TRA waunde kitengo cha upangishaji wa nyumba, kila mwenye nyumba aripoti TRA anapotaka kupangisha na iwe kwa mujibu wa sheria

TRA waunde kitengo cha upangishaji wa nyumba, kila mwenye nyumba aripoti TRA anapotaka kupangisha na iwe kwa mujibu wa sheria

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Mimi ni miongoni mwa watu naopinga sana madalali kutaka kulipwa kodi ya mwezi mmoja kwani ni kuumiza wapangaji kwa kuwaongezea gharama za maisha. Kibaya zaidi, wako wenye nyumba hawapangishi mtu bila kupitia madalali wao hata kama inawezekana kupanga bila kupitia hao madalali.

Hivyo, nakubaliana na Lukuvi wenye nyumba wawalipe madalali na jambo hili litungiwe sheria na sheria itoe adhabu ya kifungo au faini au vyote kwa pamoja kwa atakaekaidi.

Sambamba na hilo, TRA waanzishe kitengo cha upangishaji nyumba ambapo wenye nyumba watatakiwa kutoa taarifa TRA wanapotaka kupangisha, kisha jukumu la kutafuta wapangaji liwe la TRA, ila mwenye nyumba aruhusiwe kuweka mpangaji bila kupitia TRA mradi tu alipe kodi.

Utaratibu huu ukiwekwa kisheria, sio tu utaondoa unyonyaji wa madalali, bali uta-facilitate ukusanyaji wa kodi kupitia nyumba za kupangisha na ambao teyari upo kwa mujibu sheria.

Mwanachi yoyote anaetaka nyumba ya kupangisha, atakiwe(kwa mujibu wa sheria) kufika katika ofisi za TRA, na kisha TRA kupitia kitengo husika, watakuwa na jukumu la kuwapangisha wananchi na hapo hapo kukusanya kodi ya serikali.

Tena TRA wanaweza kufanya kazi hii katika mazingira bora zaidi kwa kuwapeleka wateja kwa kutumia magari yao, pikipiki au bajaji maalumu ziitazonunuliwa kwa kutumika fedha zitazokusanywa kupitia upangishaji wa aina hii.

Hakuna kinachoshindikana kama dhamira ipo. Kama kupata baadhi ya huduma tunalazjmika kwanza kupitia TRA, kwani hili la kupangisha kupitia TRA lishindikane?

Haingiii akilini hata kidogo kwa mtumishi wa serikali mwenye mshahara wa shilingi 300,000 kwa mwezi, alipe kodi(PAYE), halafu dalali au mwenye nyumba anaeingiza malaki au mamilion kadhaa anapopangisha, asilipe kodi(huu ni uwendawazimu kabisa).

Tulipendekeza hili hakuna kilichiofanyika, hivyo TRA waingie kazini.

 
Nakubaliana na wazo japo njia za kuzuia urasimu wa watumishi ndani ya TRA ziimarishwe ipasavyo
Sisi karibu kila kitu mpaka kianzie kwa wenzetu, na sisi ndio tuige na si kubuni vya kwetu kutegemea na mazingira yetu.
 
Udalali ni ajira labda waweke regulation dhidi yao sio TRA kuchukua jukumu vijana wengi wamejiajiri huku acheni mawazo potofu ukilipa ya mwezi ni fresh kwani unalipa tena
 
Kwahiyo ukijenga ndio ufanye ulanguzi kupitia madalali?
Nauli ya kuzunguka kukutafutia nyumba nzuri dalali huwa unamlipa wewe?

Kutumia dalali hujalazimishwa katafute mwenyewe basi hujazuiwa pita kila nyumba gonga hodi uliza Kama wanapangisha Kama unaona kazi ya dalali haina maana

Si kila dalali hupewa kazi ya kutafuta mpangaji na mwenye nyumba .Yeye aweza tu kukutafutia ukampa chake Kodi yote ukamalizana na mwenye nyumba yeye hapati hata Mia toka kwa mwenye nyumba

Siku ukihamia mji mgeni na wewe humjui mtu Ndipo utakapojua umuhimu wa dalali iwe utatafuta nyumba ya kupanga ,fremu au kiwanja

Hata akipata pesa kote kote shida iko wapi so ndio kujiajiri kwenyewe? Inaposemwa watu wajiajiri maana yake Nini?
 
Umekaa sijui chumba ca kupanga, Sijui kea shemeji yako.

Umeshiba kiporo Cha makande unaanza kuwadis walotoka jasho kugharamikia usingizini wako kiazi wewe.

Yaan,
Ungejua Ni jins gani ujenzi unaumiza Wala usingethubutu kuongea Ayo maneno yako mbofu mbofu.

