TP Mazembe rasmi waaga mashindano ya Klabu Bingwa CAF, Yanga SC na hesabu za Calculator kufuzu Robo Fainali

TP Mazembe rasmi waaga mashindano ya Klabu Bingwa CAF, Yanga SC na hesabu za Calculator kufuzu Robo Fainali

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Klabu ya TP Mazembe imeshindwa kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF) mwaka huu baada ya kufungwa bao 1-0 na MC Alger katika mchezo uliochezwa usiku wa Januari 10.
IMG_2453.jpeg
Timu hiyo ya DR Congo kwa sasa ina alama 2 baada ya mechi 5, na haina nafasi yoyote ya kusonga mbele hata kama itashinda mchezo wake wa mwisho.

Msimamo Kundi A
IMG_2455.jpeg
Huku pia Klabu ya Yanga ikikabiliwa na mechi ngumu ugenini siku ya Jumapili, Januari 12 dhidi ya Al Hilal SC waliokata tiketi ya kucheza robo fainali katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Stade de la Capitale huko Nouakchott, Mauritania saa 4:00 Usiku.
IMG_2454.jpeg
Wananchi wanatakiwa kushinda mbele ya Wababe hao wa Sudan ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu Robo Fainali CAF kabla ya kukutana na MC Alger, Benjamin Mkapa Januari 18 kwenye mechi ya mwisho ya kujua hatma yao.

Pia, Soma: FT: MC Alger 1-0 TP Mazembe | CAF Champions League | Stade de 5 Juillet | 10.01.2025
 
Wakiwa kambini huku wakiomba dua na kuchoma ubani wengine wakiimba tenzi za rohoni, usinipite mwokozi kuiombea dua TP Mazembe iifunge MC Alger mambo yakaenda kinyume

Mmoja wa viongozi wa Yanga aliangua kilio kulichoambatana na kwikwi akijua safari imeishia hapo na morali ya wachezaji imepotea ghafla.

Tuwaombee
 
Wengi wetu tulishangazwa na biashara ya kalikuleta kushamiri jijini dar na mikoani mwanzo tulijua ni wafanyabiashara waliotaka kurahisisha mahesabu yao,pili tukafikiri ni wanafunzi lakini tukaona wanataka kalikuleta yeyote sio kama tulivyozoea wanafunzi hupendelea zaidi sayantifiki,

Cha zaidi ni leo na jana kila mmoja na bado wapo vikundi vikundi ndipo jamaa akatusanua zaidi hii imeletwa na matokeo ya jana usiku ni kuwa kesho yanga pamoja na kuoga lakini haendi mjini sisi wafanya biashara wa kalikuleta tumefurahi kwa biashara yetu kutoka mpaka kesho jioni Alhilal 2-1 yanga je hapa hata kwa hizo kalikuleta zitasaidia nini?

Mungu ibariki yanga ifungwe 2-1 itoke kelele ziishe!
 

Attachments

  • 20250111_080005.jpg
    20250111_080005.jpg
    379.6 KB · Views: 3
Yanga anahitaji tu kushinda kwenye mechi yake ya kesho. Hana namna nyingine. Kwenye mechi ya awali alikuwa na uwezo wa kushinda au hata kutoa sare! Ila katika hali ya kustaajabisha, alipoteza! Tena kwenye uwanja wake wa nyumbani.
 
Wakiwa kambini huku wakiomba dua na kuchoma ubani wengine wakiimba tenzi za rohoni, usinipite mwokozi kuiombea dua TP Mazembe iifunge MC Alger mambo yakaenda kinyume

Mmoja wa viongozi wa Yanga aliangua kilio kulichoambatana na kwikwi akijua safari imeishia hapo na morali ya wachezaji imepotea ghafla.

Tuwaombee
Wenye Akili tunajua kuwa Safari yao ndiyo imeshakwisha rasmi.
 
Wakiwa kambini huku wakiomba dua na kuchoma ubani wengine wakiimba tenzi za rohoni, usinipite mwokozi kuiombea dua TP Mazembe iifunge MC Alger mambo yakaenda kinyume

Mmoja wa viongozi wa Yanga aliangua kilio kulichoambatana na kwikwi akijua safari imeishia hapo na morali ya wachezaji imepotea ghafla.

Tuwaombee
Kwamba kufungwa kwa MCA kungemsaidiaje Yanga? Kila mtu ashinde mechi zake
 
Wakiwa kambini huku wakiomba dua na kuchoma ubani wengine wakiimba tenzi za rohoni, usinipite mwokozi kuiombea dua TP Mazembe iifunge MC Alger mambo yakaenda kinyume

Mmoja wa viongozi wa Yanga aliangua kilio kulichoambatana na kwikwi akijua safari imeishia hapo na morali ya wachezaji imepotea ghafla.

Tuwaombee
Sawa, kila mtu ashinde mechi zake
 
Back
Top Bottom