TRA kuvunja rekodi dhidi vifo vya biashara na viwanda,tujitafakari na kujirekebisha

TRA kuvunja rekodi dhidi vifo vya biashara na viwanda,tujitafakari na kujirekebisha

Hilo la kufutiwa input nina mashaka nalo, ts either risiti ni fake au uliyenunua kwake mashine yake haijatuma report.

Ukifuta manunuzi yangu ina maana umefuta mauzo ya aliyeniuzia. Unakuwa umefanya nini? Hapo TRA si atakuwa anajaza maji kwenye gunia?
Ndugu sheria inataka utunze electrical records na hard copy, nimekuwekea sheria yenyewe na ‘part IV’ ya sheria inayozungumzia records.

Hayo ni matakwa ya kisheria ambayo lazima uyajue kama mfanyabiashara kuna consequences kubwa kutofanya hivyo kwa nchi zinazojitambua. Ndio mambo wanayo angalia siku wahusika wakija kutafuta ushahidi.

Yeye huyo mwenyekiti wenu analalamika mamlaka ikija kutaka kupata ushahidi wa madai ya VAT, wafanyabiashara awatunzi records kama sheria inavyotaka na serikali yenu sikivu imemsikia imezuia.

Kuwapa nafasi watu wasio na uwezo huko serikalini kunafanya kazi ya TRA kuwa ngumu sana (pale wanapofuata sheria).
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Ndugu sheria inataka utunze electrical records na hard copy, nimekuwekea sheria yenyewe na ‘part IV’ ya sheria inayozungumzia records.

Hayo ni matakwa ya kisheria ambayo lazima uyajue kama mfanyabiashara kuna consequences kubwa kutofanya hivyo kwa nchi zinazojitambua. Ndio mambo wanayo angalia siku wahusika wakija kutafuta ushahidi.

Yeye huyo mwenyekiti wenu analalamika mamlaka ikija kutaka kupata ushahidi wa madai ya VAT, na serikali yenu sikivu imemsikia imezuia.

Kuwapa nafasi watu wasio na uwezo huko serikalini kunafanya kazi ya TRA kuwa ngumu sana (pale wanapofuata sheria).
Nyaraka ni muhimu ndio ila kwa bulk purchase siku hizi mambo ya kujaza makaratasi ofisini tunapunguza, unatumiwa invoice unalipa e-receipt inakuja, slip ipo, cheq number ipo makaratasi ya nini? Dunia inahama huko tusipang'ang'anie. VFD nazo ni automatic unabakiwa na copy tu kwenye simu ya ofisi.
 
Nyaraka ni muhimu ndio ila siku hizi mambo ya kujaza makaratasi ofisini tunapunguza, unatumiwa invoice unalipa e-receipt inakuja, slip ipo, cheq number ipo makaratasi ya nini? Dunia inahama huko tusipang'ang'anie. VFD nazo ni automatic unabakiwa na copy tu kwenye simu ya ofisi.
Provided unaweka records zote unazotakiwa kuwa nazo kama sheria inavyotaka na inawawezesha TRA kufanya kazi yao wakija huna shida.

Mwenyekiti wenu analalamika ni uonevu jamaa wakija wakikuta mtu ambae anamadai ya input VAT halafu hana ushahidi wa receipt za manunuzi na wala hataki kukaguliwa remaining stock ili TRA ijiridhishe. Yeye anataka walipwe tu serikali yenu sikivu imekubali.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Wakae chini kujifunza hesabu za biashara au serikali ianze kuhamasisha certified accountants kuanzisha huduma za kodi.

Yaani wewe CPA upate mshahara wa million mbili kwa mwezi wakati kuna fursa ya kuwakusanya wafanya biashara kwa fees ndogo na kutengeneza zaidi ya million 100 kwa mwaka kama ‘sole proprietor’ na target ya income ya billion ni possible kabisa.

Shida kubwa ni business plan za wafanyabiashara na uelewa wao mdogo wa maswala ya kodi.
Mimi nimetengeza dodoso linalowezesha kuandika business plan ukijibu maswali na kujaza jedwali business plan yako tayari
 
Provided unaweka records zote unazotakiwa kuwa nazo kama sheria inavyotaka na inawawezesha TRA kufanya kazi yao wakija huna shida.

Mwenyekiti wenu analalamika ni uonevu jamaa wakija wakikuta mtu ambae anamadai ya input VAT halafu hana ushahidi wa receipt za manunuzi na wala hataki kukaguliwa remaining stock ili TRA ijiridhishe. Yeye anataka walipwe tu serikali yenu sikivu imekubali.
Kuna maafisa wahuni pia, unatengenezwa.
 
Kuna maafisa wahuni pia, unatengenezwa.
Hilo alikwepeki duniani bad people will exist.

Ila ukiwa umejipanga na unajua wajibu wako ni ngumu sana kukutungia.

PS naelewa changamoto za babu Rama na mis justice za TRA hadi kujipiga risasi (so let’s not dwell on isolated extreme rare cases).
 
