Kamati ya masaa 72 ya TFF imepanga kuwaita wachezaji wa Yanga na kuwahoji iwapo ni kweli timu hiyo ina njaa au wanakula kwa siri. Hatua hiyo ni baada ya wachezaji wa Yanga kufunga magoli kwa umbali wa zaidi ya mita 40 yakiwa na mwendo kasi wa 160KM/HR. Magoli yaliyoiponza Yanga mpaka kufikishwa kwenye kamati hiyo ni magoli ya Ibrahim Ajib na lile la Faisal Salum kwenye mechi ya Yanga dhidi ya Mwadui Fc. Na pia kamati hiyo ya masaa 72 inatafakari goli la tambwe baada ya kuruka juu na kukaa kama dk moja na kupiga kichwa kilisababisha kipa wa mwadui kutaka kuvunjika nyonga na kuacha mpira uende nyavuni🤣🤣🤣🤣🤣