Tozo zinaweza kugeuka na kuwa wizi wa dola dhidi ya Wananchi

Tozo zinaweza kugeuka na kuwa wizi wa dola dhidi ya Wananchi

Uamzi wowote unaofanywa na Serikali sikivu ya awamu ya 6 unakuwa umefanyiwa tathmini ya athari zake vs faida..

Hakuna mtu anaweza kukata salary ya mfanyakazi kwa hivyo mnavyosema nyie,acheni kujitungia mambo ambayo hayana realistic Ili kutetea uzembe.
Ndugu The Sunk Cost Fallacy nani anatetea uzembe hapa? Ni mimi na wenzangu au wewe...?

Sisi tunakemea uzembe wa viongozi wa serikali yako ya CCM wa kutotumia akili zao vyema ktk kubuni njia sahihi za kuingizia mapato halali nchi kwa ajili ya maendeleo na badala yake wanatumia njia za wizi wa kidola kwa kuwaibia wananchi wake hela zao kwa jina la kodi au tozo kwa kisingizio cha "..ni kwa maendeleo ya wananchi..."

Tuna rasrimali nyingi sana. Lakini viongozi wa serikali yenu ya CCM akili zao zimekufa, hazifanyi kazi tena kwa sbb ya kulewa madaraka...

Hawajui ni kwa njia gani wanaweza ku - exploit rasrimali hizi, kisha ziwe converted kuwa fedha ili wazitumie kwa matanuzi yao ya anasa na familia zao...

Badala yake, wameamua kutumia "u - Magufuli" kuwaibia wananchi wao vihela kwa njia "double taxation...."

Hii siyo sahihi wala si haki. Hii haikubaliki ndugu The Sunk Cost Fallacy...!

Jaribu kuelewa hata kwa leo tu kisha jiunge na sisi ili kukemea tabia hii mbaya ya serikali hii...

Acha kujilambia asali itakayokwisha kesho na kusahau kesho kutwa na kizazi chako...!!

Think Big. Think about your children and grandchildren's future. Usidhani kuwa, kwa sababu wewe unashiba leo, basi na watoto wako watakuwa ktk hali hiyo. Never.

Kemea na pinga ubaya leo ili usiwaathiri watoto wa watoto wako huko mbeleni...!!
 
Ndugu The Sunk Cost Fallacy nani anatetea uzembe hapa? Ni mimi na wenzangu au wewe...?

Sisi tunakemea uzembe wa viongozi wa serikali yako ya CCM wa kutotumia akili zao vyema ktk kubuni njia sahihi za kuingizia mapato halali nchi kwa ajili ya maendeleo na badala yake wanatumia njia za wizi wa kidola kwa kuwaibia wananchi wake hela zao kwa jina la kodi au tozo kwa kisingizio cha "..ni kwa maendeleo ya wananchi..."

Tuna rasrimali nyingi sana. Lakini viongozi wa serikali yenu ya CCM akili zao zimekuwa, hazifanyi kazi. Hawajui ni kwa njia gani wanaweza wanaweza ku - exploit rasrimali hizi, ziwe converted kuwa fedha kisha wazitumie kwa matanuzi yao ya anasa...

Badala yake, wameamua kutumia "u - Magufuli" kuwaibia wananchi wao vihela kwa njia "double taxation...."

Hii siyo, haikubaliki. Jiunge na sisi, acha kukamua asali itakayokwisha kesho na kusahau kesho kutwa na kizazi chako...!!
Ku extract rasilimali inatakiwa pesa na pesa ndio hizi zinapatikana kwa njia nyingi ikiwemo tozo..

Acheni ubinafsi na upuuzi usio na msingi lipa tozo Kazi iendelee
 
Wewe ndio mpumbavu kwa kujenga hoja Kwa kufanya reference ya Waziri unaemtaja..

Tuambie basi wewe hizi tozo ni Kwa ajili gani Ili na mimi nikuwekee ushahidi wa nachosema..

