ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
- Thread starter
-
- #21
Akiba hawezi pata ila on daily basis anapata.Hiyo hela ni kubwa sana hasa kwa bodaboda!
Kuna watu wanafunga mwaka hawana hata akiba ya 10000 na wamefanya kazi mwaka mzima.
Kuna sehemu tuliambiwa tulipe 3000 kwa mwezi huku uswahilini na bado watu hawapati hiyo hela, ambapo ni wastani wa shilingi 100 kwa siku.
Kuitoa 3000 kwa pamoja bila sababu zinazoeleweka ni ngumu sana kwa watu wa uchumi fulani.
Naungana nawe ila pia ela ya kodi kusikia inapgwa na wapigaji wapo tu si uzalendoHiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Kwaiyo kwakuwa bodaboda hawapigi kula ndo walipe Kodi?Rais Samia futa hili pendekezo linakuletea shida zisizo na sababu na bodaboda japo Huwa hawapigi kura.
Nawasaidia afadhari mafundi ujenzi wote wawe na leseni za ujenzi ndio walipe 100,000 Kwa mwaka.
Kuna siku moja nilikuwa naongea na jamaa mmoja Mtanzania anakaa Finland siku nyingi sana, kuhusu kodi.Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Na kodi zilizowekwa kwenye mafuta inahesabika wapi, huu sio ubunifuti kwa kutafuta mapatoBodaboda mmesikia hii? Sasa rasmi mtaanza kulipa Kodi. Hapa Serikali mmechemka na mnawaonea Bodaboda, maana kupata 20,000 kwa siku ni kazi kubwa.
----
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa katika mabadiliko ya Sheria za kodi mwaka 2023, serikali imeweka kodi ya mapato kwa wasafirishaji wa abiria kwa kutumia pikipiki zenye magurudumu mawili (Bodaboda) ambapo watatakiwa kulipa kiasi cha Sh. 65,000 kwa Mwaka.
Hayo yamesemwa jana na Afisa mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hamad Mterry, wakati akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu.
Mterry amesema kuwa hiyo ni moja ya sheria ya kodi ambayo ni mpya na imewagusa Bodaboda, ambapo watatakiwa kuichagia serikali kiasi cha Sh. 65,000 kwa mwaka, kuanzia mwaka huu wa fedha ambao tayari umeanza tangu Julai Mosi, 2023.
Afisa Mawasiliano na elimu kwa umma kutoka (TRA) Mkoa wa Simiyu, Benjamin John amesema kuwa Bodaboda anaweza kulipa kodi hiyo kwa awamu nne ndani ya mwaka, ambapo kila awamu atatakiwa kulipa Sh. 16,250.
Hata hivyo wafanyabiashara za kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki (Bodaboda) wanaona kodi hiyo inakwenda kuongeza ugumu wa maisha kwao, kutokana na kipato chao cha kila siku kuwa kidogo sana.
“ Ukizingatia kwa sasa kupata Sh. 10,000 kwa siku ni ngumu sana, lakini mafuta yamepanda bei, tunalipa LATRA, tunalipa Bima, bado familia inakutegemea, leo tumeletewa TRA, ukweli kodi hii inakwenda kutuumiza sana,” amesema Ntoni Deus.
My Take
Siungi mkono,Kwa nini pombe na Sigara zisiongezewe Kodi? Rais Samia umegombanishwa na Watu huku.
Kodi Huwa inakuwa ni ya kitu gani? Ukipata mapato lazima ulipe KodiHii ni kodi ya kitu gani???
shida sio kulipa Kodi, shida ni matumizi ya hizo Kodi. kuchangia mafisadi kunakera sana hata kama ni mia mbili.Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Cc Mpwayungu VillageKupata 10,000 kwasiku imekuwa shida tena situlikubaliana wanapata pesa kuzidi walimu tena wa degree au inakuwaje
Umeshawahi kuwa dereva bodaboda mpaka useme hicho kiwango ni kidogo?Hiyo kodi ya 65000 Kwa mwaka ni sawa na shilingi 200 Kwa siku. Ni kiwango kidogo mno lakini naamini wapotoshaji watakikuza sana na kuonesha uonevu. Uzalendo ni kuhamasisha watu kulipa Kodi Kwa maendeleo yao.
Ni Jambo Jema kwa hao bodaboda kuanza kulipa kodi.Rais Samia futa hili pendekezo linakuletea shida zisizo na sababu na bodaboda japo Huwa hawapigi kura.
Nawasaidia afadhari mafundi ujenzi wote wawe na leseni za ujenzi ndio walipe 100,000 Kwa mwaka.
[emoji23][emoji23]Wanafunzi nao waanze kulipa kodi, kuanzia ngazi ya shule ya msingi waanze kulipa kodi.