Hilo alikwepeki duniani bad people will exist.

Ila ukiwa umejipanga na unajua wajibu wako ni ngumu sana kukutungia.

PS naelewa changamoto za babu Rama na mis justice za TRA hadi kujipiga risasi (so let’s not dwell on isolated extreme rare cases).
Hapa kwetu si rare, tunawindana. TRA anamwinda mfanyabiashara na mfanyabiashara anajilinda asiliwe nyama. Ukikosea tu imekula kwako.
 
✅Sera nzuri Za biashara,Sheria rafiki Kwa biashara,Usimamizi Mzuri wa Sheria,Uadirifu wa maafisa kodi,Matumizi mazuri ya kodi..

✅Heshima Kwa walipa kodi (Wadogo Kwa wakubwa)..Sio dharau,kiburi,dhihaka,Kejeli na ubabe..

✅Elimu ya kina kwa walipa kodi..Haki,wajibu,majukumu,nidhamu..

✅Ubia endelevu kati ya walipa kodi na wa Kusanya kodi..

✅Incentives Kwa Walipa kodi-Hamasa..
 

Kwa Mtazamo wangu

TATIZO LA KARIAKOO NI ZAIDI YA WAFANYABIASHARA,WACHUUZI..LETS BE SERIOUS.

Tatizo la kariakoo haliwezi Kwisha ikiwa total supply chain ya mizigo inayouzwa kariakoo isiporekebishwa au kudhibitiwa kupitia maamuzi magumu na kutooneana haya wala aibu..

Bidhaa nyingi zinazouzwa kkoo zinaingizwa (Imported) toka China,India,Uturuki,Thailand,Vietnam,Zambia,Uganda,etc..Mfumo wa uingizaji na ulipiaji kodi wa mizigo husika ndio mzizi wa shida na tatizo lililopo na litakalokuwepo..

Cartel inayoratibu Logistics na supply chain ya mizigo ya wafanyabiashara wa karikoo isipodhibitiwa kila nyakati tutaona fukuto na migomo isiyohitaji siasa Bali utashi wa maamuzi magumu kudhibiti wahujumu uchumi tunaowalinda..

Mathalani,Mfanyabiashara akiagiza mzigo wa viatu Kwa kontena na kulipa ushuru stahiki kisha kuwa na nyaraka zote Za kikodi (Import duties,Port charges,Wharfage,VAT) inamgharimu milioni 45….NOTE:- Ila akiagiza mzigo huo huo kwa kutumia Logistics Cartels inamgharimu Milioni 15 tu pasipo nyaraka zozote lakini Ana uhakika wa kufikishiwa mzigo dukani au warehouse kwake pasipo usumbufu..

Sasa wale wafanyabiashara waliokuwa wakikomaa na kufuata taratibu stahiki wamejikuta wakishindwa kushindana ktk soko na kufirisika ama kufa kibiashara sababu ya ughali wa bidhaa dhidi ya wale wanaotumia Logistics Mafia..

On the other hand wanaotumia huduma za logistics cartel au mafia inawawia Vigumu sana kufanya compliance za kikodi sababu ya kukosa nyaraka muhimu kussuport mapana ya stock zao..Mauzo yao,returns zao..Hapa ndio kwenye shidaa haswaa…Wengi wana stock kubwa kuliko vielelezo vya manunuzi ya stock husika..Wamegeuka wachuuzi..Wanaouza ambacho hawana nyaraka Za wametoa wapi..SHIDA.

Logistics Cartel/Supply chain Mafia:-Ni kundi hatari lenye nguvu kupitia wanasiasa wakubwa waliopo na wastaafu..Wana ukwasi mkubwa na umaarufu mkubwa ktk Kiwango cha kuogopeka na Wakubwa wa TRA,Polisi,Etc..Wana nguvu mnooo ya kufanya wakubwa ktk mamlaka Za kodi watumbuliwe,Wafanyakazi wahamishwe,Wawe demoted..Wapate Stroke..Nina hakika hata CG wa TRA anawaogopa..Hana la kuwafanya..Inasemekana baadhi ya viongozi ni marafiki wakubwa..

Cartels hizi zimehodhi Supply chain Za uagizaji bidhaa,usafirishaji,Ulipaji kodi,Udanganyifu (under declaration&Falsa Declarations),Uzungushaji mizigo (Taarifa Za kampuni Za tracking devices Za mizigo ya transit zina mengi)..Wanamiriki makampuni ya uagizaji,Usafirishaji,Bonded Warehouses,ICD’s,CFS..yaani acha tu..

Kwa hakika tunapoteza kodi nyingi sana zinazoingia mifukoni mwa wachache tunaowaimbia mapambio ya utajiri na ubilionea huku wachache wakikamuliwa hata kuzirai kibiashara..Bila maamuzi magumu na dhabiti tutaendelea kukwama na kuumiza wasiostahili..

Tukiamua Tunaweza..Viongozi wenye dhamana Simameni kwenye haki na ukweli..
 
Back
Top Bottom