Mwisho CCM kushindwa miaka mingine haimaanishi itashindwa na leo,Leo Rais ni Mwanamama na miaka hiyo Marais walikuwa Wanaume ambao kwa hulka huwa ni wezi..

Nasisitiza Rais Samia ataweza hayo ndio maana mwaka mmja tuu kajenga vituo vya afya 252,taja Rais mwingine aliyewahi weza?

Rais Samia Ataweza ndio maana mwaka mmja huu kahamisha bajeti ya barabara Vijijini kutoka bil.252 hadi bil.802 Ili kutimiza hiyo azma..

Rais Samia ataweza ndio maana kwa mwaka mmja Katia bajeti ya Maji kutoka bil.334 hadi bil.787 na maelfu ya miradi inaendelea..

Hivyo hivyo na sekta zingine zote kama kilimo nk..So Usilete ujinga wa kujenga hoja yako kwa failures.
Hivi hivyo vituo vya afya vimejengwa wapi?
Mbona huku nilipo nimetembelea kata tano na zote hazina vituo vya afya?
 
Hivi hivyo vituo vya afya vimejengwa wapi?
Mbona huku nilipo nimetembelea kata tano na zote hazina vituo vya afya?
Huko wapi? Kutaje Ili tuone kwenye list..

Hata hivyo Tanzania ina kata zaidi ya 3,950 na Kati ya hizo vituo vya afya kwa ujumla wake havizidi 1,200 Nchi nzima so hapo unaweza ona kwamba zaidi ya nusu ya kata hazina so Kazi bado kubwa ya kufanya.

Ila cha kufahamu ni kwamba hakuna Jimbo ambalo hakuna Kituo Cha afya walau kimoja au viwili vinajengwa..

Mfano soma hapa 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220812-104841.png
    Screenshot_20220812-104841.png
    268.4 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220812-104856.png
    Screenshot_20220812-104856.png
    259.9 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220723-121202.png
    Screenshot_20220723-121202.png
    107.8 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220719-085937.png
    Screenshot_20220719-085937.png
    143 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220713-194118.png
    Screenshot_20220713-194118.png
    155.5 KB · Views: 2
Ku extract rasilimali inatakiwa pesa na pesa ndio hizi zinapatikana kwa njia nyingi ikiwemo tozo..
Mimi ni mkristo ndugu The Sunk Cost Fallacy. Sijui wewe ni dini gani...

Katika biblia 1 Yoh. 5:17 imeandikwa hivi..

"..kila LISILO HAKI ni dhambi, na iko dhambi isiyo ya mauti..."

Ni sawa wanapata pesa. Lakini wanaipata kwa njia ya haki...?

Unajua ukiniibia mimi pesa, utakuwa umepata pesa na utaitumia kwa mambo yako na utatamba mitaani kuwa umeula, umetajirika...

Lakini unapotamba umejenga nyumba lakini kwa fedha ya wizi, wewe mwenyewe ktk nafsi yako utakuwa unajisikiaje...?

Ni wazi utakuwa unahukumiwa, au siyo. Utakuwa una nyumba, NDIYO....

akini hukuipata kwa njia halali. Umeipata kwa wizi. Utaudanganya umma lakini nafsi haidanganyiki...!!

Ndicho inachofanya serikali yako. Inaibia wananchi wake kwa hoja kuwa ni kwa maendeleo yao...

Hii siyo HAKI. Ni laana kuwaibia wasionacho na masikini..


Acheni ubinafsi na upuuzi usio na msingi lipa tozo Kazi iendelee
Wewe na wenzako huko serikalini ndiyo muache ujinga, upuuzi na uzembe wa kutofikiri vyema...!

Tumieni akili zenu alizowapa Mungu bure kabla hajawanyang'anya hizo akili ndogo mlizobakisha kabisa pamoja na vyote kurekebisha makosa haya...

Mungu anawaona eti. Mungu hajalala eti. Msifikiri Mungu hawezi kuweka watu wengine kuiongoza nchi hii na watu wake..

