapolinunua hilo gari likiwa limetumika
- Linakunywa mafuta zaidi ya magari ya Ulaya ya level moja, kama BMW 3 series (E46) na Mercedes C class (W203).
- Kwa kuwa ni sport car, suspension zake ni ngumu kiasi, na rims za size 17 ambazo zinakuja na gari, tairi linakuwa na low profile, hivyo haliko comfortable saana kwenye barabara za vumbi (rough roads).
- Seats za nyuma ni finyu kidogo kwa watu warefu, hasa kama dereva ni mrefu pia.
- Liko chini saana, hasa kwa barabara zetu za mtaani ambazo mara nyingi haziko kwenye hali nzuri. Hii husababisha watu wengi kuligonga sehemu za chini na kwenye bumper kama wakilitumia bila kuliinua. Na ukiliinua linakuwa bayaa, na linapoteza stability.
- Radio yake ya CD 6 huwa inaharibika kirahisi huo mfumo wa kubadilisha CD hasa inapotumiwa na watu wasio wazoefu.
Maoni yangu
- Models zote za tangu 2001 mpaka 2005 hazina tofauti kubwa, sababu gari hilo halikufanyiwa mabadiliko yeyote makubwa ndani ya kipindi hicho, zaidi ya mabadiliko madogo (facelift) mwaka kwa model ya mwaka 2003 ambapo, taa na navigation screen ndio vilibadilishwa na vitu vichache vya ndani.
- Ukinunua likiwa chini ya km 100,000 hakikisha unamuuliza muuzaji kama alibadilisha timing belt, maana huwa zina kawaida ya kukatika baada ya kufikisha km hizo. Na zikikatika zinaweza kuleta madhara makubwa kwenye engine. Kama ni Japan, hakikisha linabadilishwa huko huko.
- Usinunue ambalo lina dalili za kuwa modified saana kama hauna lengo la kulitumia kwenye mashindano na kupiga misele (drifting). Maana hizi gari zilipendwa saana na racer boys, walikuwa wanazitumia kwenye mashindano, hivyo zilikuwa abused saana.
- Manual transmission inafurahisha saana kuendesha. Ina gia sita. Japo kiukweli, hizi nimeziona chache saana. Automatic transmission nazo hazina shida. Kuna za gia nne, na gia tano. Ukiwa na auto, hakikisha unatumia ATF ya Toyoto TIV, kama hauwezi, basi bora usibadilishe kabisa.
- Engine ya 1G inatabia ya kuvuja oil kwenye Valve cover, hasa kama utajaza engine oil kupita kiasi wakati wa kufanya service. Hakikisha oil ya viscosity ya 5W40 au 10W40, na usizidishe lita 4.1. Mafundi wenge huwa wanashauri kuweka lita 5. Ni makosa ina haribu oil seals. Na usitumie oil filter za elfu 5, nunua genuine ππ.
- Hizi gari hasa zikiwa na km nyingi, bush za low control arms (lower wishbone) za mbele huwa zinaisha, na kusababisha gari kula tairi upande wa ndani. Usijaribu kufanya wheel alignment ukiona inakula tairi. Hilo sio tatizo la alignment. Tafuta hizo wishbone bushes ubadilishe. Hakikisha unaweka alama kwanza kabla ya kufungua wishbone, maana ukikosea kuzirudisha kwenye alignment tu unaharibu handling na litaboa kuendesha..
Hizi ni gari nzuri saana, ukizitunza unaweza kuzitumia kwa muda mrefu saana bila kukuletea shida yeyote. Na idadi yake sio kubwa, hivyo ukiwa nalo linakuwa unique kidogo. Ila kama unaishi sehemu yanye barabara mbovu, halikufai, hata kama wewe ni dereva mzuri. Utachoka kuliendesha.
Karibuni tupeane uzoefu.
hivi zile zenye antenna kwenye boot ndo hizo Gita?resale value ya gari zote ndogo zenye engine ya 2.0 ltr ni ndogo mno
kwa sababu mtu anafata gari ndogo ili apate fuel economic ila kwa altezza hutopata thats why unaona resale value ni ndogo the same na mark x na brevis and the likes
ukija kwenye resale value IST ipo juu kuliko mark x na tezza kwasababu ya fuel economic lakin hakuna tatizo kiufundi
chengine mkuu kwenye kununua altezza kama unataka isiyokula mafuta sana usidanganyike ukaenda kwenye 3S-GE I4 kisa eti ina cylinder 4 ukaacha 1G-FE I6 yenye cylinder 6 ukizani hii ya 6 ndio inakula mafuta
3S-GE I4 2.0 ltr hii inakula mafuta kuliko 1G-FE I4 2.0 licha ya kuwa hii 1G ni six na hyo 3S ni 4
sababu hyo 3S-GE yamaha waliitengeza kisport zaidi so piston room zake ni kubwa zaidi japo zipo nne kuliko zile za 1G zilizopo sita na hata kwenye power 3S-GE ina 210 bhp huku 1G-FE ikiwa na 160-180 bhp
so kama unataka altezza yenye unafuu wa mafuta usitishike na wingi wa cylinder chukua 1G-FE I6
ila kama unataka altezza yenye power chukua 3S-GE I4 kwa saloon na kwa GITA nenda kwenye badass machine 2JZ-GTE
Zile zenye kisogo ndio gita.hivi zile zenye antenna kwenye boot ndo hizo Gita?