TRA wanavyomjaribu Rais Samia Suluhu

TRA wanavyomjaribu Rais Samia Suluhu

Mtakuwa mnabadilisha Wakuu mpaka kiama, Utitiri wa Kodi kubwa na Matozo yasioisha

Ujumbe wako watausoma..mbona miaka nenda rudi.. hautaki kukubali kwamba mimi sipo huko.. ni mwananchi wa kawaida tu!!!
 
Ifike mahala tuseme tuu mwendazake alikuwa anakusanya kodi za vilio na laana ndo maana ndege zimeendeshwa kwa hasara kubwa mno,
 
TRA staff wanatumia gmail account? no wonder Tz hatuna maendeleo kumbe inaweza isiwe serikali bali umbumbu wa wananchi, hivi mnadhani e-mail pekee inaweza kuwa evidence kushawishi kuwa mtu ana onewa?
 
Daa hiyo barua inahuzunisha sana yaani jamaa ni muungwana sana
Anajali familia za watanzania watakao kosa ajira na hajui aanzaje kuwaambia

Ni hali ya kutisha sana hii kwa kutaka hela zote hizo
Kweli hatujui nyuma ya pazia kitu gani kinaendelea ila hali sio nzuri kwa watu kama hao
Bila kubomoa mfumo wa uendeshaji ofisini na idara za umma kazi itakuwa ngumu. Tatizo kubwa sana kwa baadhi ya wafanyakazi wa umma ni kugeuza ofisi za umma kuwa sehemu ya vitega uchumi vyao!

Mfano, TRA inabidi kuwa na mentality ya kutoa huduma kwa wafanyabiashara na wa wekezaji badala ya kuwa kero! Ofisi za umma ni lazima ziwe na viongozi wenye corporate mindset zaidi ya hapo nchi hii hatawaletea wananchi wake maendeleo yanayotarajiwa.
 
TRA staff wanatumia gmail account? no wonder Tz hatuna maendeleo kumbe inaweza isiwe serikali bali umbumbu wa wananchi, hivi mnadhani e-mail pekee inaweza kuwa evidence kushawishi kuwa mtu ana onewa?
Uwe muelewa basi hiyo e mail haitoki kwa staff wa TRA ila maelezo ndani yake yanamhusisha staff wa TRA kutoka ofisi ya Mwenge aliye m harass huyo mfanyabiashara
 
Huyu Mheshimiwa anaweza akawa haelewi kodi na namna ya kulitatua hili au Mamlaka ya TRA wanadai kodi ambayo si halali either kwa makusudi au kwakuwa hawana taarifa sahihi za mlipa kodi wao. Audit inapofanyika, TRA hutumia evidence walizonazo kutoa makadirio kama watakuwa wamekukagua. Wewe jukumu lako ni kujitetea kuwa TRA hamkupitia kitu moja mbili tatu wakati mnaandaa hesabu zenu. Una nafasi ya kufanya hivyo ndani ya siku 30 (siku za pingamizi kama ulikaguliwa na wakatoa assessment). Huyu kapewa nahisi ni Demand Notice. Ambayo unaijibu ndani ya Muda waliokupangia au unaomba Muda wa kujibu.

Ukionewa unaweka pingamizi kwa Commissioner, Commissioner akikuonea unaenda Tax Revenue Appeals Board (TRAB), inatoa maamuzi, ukionewa unaenda TRAT (Tax Revenue Appeals Tribunal) ukionewa na hapo unaenda Mahakamani.

Pia kuna muda watu hawajui Sheria ndio maana wanajikuta wanapigwa kodi kubwa. Mimi nilikuwa na mteja wangu mmoja wa Oil and Gas nikiwa Consultant wa Kampuni fulani alipigwa Kodi 9billion mpaka nikaduwaa.

Tukapambana tukaweka vielelezo akaishia kulipa Million 230 tu.

Jamani huko TRA weledi ni Mdogo sana wa Watendaji lakini pia kuna Tatizo la Walipa kodi kutokujua Sheria.

Natamani Siku humu ndani nifunguke kuhusu Kodi, Changamoto zake na Pia Madhaifu ya TRA na Madhaifu ya Walipa kodi na Ninyi cha Kufanya.

Mkiniruhusu naweza weka Uzi mmoja wa hayo yote hapa. Ila pia mwenye Maswali ya kodi ananiuliza hapa (nisiyoyajua naenda kuwataftieni majibu). Ahsanteni.
Mkuu weka na tueleze 9b madhara yake ni yapi? at the first place- kabla wewe hujaingia na huo u consultant wako mtu kisha kufa kwa pressure. Ndivyo watu wanafanya kazi hivi kweli? na nyie ndio mnao wacgulia TRA rushwa kutoka kwa wateja wenu mkiwa watu wa kati.
 
Kuna Wageni wengi sana nchini wana operate biashara zao Kinyemela na udanganyifu mwingi wanavyokua Exposed na Sheria zetu ndiyo wanaanza kulia lia. TRA kazeni
 
Kuna Wageni wengi sana nchini wana operate biashara zao Kinyemela na udanganyifu mwingi wanavyokua Exposed na Sheria zetu ndiyo wanaanza kulia lia. TRA kazeni
ma wenyeji kama Don wenu Mbowe?
 
TRA, TIC, BRELA, Halmashauri na taasisi zingine zinazohusika na utoaji wa vibali na usimamizi ni shida kubwa sanaa
Mbona wakati wa Mwendakazikwa ulikuwa ukikata viuno kuwa umeingia Uchumi wa katikati ya makaratasi
 
Mbona wakati wa Mwendakuzikwa ulikuwa ukikata viuno kuwa umeingia Uchumi wa katikati ya makaratasi

Acha kisran buana, hii issue tuliijadili sana mwaka jana na mwaka juzi hapahapa Jf
Uwe unajiridhisha kabla hujaongea mambo ya uongo kuhusu mtu au viti maana uongo unakuvunjia heshma
 
Ndie huyo huyo
Wewe ndio hunijui au umejisahau kama ilivyo kawaida yenu

Apumzike kwa amani shujaa JPM, rais wa karne
Haya bana anyway hongera nimekuona kwenye sekretariet iliyolala kwenye kaburi jana
 
Kwani TRA hawawezi kuweka namba za malalamiko? waweke hata na za watu wasiojulikana ili malalamiko yawe yanafanyiwa uchunguzi....
 
TRA Mwenge wametembeza barua nyingi sana kwa jina la audit. Watu wanapigwa hela ndefu kimya kimya. Yaani ni balaa. Unaletewa 400M muamze maongezi, mwisho wa siku mtu anafika 50m mtu anatia mfukoni maisha yanaendelea
Watumishi wengi wa taasisi za serikali ni janga... nisinukuliwe vibaya sijamaanisha wote ila wengi wao WATU WANATENGENEZA AJIRA MAAFISA WA UMMA WANAZIBOMOA!! Katika haya matukio hata WIZARA ZA FEDHA, MAMBO YA NDANI BILA KUSAHAU WIZARA YA KAZI NAZO ZIJITATHMINI....
 
Back
Top Bottom