Waambie wenzake, wasije kulalamika kuwa hatukuonywa...!
 
ilimradi maendeleo tanayaona hakuna shida kabisaaa......tozo iendelee tena nashauri ziangaliwe njia nyingine za kuchangia maendeleo yetu, badala ya kuchangia harusi na masharehee mengine sasa tunaweza kuchangia 1200 maendeleo ya barabara zetu, hospitali, maji n.k

Mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe.
tusitegemee kujengewa nchi yetu na mataifa mengine.

wala tusifikirie eti jinsi awamu ya 1 hadi ya 6 walivyo ongoza lazima ifanane na awamu hii ya 5, kila kiongozi anamaono yake ya kutuletea maendeleo.

Tutaendelea kulipa tozo bila shida yoyote.
 
Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za serikali. Hii ni kanuni mama ya kodi.

Kanuni kuu ya pili, mapato yaliyokwishalipiwa kodi, tozo au ushuru hayastahili kulipishwa tena kwa mara ya pili. Double taxation inazuiwa.

Wizi ni kuchukua kitu chochote ambacho siyo stahili yako. Wizi huu unaweza kuwa wa mtu mmoja dhidi ya Serikali, taasisi, mtu mwingine au kikundi au serikali dhidi ya wananchi wake au dhidi ya mwananchi mmoja.

Serikali inapomtoza mwananchi kodi zaidi ya kiwango halali au zaidi ya mara moja kwa mapato yale yale, huo ni wizi wa dola dhidi ya mwananchi.

Maswali muhimu ya kujiuliza:

1) Kwa mfano, mfanyakazi au mfanya biashara amepata mshahara au pesa ya mauzo, ameilipia kodi tayari, ikawekwa benki, benki amelipia gharama ya huduma, na benki inalipa kodi kwa mapato yanayotokana na utoaji huduma, huyu mteja anapotaka kuichukua pesa yake, akatozwa tena na serikali, ni mapato gani ameyapata kule benki?

2) Kwa mfano, mfanyakazi, kwenye mshahara wake amekatwa PAYE, pesa imeenda benki, anatoa kwenye ATM, anakatwa kodi kwa mara ya pili, anaweka kwenye simu, pesa ile ile anaituma kwa mama yake kijijini anakatwa kodi, mama yake anaenda kwa wakala kuchukua ile pesa, anakatwa kodi.

Pesa siyo chakula, lazima huyu mama ataitumia, anaenda kununua chumvi anakatwa kodi. Yaani makato mara 5 kwa mapato yale yale, hii ni halali? Lakini ikumbukwe kwamba, benki kutokana na mapato yake yanayotokana na utoaji huduma imekatwa kodi, mtandao wa simu kutokana na mapato ya utoaji huduma ya usafirishaji fedha, nao umekatwa kodi, na muuzaji wa chumvi naye amekatwa kodi.

Tax regime ya Tanzania ni lazima iangaliwe upya. Siyo regime rafiki kwa wananchi wala wawekezaji.

Siku zote kodi utitiri au kubwa huua uwekezaji. Hakuna nchi hata moja duniani iliyokuwa maskini ambayo iligeuka kuwa tajiri kwa haraka kwa kuwa na kodi utititiri au kodi kubwa.

Dubai, ilipata maendeleo makubwa, na kubadilika kabisa ndani ya miaka 15 tu kwa kufuta kabisa kodi nyingi na kubakia na kodi chache sana. Mpaka leo Dubai ni kituo cha biashara duniani.

Anayehamasisha Tanzania kuwa na kodi utitiri na kodi kubwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu.

Nchi hii inahitaji sana uwekezaji ili watu wetu wapate ajira, na serikali iwe na vyanzo vingi vya mapato, na siyo kuongeza kodi kwa vyanzo vile vile.

Wazalendo wa nchi hii, wanaoitakia mema Tanzania tukatae mambo yote yanayoua uwekezaji katika taifa letu.

