Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Ukweli mbaya ni kuwa mwishowe atalipa mpangaji tu. Mfano TRA wakisema mwenye nyumba alipe, na mie ni mwenye nyumba nataka nipate shs 360 000 kwa mwezi kama kodi, nitakachofanya ni kama ifuatavyo:TRA mnatupa namba za simu eti kwa maelezo zaidi! Mimi mpangaji na mpokeaji simu hatuwezi kutatua tatizo kupitia simu, kodi ua ZUIO inahitaji maelezo ya kina kutoka uongozi na si marisepshenisti. Tunataka kodi ya ZUIO ilipwe na mwenye nyumba na si mpangaji.
Andika vizuri ueleweke.Ulipaji wa kodi ya zuio bado utaghubikwa na tatizo lingine la uwepo wa mikataba feki ya upangishaji wa nyumba. Kwa kiwango cha kodi cha 10% ina maana wenye nyumba ataambulia 90% katika mapato yake.
Endapo mwenye nyumba ndiye atawajibika kulipa, itawafanya watengeneze mikataba mingine feki yenye kuonyesha kuwa analipwa kiasi kidogo na wapangaji wao.
Katika suala zima la "tax paying culture" hasa hili la "voluntary compliance" ni vyema wapangaji ndiyo wawajibike kulipa kodi hii ya zuio, kwani kwa upande wao ni guarama ya matumizi ya kupanga nyumba hawawezi kuiepuka. Ila kwa wenye nyumba kulipa yeye mwenyewe kuna nafasi kubwa ya kufanya "tax evasion"
Miaka yote wapangaji ndio wanaolipa kwa niaba ya mwenye nyumba, TRA inamshauri mpangaji amtake mwenye nyumba mwisho wa mwaka amfidie kiwango alicholipa! Hii haiwezekani, lakini pia mpangaji anaweza akahama kabla ya mwisho wa mwaka, hapa TRA haina maelezo kama itamrudishia baadhi ya kodi ya miezi iliyosalia.Ukweli mbaya ni kuwa mwishowe atalipa mpangaji tu. Mfano TRA wakisema mwenye nyumba alipe, na mie ni mwenye nyumba nataka nipate shs 360 000 kwa mwezi kama kodi, nitakachofanya ni kama ifuatavyo:
X - 0.1X = 360 000
0.9X = 360 000 (gawanya kwa 0.9 kila upande)
X = 400 000
Hivyo, nitaingia mkataba na wewe wa kulipa kodi ya Shs 400 000 kwa mwezi 🙂
TRA wanafanya hivyo wakiamini itakuwa rahisi kwao kukusanya kodi. Ukitaka kujua hivyo fungua biashara na kama sehemu ya biashara sio yako lazima utaulizwa mkataba wa pango na ulipe 10% ya kodi ya pango ya mkataba ili uweze kupata Tax Clearance certificate.
Kutokana na nfano huo, ni afadhali alipe mpangaji kwani kwa kodi ya 360 000 kwa mwezi, atalipa jumla shs 396 000 kwa mwezi. Akilipa mwenye nyumba, mpangaji atalipa shs 400 000 kwa mwezi
Hujui usemalo kijana.TRA mnatupa namba za simu eti kwa maelezo zaidi! Mimi mpangaji na mpokeaji simu hatuwezi kutatua tatizo kupitia simu, kodi ua ZUIO inahitaji maelezo ya kina kutoka uongozi na si marisepshenisti. Tunataka kodi ya ZUIO ilipwe na mwenye nyumba na si mpangaji.
Sasa kama mpangaji analipa kwa niaba ya mwenye nyumba, itakuwaje tena mpangaji afidiwe na mwenye nyumba wakati hela alizolipa TRA ni za mwenye nyumba?Miaka yote wapangaji ndio wanaolipa kwa niaba ya mwenye nyumba, TRA inamshauri mpangaji amtake mwenye nyumba mwisho wa mwaka amfidie kiwango alicholipa! Hii haiwezekani, lakini pia mpangaji anaweza akahama kabla ya mwisho wa mwaka, hapa TRA haina maelezo kama itamrudishia baadhi ya kodi ya miezi iliyosalia.
