Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama ulikuwa unanufaika kwa nanna yeyote,wakati zikipitiamo sasa connection imeparaganyika,jipange upya update tena,connection huko ziliko hamia,usije kujiliza humu.Hili la TRA kuhamishia account za kenya commercial bank KCB toka bank ya kitanzania NMB jamani limekaa vipi? Jambo kama hili wakati wa magufuli lisingewezekana kabisa. Inaelekea mbinu za kifisadi wakenya kuhodhi uchumi tanzania zimeanza kufanikiwa tena. Watanzania hawana imani na wakenya. Ni jambo la kustaajabisha wananchi kuona mamlaka ya fedha TRA kuacha bank za nchini na kutumia bank ya kenya. Serikali ina hisa NMC na bank hiyo ni kubwa na yenye uwezo ila mbinu za hila za wakenya ndio zinawezesha uamuzi wa mamlaka kubwa ya serikali kama TRA kuweza kuacha kutumia bank ya nchini na kutumia bank ya nje. Jambo hili inafaa waziri wa fedha aingilie mara moja vinginevyo ataendelea kuwaudhi wananchi ambao wana wasiwasi juu ya uwezo wake.
Huyu jamaa ni kilaza sana hawa ndio walishikwa akili za udanganyifu wa mzee wanadhani kila kinachofanyika watu wanapiga dili.Tuna safari ndefu sana. Mabenki ni wakusanyaji tu wa mapato ya TRA yanayopelekwa BoT. Huko kwenye taasis za kifedha zinapita tu.
Hapo chini kwenye kiambatanishi inasoma to
Commissioner of customs and excise
TRA
BoT
Sasa hapo KCB analaumiwa kwa lipi?
Tukiambiwa malipo yote yafanyike kwa bank moja hizo foleni na ucheleweshwaji tutauvumilia?
Kama sijaelewa vizuri naomba kueleweshwa.
Soko huria mzeeSikia ndugu, serikali ina hisa 100% kwenye benki ya serikali iliyoitwa TPB bank (Tanzania Postal Bank) au Bank ya Posta ambapo kwa sasa inajulikana kama TCB (Tanzania Commercial Bank), sasa swali la kizushi ni kwamba kwanini huduma nyingi za kiserikali hazipitii bank hii ya serikali mfano mishahara ya watumishi wa umma na malipo mengine kadha wa kadha?
Kwamba ndiyo ma_facilitator wa kuondoka kwake yule wa 17/3?Kama ni kweli, inaanza kuyapa nafasi yale maneno ya chini chini juu ya wakenya.
We ni mkenya?Kama ulikuwa unanufaika kwa nanna yeyote,wakati zikipitiamo sasa connection imeparaganyika,jipange upya update tena,connection huko ziliko hamia,usije kujiliza humu.
Kwa kuwa mliaminishwa jirani yenu,ndio mbaya wenu au ipo hoja ya msingi zaidi ya hiyo.Ni ya kweli hayo? Kama ni kweli nafikiri litafanyiwa kazi maramoja.
Kwani hata Mimi tayari mnataka mwanze kunibagua?Kabila yangu ya nini?We ni mkenya?
Ww ndio hujui kitu, Tanzania Government ina NMB shares 31.8%. Next time kama hujui kitu, nyamaza!
![]()
NMB Bank Tanzania - Wikipedia
en.wikipedia.org
Na wewe? Yaani hujui kuwa serkali ina zaidi ya aslimia 30 ya hisa huko?Aliyekwambia NMB inamilikiwa na Tanzania nani?
Na wewe? Yaani hujui kuwa serkali ina zaidi ya aslimia 30 ya hisa huko?