Tukiwa na sera na sheria ambayo inachochea uwekezaji kivitendo, kama uwekezaji utasababisha japo watanzania milioni 15 kupata ajira za uhakika, na hao milioni 15 angalau kila mmoja kwa wastani akalipa kodi ya sh milioni 4 kwa mwaka, PAYE pekee yake itaipatia Serikali 4,000,000×15,000,000 = 60,000,000,000,000 (trillion 60).

Haya ni mapato ambayo ni karibu 50% ya makusanyo ya serikali kwa sasa. Na haya ni mapato ambayo serikali itayapata, na huku mlipa kodi akifurahi kwa kuwa ana ajira inayompa kipato cha uhakika.
Kwa hizi facts, Kibatala & co. wangekuwa wazalendo wangeiburuza serikali mahakamani ili kuwatetea watu wa kipato cha chini waliotoa jasho la damu kuwawezesha kupata hiyo elimu ya sheria waliyo nayo.
 
Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za serikali. Hii ni kanuni mama ya kodi.

Kanuni kuu ya pili, mapato yaliyokwishalipiwa kodi, tozo au ushuru hayastahili kulipishwa tena kwa mara ya pili. Double taxation inazuiwa.

Wizi ni kuchukua kitu chochote ambacho siyo stahili yako. Wizi huu unaweza kuwa wa mtu mmoja dhidi ya Serikali, taasisi, mtu mwingine au kikundi au serikali dhidi ya wananchi wake au dhidi ya mwananchi mmoja.

Serikali inapomtoza mwananchi kodi zaidi ya kiwango halali au zaidi ya mara moja kwa mapato yale yale, huo ni wizi wa dola dhidi ya mwananchi.

Maswali muhimu ya kujiuliza:

1) Kwa mfano, mfanyakazi au mfanya biashara amepata mshahara au pesa ya mauzo, ameilipia kodi tayari, ikawekwa benki, benki amelipia gharama ya huduma, na benki inalipa kodi kwa mapato yanayotokana na utoaji huduma, huyu mteja anapotaka kuichukua pesa yake, akatozwa tena na serikali, ni mapato gani ameyapata kule benki?

2) Kwa mfano, mfanyakazi, kwenye mshahara wake amekatwa PAYE, pesa imeenda benki, anatoa kwenye ATM, anakatwa kodi kwa mara ya pili, anaweka kwenye simu, pesa ile ile anaituma kwa mama yake kijijini anakatwa kodi, mama yake anaenda kwa wakala kuchukua ile pesa, anakatwa kodi.

Pesa siyo chakula, lazima huyu mama ataitumia, anaenda kununua chumvi anakatwa kodi. Yaani makato mara 5 kwa mapato yale yale, hii ni halali? Lakini ikumbukwe kwamba, benki kutokana na mapato yake yanayotokana na utoaji huduma imekatwa kodi, mtandao wa simu kutokana na mapato ya utoaji huduma ya usafirishaji fedha, nao umekatwa kodi, na muuzaji wa chumvi naye amekatwa kodi.

Tax regime ya Tanzania ni lazima iangaliwe upya. Siyo regime rafiki kwa wananchi wala wawekezaji.

Siku zote kodi utitiri au kubwa huua uwekezaji. Hakuna nchi hata moja duniani iliyokuwa maskini ambayo iligeuka kuwa tajiri kwa haraka kwa kuwa na kodi utititiri au kodi kubwa.

Dubai, ilipata maendeleo makubwa, na kubadilika kabisa ndani ya miaka 15 tu kwa kufuta kabisa kodi nyingi na kubakia na kodi chache sana. Mpaka leo Dubai ni kituo cha biashara duniani.

Anayehamasisha Tanzania kuwa na kodi utitiri na kodi kubwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu.

Nchi hii inahitaji sana uwekezaji ili watu wetu wapate ajira, na serikali iwe na vyanzo vingi vya mapato, na siyo kuongeza kodi kwa vyanzo vile vile.

Wazalendo wa nchi hii, wanaoitakia mema Tanzania tukatae mambo yote yanayoua uwekezaji katika taifa letu.

