Tozo Miamala ya Simu bado kimeumana

Tozo Miamala ya Simu bado kimeumana

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Alisikika Mh. Rais kuwa tozo kwenye miamala ya simu zimeridhiwa na wananchi kwa maslahi yao.

Mapema aliwahi kusikika Dkt. Mwigulu akisema tozo zenyewe ni ndogo tu.

Bila shaka msomi huyu alisahau kuwa chochote cha zaidi kwenye nyingi zilizopo, hakuufanyi mzigo wa tozo zote kwa watu kuwa mwepesi.




Kwamba bado kimeumana. Yuko wapi Mwigulu? Wako wapi wananchi walio zi-ridhia?

Wako wapi Mataga kuonyesha kwa vitendo namna ya kuunga mkono hoja mbili hizi?
 
Hameni Burundi Ila kwenye uchaguz mtaitwa tna msijal kofia zitatolewa bure bila kusahau buku7 daah sjui tatizo letu linaanzia Lindi vichwa havichaj
 
Hakuna anayekataa kulipa kodi, hata kwenye miamala tulikuwa tunalipa kodi, Tatizo ni pale tozo zinapokuwa kubwa kuliko uwezo wetu kuzimudu!

Mbaya zaidi:

IMG_20210812_095720_799.jpg


Mawaziri waachie Ngazi kutoa Nafasi kwa Mwanzo Mpya
 
Tunaambiwa Wanaisimamisha nchi"hatujui lini ililala' kwa Kutegemea tozo za simu, Walaji tumeshtuka kuna options tunazitumia na Maisha yanaendelea.

Hata wasipopunguza, waendelee tu na Kiburi chao cha Kutokutujali tuliowapigia kura. Time will tell..hakuna cha M-pesa wala Tigo Pesa Mchezo wao wa Kudharau Waajiri wao "Wapiga kura' Umekwama mazima.
 
Hameni Burundi Ila kwenye uchaguz mtaitwa tna msijal kofia zitatolewa bure bila kusahau buku7 daah sjui tatizo letu linaanzia Lindi vichwa havichaj

Umetuma double double rejea kujiridhisha kama ndiyo ilikuwa nia yako.

Unga mkono juhudi kwa kutuma miamala zaidi tafadhali.

😂😂😂😂

Soko limedorora!
 
Alisikika Mh. Rais kuwa tozo kwenye miamala ya simu zimeridhiwa na wananchi kwa maslahi yao.

Mapema aliwahi kusikika Dkt. Mwigulu akisema tozo zenyewe ni ndogo tu.

Bila shaka msomi huyu alisahau kuwa chochote cha zaidi kwenye nyingi zilizopo, hakuufanyi mzigo wa tozo zote kwa watu kuwa mwepesi.


View attachment 1889245

Kwamba bado kimeumana. Yuko wapi Mwigulu? Wako wapi wananchi walio zi-ridhia?

Wako wapi Mataga kuonyesha kwa vitendo namna ya kuunga mkono hoja mbili hizi?
Hawa kikundi cha utawala hawasikii maumivu yeyote ya tozo na kodi lukuki kwa watawaliwa bila kujali hali ya kipato. Ndiyo maana watu wote wakawekwa kapu moja bila kujali kipato. Watawala wanaishi "0" grazing kwa kodi za watawaliwa.

Usafiri gari na mafuta ni free, mawasiliano ni free, chakula free, nyumba na malazi free, maji free, umeme free, ulinzi free, wasaidizi nyumbani free, akitaka kwenda nje.ya nchi kwa kikazi au binafsi free nk.

Sasa hawa wabunge, mawaziri, ma RC, ma DC, na genge lote la watawala ukiwaambia tozo zinaua na ni maumivu makubwa hawakuelewi kabisa na wanatuona wachochezi.

Fikiria mtu mnyonge kabisa ana mtoto shule ya kata ila mbali na nyumbani na anakaa hukohuko kwenye bweni lililojengwa kwa nguvu za wananchi. Mzazi anauza kuku 1 tshs. 10,000/= anatuma kwa m pesa kwa mtoto ili apate matumizi. Mzazi anakatwa 750 hivyo zinabaki 9,250/= akituma mtoto anakatwa 1'750/=.

Hivyo muamala wote unakatwa 2,500/= na bakaa ni 7,500/= Kwa hawa wakubwa ni pesa kidogo sana, ila kwa mzazi na mwanafunzi ni balaa kabisa na ni kilio kwa familia yote.

Ongezeko la tozo za miamala kwa lengo la kuongeza makusanyo ya kodi ni jambo halikubaliki kabisa haswa kipindi hiki cha COVID 19 halikubaliki kabisa na ni kuua kabisa uchumi wa mwananchi mnyonge. Ila kwa vile watawala wameamua kutukomoa! No way out. But God is with us.
 
Hawa kikundi cha utawala hawasikii maumivu yeyote ya tozo na kodi lukuki kwa watawaliwa bila kujali hali ya kipato. Ndiyo maana watu wote wakawekwa kapu moja bila kujali kipato. Watawala wanaishi "0" grazing kwa kodi za watawaliwa...
Kuwasubiri kuwa watapata moyo wa huruma, ni sawa na kuwasubiri nzige wale shambani wakishiba wataondoka.
 
Wapo humu wanatuenjoy tu kuwa watalialia baadae watakaa kimya [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tunaambiwa Wanaisimamisha nchi"hatujui lini ililala' kwa Kutegemea tozo za simu, Walaji tumeshtuka kuna options tunazitumia na Maisha yanaendelea. Hata wasipopunguza, waendelee tu na Kiburi chao cha Kutokutujali tuliowapigia kura. Time will tell..hakuna cha M-pesa wala Tigo Pesa Mchezo wao wa Kudharau Waajiri wao "Wapiga kura' Umekwama mazima.

Bila shaka wanasimamisha uchumi wao kwanza chanzo muhimu tukiwa sisi
 
Back
Top Bottom