TRA muda umepita wa kutoa "LIFETIME" "plate number" za magari, zilipiwe kila mwaka mtaondoa plate number fake nyingi

Hoja kama hii madelu akiiiona anatabasamu kinyama, maana ni mchumi first class asiyekuwa na ubunifu zaidi ya kubuni tozo mpya.
 
Chukulia Tshs 30,000 kwa mwaka, mara magari 1,000,000= Tshs 30,000,000,000 bila jasho zinaingia kila mwaka

"Bila jasho zinaingia kila mwaka"--- umesahau kwamba huyo atakayetoa hizo pesa naye kazipata kwa jasho.

DEC 2023 (hapa mtu hawezi endesha gari JAN 2024) anakutana na Trafiki anapigwa fine

Hicho ni kitendo cha kuongeza ugumu wa maisha kwa wenye magari, unataka kufanya mtu kumiliki gari iwe laana.
 
Hakuna plate number bhana wewe wamekuelewa kwa kuwa wanakuheshimu tuu ni number plate hata mimi nimejifunza tuu si unajua viingereza vimekuja na Meli hivi na wala sikucheki nakusahihisha...ila ukikomaa endelea kutumia hicho kiswahili ueleweke vizuri...
 
Wapunguze kwanza kodi ya Magari maana HAIWEZEKANI ununue gari Tsh 10M halafu ulipe kodi 12M.
 
Mh! Kwani vyanzo vingine vya mapato mfano madini, utalii na bandari vimeisha mpaka tuongeze tena tozo kwenye plate number?

Mimi nafikiri baada ya bandari kuuzwa, ni muda muafaka kodi ya magari ishuke ili Watanzania wanunue magari mazuri mazuri ya mapya au ya hivi karibuni.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Unakitu utfika mbali.
Huyu jamaa forcus yake ya kodi ipo kwa magari tu kuongezewa kodi
Nakumbuka kwenye moja ya posti zake ilikuwa magari yalipe shs 1000 kila mwezi iongezwe kwenye petrol
watu wengi wakachangia kuwa petrol tayari inakodi lukuki......nk hivyo ni bora atoke huko kwenye magari aje na ubunifu mpya!!!
 
Pata picha ndio anakuwa rais wa nchi. Yaani anashindwa kuelewa nchi hii ina rasilimali nyingi ambazo zikitumiwa vizuri nchi inapiga hatua mpaka kushusha kodi za magari ili Watanzania wengi waendeshe magari mazuri.

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…