TPLB yamfungia Kocha wa Yanga Nabi mechi 3 na faini laki 5 huku Simba SC, Azam FC, Coastal wakilimwa 1ml

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kocha wa Yanga Nabi Nasreddine amefungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya shilingi 500,000 (laki tano) na TPLB kwa kosa la kuwashambulia kwa maneno mwamuzi wa kati na mwamuzi wa akiba kwenye mchezo ambao Yanga walipigwa 2-1 dhidi ya Ihefu FC.

Kamati ya usimamizi wa Ligi Kuu TPLB imeitoza Klabu ya Simba Shilingi 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la baadhi ya wachezaji wake kuingia uwanjani kwa kupitia milango isiyokuwa rasmi kwenye mchezo ambao Simba SC walitoka sare ya moja kwa moja dhidi ya Mbeya City.

Mchezaji Gadiel Michael amefungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya shilingi 500,000 (laki tano) na TPLB kwa kosa la kulazimisha kuingia uwanjani saa 4: 25 asubuhi kwa kile alichoeleza alitaka kukagua Uwanja kuelekea mchezo wa Mbeya City dhidi Simba SC.

 
Nabi Nasreddine alistahiki kupata adhabu kwani hakuwa fair kwenye mchezo licha ya kuonywa kwa Kadi ya Njano.

Mambo ya kupitia milango isiyokuwa sahihi kila siku tunawalaumu Yanga sasa Simba yametoka wapi? Nani ameshauri hili jambo la hovyo..!
 
Nabi Nasreddine alistahiki kupata adhabu kwani hakuwa fair licha ya kuonywa kwa Kadi ya Njano.

Mambo ya kupitia milango isiyokuwa sahihi kila siku tunawalaumu Yanga sasa Simba yametoka wapi? Nani ameshauri hili jambo la hovyo..!
Kabisa. Hakufanya kitendo cha kiuungwana
 
Hizi faini kwa mkupuo namna hii haijawahi kutokea, haya sasa ndo mavuno kwa TFF.

1. Kocha Nabi laki tano.
2. Gadiel Michael laki tano.
3. Simba SC, milioni moja.
4. Azam FC milioni moja.
5. Coastal Union milioni moja.
6. Ruvu Shooting laki tano.
7. Mbeya City laki tano.
8. Mchezaji wa Coastal laki tano.
 
Nabi Nasreddine alistahiki kupata adhabu kwani hakuwa fair kwenye mchezo licha ya kuonywa kwa Kadi ya Njano.

Mambo ya kupitia milango isiyokuwa sahihi kila siku tunawalaumu Yanga sasa Simba yametoka wapi? Nani ameshauri hili jambo la hovyo..!
Kwa hiyo unataka kusema siku zote ulikuwa hujui Yanga na simba baba yao ni mmoja?
 
Hivi huwa wanazipeleka wapi hizi hela? Yaani matumizi yake yakoje, baada ya kulipwa?
 
Izi rekodi za mambo ya kichawi apa Nchini Simba inazishikilia Kwa mda mrefu sana na Kwenye mashindano ya Caf wanatisha Kwa shirki.
 
Nabi Nasreddine alistahiki kupata adhabu kwani hakuwa fair kwenye mchezo licha ya kuonywa kwa Kadi ya Njano.

Mambo ya kupitia milango isiyokuwa sahihi kila siku tunawalaumu Yanga sasa Simba yametoka wapi? Nani ameshauri hili jambo la hovyo..!
Sijui kwanini mpira wetu licha ya kuongozwa kwa sheria na taratibu lakini upo kama mpira wa mitaani, hizi sheria haziheshimiwi licha ya adhabu wanazopewa wavunja sheria kila mara.

Naona kuna mahala tunakwama, inaonekana hawa wachezaji wa ligi yetu bado hawajitambui, wapo wapo tu, ndio maana wengine wanaudharau huu mpira wetu.
 
Wacha TFF wavune tu, hawa jamaa hawaishiwi ujinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…