Tukiwa na sera na sheria ambayo inachochea uwekezaji kivitendo, kama uwekezaji utasababisha japo watanzania milioni 15 kupata ajira za uhakika, na hao milioni 15 angalau kila mmoja kwa wastani akalipa kodi ya sh milioni 4 kwa mwaka, PAYE pekee yake itaipatia Serikali 4,000,000×15,000,000 = 60,000,000,000,000 (trillion 60).

Haya ni mapato ambayo ni karibu 50% ya makusanyo ya serikali kwa sasa. Na haya ni mapato ambayo serikali itayapata, na huku mlipa kodi akifurahi kwa kuwa ana ajira inayompa kipato cha uhakika.
Madhara ya hii tozo ya benki bado kidogo tu yataanza kuonekana Sasa hivi wengi wanatoa pesa zao benki wanapeleka nyumbani na wenye frdha nyumbani hawapeleki benki fedha zinaondoka kwenye mzunguko baadae benki zitaathirika kwani kazi ya benki ni kutunza hela na kuzifanyia biashara na kutoa gawio kwa Serikali in the long run madhara yatakuwa wazi
 
Hii nchi ina laana.
Akili ndogo ndio wanaopanga mikakati ya nchi na watanzania tukiwa tumelala. Sisi si tulikubali kuwa wanyonge. Tutaendelea kunyonywa
Sio lazima kusoma uwe kiongozi ,ishu kubwa Ni talanta ya kuingiza Basi. Sasa saivi hatutaki wenye elimu kubwa hata cheti Cha fomu Foo vya miaka mitatu kwa pamoja vinakubalika.
Kila mwaka c zako na d ama na f kadhaa balansi zinajumlishwa kwa pamoja
 
Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za serikali. Hii ni kanuni mama ya kodi.

Kanuni kuu ya pili, mapato yaliyokwishalipiwa kodi, tozo au ushuru hayastahili kulipishwa tena kwa mara ya pili. Double taxation inazuiwa.

Wizi ni kuchukua kitu chochote ambacho siyo stahili yako. Wizi huu unaweza kuwa wa mtu mmoja dhidi ya Serikali, taasisi, mtu mwingine au kikundi au serikali dhidi ya wananchi wake au dhidi ya mwananchi mmoja.

Serikali inapomtoza mwananchi kodi zaidi ya kiwango halali au zaidi ya mara moja kwa mapato yale yale, huo ni wizi wa dola dhidi ya mwananchi.

Maswali muhimu ya kujiuliza:

1) Kwa mfano, mfanyakazi au mfanya biashara amepata mshahara au pesa ya mauzo, ameilipia kodi tayari, ikawekwa benki, benki amelipia gharama ya huduma, na benki inalipa kodi kwa mapato yanayotokana na utoaji huduma, huyu mteja anapotaka kuichukua pesa yake, akatozwa tena na serikali, ni mapato gani ameyapata kule benki?

2) Kwa mfano, mfanyakazi, kwenye mshahara wake amekatwa PAYE, pesa imeenda benki, anatoa kwenye ATM, anakatwa kodi kwa mara ya pili, anaweka kwenye simu, pesa ile ile anaituma kwa mama yake kijijini anakatwa kodi, mama yake anaenda kwa wakala kuchukua ile pesa, anakatwa kodi.

Pesa siyo chakula, lazima huyu mama ataitumia, anaenda kununua chumvi anakatwa kodi. Yaani makato mara 5 kwa mapato yale yale, hii ni halali? Lakini ikumbukwe kwamba, benki kutokana na mapato yake yanayotokana na utoaji huduma imekatwa kodi, mtandao wa simu kutokana na mapato ya utoaji huduma ya usafirishaji fedha, nao umekatwa kodi, na muuzaji wa chumvi naye amekatwa kodi.

Tax regime ya Tanzania ni lazima iangaliwe upya. Siyo regime rafiki kwa wananchi wala wawekezaji.

