Tozo sasa miamala ya bank, sisi tuliokimbila bank tuhamie kwenye vyungu. Hatari sana wametufuata

MakinikiA

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2017
Posts
5,104
Reaction score
6,827
Wandugu hii nchi kama tumelaaniwa vile, zile tozo za kwenye simu sasa rasmi kwenye bank transaction zote ni balaa. Siku ya kufa nyani miti yote huteleza, najifikiria sasa bora bitcon kama zingekuwa kima cha chini, ukigeuka huku mfumuko wa bei, kule tozo .
 
Vyama vya wafanyakazi vimelala usingi wa pono na hali serikali inawa ibia wafanyakazi hii ni double tax
 
Ukikimbilia huku wanakujaaaaa ukienda kule wanakujaaa hadiiii wakumalize kabsaaaa uwe teja
 
Mkuu tozo ni bei gani sasahivi, last time ilikuwa buku 6!
 
Hivi wahasibu/ watu wa kodi hawana vyama vya kusemea hili maana imewagusa kwenye fani zao nao wapo km mabubu mibenki itakufa ujue.
 
"Mtanikumbuka kwa mazuri.. sio mabaya"

Hapa ndo kwanza unetimia mwaka mmoja mpaka ifike 2025 tutarajie kuona mengi
 
Hizo tozo ni hatari kabisa.

Ukitumia sim banking, ili uweze ku access account yako unakatwa tsh 100 halafu tozo nyingine ziendelee unapofanya miamala mingine.
Hiyo 100 ni kawaida haina madhara, ,sasa baada ya balaa hili nimehamisha 5000 imekatwa 4000 jumla 9000 kwa sasa hata, ATM,bank teller zinawekwa tozo rasmi kwa sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…