Jenga nyumba yako afu uje Tena na huu utopolo wako humu.
 
Nauli ya kuzunguka kukutafutia nyumba nzuri dalali huwa unamlipa wewe?

Kutumia dalali hujalazimishwa katafute mwenyewe basi hujazuiwa pita kila nyumba gonga hodi uliza Kama wanapangisha Kama unaona kazi ya dalali haina maana

Si kila dalali hupewa kazi ya kutafuta mpangaji na mwenye nyumba .Yeye aweza tu kukutafutia ukampa chake Kodi yote ukamalizana na mwenye nyumba yeye hapati hata Mia toka kwa mwenye nyumba

Siku ukihamia mji mgeni na wewe humjui mtu Ndipo utakapojua umuhimu wa dalali iwe utatafuta nyumba ya kupanga ,fremu au kiwanja

Hata akipata pesa kote kote shida iko wapi so ndio kujiajiri kwenyewe? Inaposemwa watu wajiajiri maana yake Nini?
Basi hata majambazi na wapiga dili nao wamejiajiri.
 
Umekaa sijui chumba ca kupanga, Sijui kea shemeji yako.

Umeshiba kiporo Cha makande unaanza kuwadis walotoka jasho kugharamikia usingizini wako kiazi wewe.

Yaan,
Ungejua Ni jins gani ujenzi unaumiza Wala usingethubutu kuongea Ayo maneno yako mbofu mbofu.

Jenga nyumba yako afu uje Tena na huu utopolo wako humu.
Kama ulivyoumia kujenga nyumba, hata mpangaji anaumia kupata hiyo hela.

Hata sisi tunajua maumivu ya kujenga.
 
Na laiti ungejua,

Ungewahurumia Sana wenye nyumba.

Biashara ya nyumba kwa bongo hii bado Ni biashara kichaa.

Iyo Kodi unayolipa haiwezi kurudisha uwekezaji aloweka kukutetengenezea huo usingizini wako.

Na ndo maana kila sikU wanaomiliki nyumba zao Ni wachache mno kuliko wanaohitaji kupanga.

Iyo Yote ni kwasababu

Gharama za kujenga nyumba ziko juu sana na kujenga Nyumba ya kuipangisha kwa ajili ya makazi Hailipi Kama unavotaka kutuaminisha humu ndani.

Kiasi kwamba we unaona kama wenye nyumba wanafaidi Sana.[emoji3525]

Mfano: mtu anajenga nyumba+kiwanja kwa JUMLA ya mil. 100 .
Afu Kodi unalipa laki 3 kwa mwezi.

Hivi unategemea kwa iyo laki 3 kwa mwezi, iyo pesa mil 100 unairudisha vipi,lini na kwa MDA gani.

Ikiwa Bado Kuna ukarabati wa vitu vidogo vidogo kila angalau miaka 2 au mpangaji akihama.

Vitu Kama Rangi,sakafu, mifumo ya maji, umeme, mazingira n.k
 
Kama ulivyoumia kujenga nyumba, hata mpangaji anaumia kupata hiyo hela.

Hata sisi tunajua maumivu ya kujenga.
Kama mnaumia basi jengeni zenu

Mwende mkaweke izo sheria zenu uko kwenye nyumba zenu.

Sio unaweka sheria mbofu mbofu kwenye jasho la Wanaume wenzenu.
 
Na laiti ungejua,
Ungewahurumia Sana wenye nyumba.

Biashara ya nyumba kwa bongo hii bado Ni biashara kichaa.

Iyo Kodi unayolipa haiwezi kurudisha uwekezaji aloweka kukutetengenezea huo usingizini wako.

Na ndo maana kila sikU wanaomiliki nyumba zao Ni wachache mno kuliko wanaohitaji kupanga.

Iyo Yote Ni kwasababu,
Gharama za kujenga nyumba ziko juu sana na
Kujenga Nyumba ya kuipangisha kwa ajili ya makazi Hailipi Kama unavotaka kutuaminisha humu ndani.

Kiasi kwamba wee unaona Kama wenye nyumba wanafaidi Sana.[emoji3525]

Mfano: mtu anajenga nyumba+kiwanja kwa JUMLA ya mil. 100 .
Afu Kodi unalipa laki 3 kwa mwezi.

Hivi unategemea kwa iyo laki 3 kwa mwezi, iyo pesa mil 100 unairudisha vipi,lini na kwa MDA gani.

Ikiwa Bado Kuna ukarabati wa vitu vidogo vidogo kila angalau miaka 2 au mpangaji akihama.

