TPL: Simba SC vs Yanga SC - Sept 30, 2018 (FT: 0-0)

Mkuu sembo nimeondoka hapo napitia barabara ya Mandela hadi Kigamboni

Ila mchezo wa leo kuna mengi ya kujiuliza aisee
Ni kweli Mkuu ... Hawa Ndala hawaba pakutokea tena. Tutaanza nao Muungano kama wakifanikiwa.
 
Dah,
Manake Draw hapa ni kuanzia 3.5 kwa game tatu kisha ukatia hata 10,000 hukosi laki 5 aisee,
Embu nitabirie zijazo bas kaka nimpige kanji
Mkuu hizo za ulaya sikutabiri japo ya Chelsea jana imenipa supu nilichez inplay baada ya Chelsea kupata goli,droo ilikuwa na odds 3.3 Kwa kutumia matokeo ya Timu za Ulaya nikaotea na Derby ya Kariakoo nikajua tu kuwa nyota ya weekend inafanana kote
 
'Kama Huwezi shinda, usipigwe' - Zahera
'Wachezaji wengi walipotea sababu tulibadiri tactic, hili ni tatizo kwa Wachezaji Naona huku' - Zahera
'Mechi ya Coastal Ngassa alipotea vile tulibadiri tactic, leo Ajib na Kaseke wakapotea, mchezaji wa Duniani inatakiwa ufanye vile unaambiwa na kufanya kazi, ni kama unafanya copy' - Zahera
'Tulipanga tuwaachie mpira, inatakiwa ukimuachia mipira ukipata kimbia sana, lkn problem Ajib, Kaseke wakipata mipira wanatembea' - Zahera
'Tuliwaambia vile Simba wanacheza watajaa kati kati hivyo Tuliwaambia Ajib, Kaseke na Tshishimbi wajae Ndani wawe wanakimbia ndani na kufunga' - Zahera
'Niliwatoa Ajib na Kaseke kwa sababu walishindwa kufuata vile tumeongea na kukubaliana'- Zahera

Hapa Yanga kocha tumepata
 
Unaomboleza wengine wanashangilia droo. Tupo tofauti mkuu..!
Shukuruni hata Kwa hicho kidogo,nyie hamjui Historia ya Simba na Yanga.Timu moja hata iwe mbovu kiasi gani lakini ikifika Derby ubovu wa Timu moja Huwa hauipi guarantee Timu pinzani kushinda
 
Huu mkocha.. Mda wake wa kufanya kazi Tanzania unahesabika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…