Kwahiyo akipandisha hiyo 10% haitakuwepo! Pandisha vyovyote 10% itakuwepo tu.Hujui usemalo kijana.
Hata mwenye nyumba alioe kodi ujue hiyo 10% itatoka kwsko sababu atapandisha kodi kwa 10% au zaidi.
Hii imetoka mzee baba
Tu assume hakuna tax evasion na kila kitu ni legit, ni afadhali alipe mpangaji kwani ni nafuu kwake kutokana na mfano niliotoa.Ulipaji wa kodi ya zuio bado utaghubikwa na tatizo lingine la uwepo wa mikataba feki ya upangishaji wa nyumba. Kwa kiwango cha kodi cha 10% ina maana wenye nyumba ataambulia 90% katika mapato yake.
Endapo mwenye nyumba ndiye atawajibika kulipa, itawafanya watengeneze mikataba mingine feki yenye kuonyesha kuwa analipwa kiasi kidogo na wapangaji wao.
Katika suala zima la "tax paying culture" hasa hili la "voluntary compliance" ni vyema wapangaji ndiyo wawajibike kulipa kodi hii ya zuio, kwani kwa upande wao ni guarama ya matumizi ya kupanga nyumba hawawezi kuiepuka. Ila kwa wenye nyumba kulipa yeye mwenyewe kuna nafasi kubwa ya kufanya "tax evasion"
Sidhani kama umenielewa.Kwahiyo akipandisha hiyo 10% haitakuwepo! Pandisha vyovyote 10% itakuwepo tu.
Hii kodi ya ZUIO nimekuwa nikiilipa kwa zaidi ya miaka 15 hivyo si ngeni kwangu kwa unavyodhani, tatizo JF kumejaa vidudu mtu vyenye dharau na matusi.
Pandisha vyovyote vile 10% itakuwepo, pandisha toka laki moja kwenda laki tano 10% ipo palepale.Sidhani kama umenielewa.
Nilimaanisha kuwa ikiwa mwenye nyumba anapaswa kuilipa ili afanikishe hili itamlazimu apandishe kodi kwa 10% ili ahakikishe anayeilipa ni mpangaji kupitia hayo malipo ya kodi ili kodi yake ibaki kama awali.
Usihangaike na maelezo hayo, kiasi chochote atakachoongeza ili aikomboe 10% bado 10% itakuwepo, labda ashushe kodi isifikie kiwango cha kisheria kulipa kodi yaani 500,000/=.Labd serikali itoe bei elekezi kwanza kwa wenye nyumba ili ieleweke vzr maana hapa nachokiona ni kile alichokikokotoa mwenzetu hapo juu.
Nilimaanisha bei ya kupanga chumba iwekwe kisheria na isimamiwe kikamilifu isikiukwe mfano kama ni laki 3 kwa mwezi basi iwe hivyo ili mwenye nyumba asimpandishie mpangaji kwa 10% kwamba laki 3 yake isiathiriwe.Usihangaike na maelezo hayo, kiasi chochote atakachoongeza ili aikomboe 10% bado 10% itakuwepo, labda ashushe kodi isifikie kiwango cha kisheria kulipa kodi yaani 500,000/=.
Bei yoyote ile inayo 10%, na si jukumu la TRA kupanga bei za vyumba.Nilimaanisha bei ya kupanga chumba iwekwe kisheria na isimamiwe kikamilifu isikiukwe mfano kama ni laki 3 kwa mwezi basi iwe hivyo ili mwenye nyumba asimpandishie mpangaji kwa 10% kwamba laki 3 yake isiathiriwe.