TRA tokeni maofisini kakagueni magari, mengi Mjini hayajalipiwa na mengine yana sticker za bima fake

Mbaya sana unalipia bima ya gari kila Mwaka kumbe unauziwa bima fake [emoji87][emoji87]

Unaibiwa hela yako !

Na ikitokea ajali unaambiwa bima yako fake haitambuliki jamaa alikuibia hela zako kwa miaka yote!

Au trafiki anakusimamisha anakwambia bima yako inaonesha ni ya Phonix lakini kiukweli siyo Phoenix badala yake inasoma Zanzibar Insurance,

Wakati huo kwenye kumbukumbu za Zanzibar Insurance haupo!

Kuna jamaa alinifanyia hivyo lakini bahati yake nilikuwa rohoni vinginevyo ningeshirikiana na polisi kumfikisha kwenye vyombo vya dola!

Tena ingekuwa rahisi sana tu!

Uniibie malaki yangu kila Mwaka halafu nikuache?

Kwa hiyo acheni kutetea uovu!
 
Road licence ilishafutwa. TRA hawahusiki na bima. Trafiki na TIRA ndio kazi yao labda waonganishe nguvu tu.

Unapokata bima insurance company anakatwa kodi kupitia hiyo premium. Kwaiyo TRA anahusika usipokata bima insurance company haipati premium hivyo kodi inakosekana
 
Wewe nawe sijui wamekunyima lift; TRA wanahusikaje na bima kwa mfano? Utapataje usajili wa gari bila kulipia? Road license ilifutwa na malipo gani mengine wenye magari wanatakiwa kulipa kutokana na huu udaku wako?
 
TRA malipo yao yaneunganishwa kwenye mafuta.
 
Inakukera nini mtu kuwa na bima fake wakati hata hupandi hilo gari na likipata tatizo anapambana na hali yako hategemei chochote kutoka kwako? Mkuu fanya yako achana na ya watu.
Akikugonga mtembea kwa miguu? Au akikugonga wakati una third party insurance? Bima fake inaathiri wengi ndio maana imawekwa third party insurance imlinde utakaemgonga, wewe ubaki upambane na hali yako
 
Unapokata bima insurance company anakatwa kodi kupitia hiyo premium. Kwaiyo TRA anahusika usipokata bima insurance company haipati premium hivyo kodi inakosekana

Pia wale wezi wanaoibia watu kwa njia ya bima fake wenyewe hawalipi kodi kupitia hayo malipo wanayopokea wakati pesa hiyo ingeenda kwenye mashirika ya bima halali wangelipia kodi stahiki.
 
Acha wivu wewe unawafundisha kazi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…