Siku zote kodi utitiri au kubwa huua uwekezaji. Hakuna nchi hata moja duniani iliyokuwa maskini ambayo iligeuka kuwa tajiri kwa haraka kwa kuwa na kodi utititiri au kodi kubwa.

Dubai, ilipata maendeleo makubwa, na kubadilika kabisa ndani ya miaka 15 tu kwa kufuta kabisa kodi nyingi na kubakia na kodi chache sana. Mpaka leo Dubai ni kituo cha biashara duniani.

Anayehamasisha Tanzania kuwa na kodi utitiri na kodi kubwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu.

Nchi hii inahitaji sana uwekezaji ili watu wetu wapate ajira, na serikali iwe na vyanzo vingi vya mapato, na siyo kuongeza kodi kwa vyanzo vile vile.

Wazalendo wa nchi hii, wanaoitakia mema Tanzania tukatae mambo yote yanayoua uwekezaji katika taifa letu.

Tukiwa na sera na sheria ambayo inachochea uwekezaji kivitendo, kama uwekezaji utasababisha japo watanzania milioni 15 kupata ajira za uhakika, na hao milioni 15 angalau kila mmoja kwa wastani akalipa kodi ya sh milioni 4 kwa mwaka, PAYE pekee yake itaipatia Serikali 4,000,000×15,000,000 = 60,000,000,000,000 (trillion 60).

Haya ni mapato ambayo ni karibu 50% ya makusanyo ya serikali kwa sasa. Na haya ni mapato ambayo serikali itayapata, na huku mlipa kodi akifurahi kwa kuwa ana ajira inayompa kipato cha uhakika.
Mkiambia serikali hii haifai mnamsifia eti ana upiga mwingi!!!! Seriously?
 
Nashauri Kodi ziongezeke zaidi kwani ni kwa Maendeleo yetu wana wa nchi
 
Nashauri Kodi ziongezeke zaidi kwani ni kwa Maendeleo yetu wana wa nchi
Kodi inabidi ziwe rafiki,ziwafanye watu walipe
Ukiweka makodi ambayo yatamuumiza mfanyabiashara/watu
Utafanya watu waingie kwenye kufanya mambo ndivyo sivyo
We unafikiri kwanini watu wanafanya biashara za magendo!

Kingine,unaweza mtoza watu kodi za biashara zao,wakati wao hawana uwezo wa kulipa kiasi cha kodi ulichowapangia...mwisho wa siku anaacha biashara,sasa hapo utakuwa umemjenga au kumbomoa

Hao wanaolipisha makodi na matozo je wanafanya nini kuwainua watu kiuchumi wawe na fedha,je wanafanya hilo

Ova
 
Mtapiga makelele wewe ila come 2025 mtakapokuta kila Kijiji kina maji,kina barabara,kina Zahanati na vituo vya afya ,kina umeme nk mtajua kwamba kumbe mlikuwa wajinga.
Maisha ni leo siyo mwaka 2025. Wengi wanatafuta kuishi leo siyo kesho. Tozo zaidi ya 1% kwa muamala siyo sahihi. Benki nyingi za biashara zinatoa asilimia 4 tu- huku pesa yako imekaa mwaka mzima. Lazima watu wenye uwezo mdogo wasaidiwe na serikali kupunguza ukali wa maisha - vitu vingi vimepanda bei. Watu wana njaa leo siyo 2025. Huu mtazamo wa 2025 bila kujali maisha ya leo - si sahihi.
 
Maisha ni leo siyo mwaka 2025. Wengi wanatafuta kuishi leo siyo kesho. Tozo zaidi ya 1% kwa muamala siyo sahihi. Benki nyingi za biashara zinatoa asilimia 4 tu- huku pesa yako imekaa mwaka mzima. Lazima watu wenye uwezo mdogo wasaidiwe na serikali kupunguza ukali wa maisha - vitu vingi vimepanda bei. Watu wana njaa leo siyo 2025. Huu mtazamo wa 2025 bila kujali maisha ya leo - si sahihi.
Mjadala wa tozo umefungwa
 
Back
Top Bottom