TPA yahamishia shughuli zake Dodoma

TPA yahamishia shughuli zake Dodoma

Sasa kuna ulazima gani Operation za Bandari iliyo Dar Ofisi zipelekwe Dodoma ni akili ?

Tena kipindi hiki cha ki-dijitali wizara ya uchukuzi na ujenzi kama wanataka taarifa zozote wangeweza kuwa na vikao vya zoom n.k na uongozi za TPA uliopo Dar es Salaam badala ya kuhamishia baadhi ya shughuli za kiofisi za TPA kwenda Dodoma.

Muonekano wa operesheni za kazi ktk bandari ya Dar es Salaam, Tanzania


Bandari ya Dar es Salaam, Tanzania
Source : Cloudsmedia
 
Rais William S. Ruto arejesha huduma za bandari Mombasa



Hiyo ni baada ya baadhi ya huduma zilizokuwa vikitolewa pwani kupelekwa bara, Naivasha. Hali hiyo ilisababisha zogo kubwa baina ya serikali ya Uhuru Kenyatta na washika-dau (stakeholders) kama kampuni za clearing and forwarding, wananchi wa pwani waliokuwa wanafaidi mnyororo wa fedha kutokana na shughuli kuwepo pwani

13 September 2022

Rais William Ruto amesema ahadi yake ya kurejesha shughuli za utaratibu wa kutoa bidhaa katika bandari ya Mombasa.

Ruto amefichua kwamba atatoa maagizo zaidi kuhusu utendakazi wa bandari ya Mombasa ili kuwezesha urahisi wa kufanya biashara na kuinua uchumi wa Mombasa.

Uhamishaji wa shughuli za bandari hadi Bandari Kavu ya Naivasha ilikuwa ajenda kuu wakati wa kampeni.

"Mchana wa leo, nitakuwa nikitoa maagizo ya kuondoa bidhaa na majukumu mengine ya kiutendaji katika bandari ya Mombasa kama nilivyotoa ahadi kwa Wakenya. Hii itarejesha maelfu ya kazi katika jiji la Mombasa," alisema.
 
Back
Top Bottom