Vitu Kama Rangi,sakafu, mifumo ya maji, umeme, mazingira n.k
Sasa kama hela unajua ni ngumu, kati ya dalali na mpangaji, nani anastahili kutetewa?
 
Inawezekana kabisa kukawa na kanzi data (database) ya nyumba zote zinazopangishwa zilizopo Tanzania then zikawepo kwenye website fulani ambapo picha za nyumba, vyumba, mazingira, mtaa nyumba ilipo na details zingine nyiingi zitaonekana peupeeeee. infact kama serikali ingekuwa makini inatakiwa namba ya mtu ya NIDA ikibofya ionyeshe detail nyingi za mtu huyo mwenye namba hiyo na nyumba majengo anayomiliki yakiwemo status yake kuhusu ulipaji wa kodi. Ni kweli ni kazi nzito kuwa na database ya aina hii but kidogokidogo serikali ikianza kwa mfano na wilaya let say ya Ilala, then ikaroll out project nzima kwa maeneo mengine kidogokidogo naamini inawezekana baada ya miaka michache TRA itakuwa imeongeza mapato (yatokanayo na kodi ya zuio kwenye kodi za majengo kwa kiasi kikubwa tu.

Tatizo viongozi wa kiafrika huwaza kwanza 50% ya rushwa kwenye project kama hii toka kwa wakandarasi/wadhabuni atapata kiasi gani anaacha kuangalia manufaa ya vizazi na vizazi yatakoyotokana na utekelezaji wa project kama hii. Sasa hivi ile kodi ya zuio kwenye kodi na ushuru wa stemp wanalipia makampuni, NGOs na baadhi ya biashara maana hawa hawana namna inabidi wakomply maana watapigwa penalti wasipocomply na pia hubanwa na TRA (kuwa je ushuru wa stamp wa mkataba wa nyuma na kodi ya zuio kuhusu nyumba/ofisi waliyopanga vimelipwa?) pindi kwa mfano wanapotaka kupata huduma fulanifulani toka TRA.

Nenda kwa wabunge wenye nyumba dodoma chunguza ni wangapi ambao wapangaji wao hawawakati kodi ya zuio na kuipeleka TRA utakuta ni wengi sana na wabunge si rahisi kuunga mkono hili maana itapunguza mapato yao yatokanayo na biashara zao za nyumba/majengo ya kupangisha. Wanasiasa wanafiki sana eti Lukuvi ansema alikuwa hajui kama madalali huchukua kodi ya mwezi mmoja!!!! na hapa ndipo Mange anapopataga umaarufu wa burebure maana anaoneka kawasemea watanzania

Mifumo ya IT ikitumika vizuri inapunguza sana upotevu wa kodi au kuepusha migogoro ya ardhi isiyo ya lazima hivi kwa mfano why kusiwe na database i.e. landbank database ambapo mtu akisema nauza kiwanja changu tegeta wateja just wanaingiza details za huyo muuzaji then wateja wanajua kama kiwanja ni cha kwake kweli huyo muuzaji au la. Maana utacompare taarifa alizokupa mnunuzi na taarifa za kanzidata then itajulikana kama muuzaji ni mmiliki halal n.k.

Tatizo kama nilivyosema awali viongoz wa kiafrika kitu/wazo linalonufaisha wananchi na kuwaondolea ulaji wao hawapendi asilani, wakati wazo la kuwa na mfumo wa kihasibu wa kutunza matumizi, mapato, bajeti kwa serikali ambao ni computerized lilipingwa sana na viongozi fulai fulan tena wengine wa nafasi za juuu na wameenda shule huwezi amini!! kwa nini walipinga ni kwa kuwa ulaji wao ungepungua kwa kuwa sasa taarifa za mapato matumizi bajeti zingekuwa rahisi sana kupatikana.

Ashukuriwe Mungu hatimaye serikali na taasisi zake baada ya muda zililazimika kuwa na mifumo hiyo ya kihasibu but ilikuwa ni vita
 
Kama mnaumia basi jengeni zenu,
Mwende mkaweke izo sheria zenu uko kwenye nyumba zenu.

Sio unaweka sheria mbofu mbofu kwenye jasho la Wanaume wenzenu.
Unadhani hatuna nyumba?

Hela upate mwenye nyumba, halafu dalali uliempa kazi alipwe na mpangaji?

Mnapolalamika serikali kuwatoza tozo/kodi mara mbili mbili, mjiulize mnachokifanya kina tofauti gani na kumtoza mwananchi gharama kubwa isio na uhalali?
 
Kw Hii Tanzania

Nyumba ya kupanga ni huduma kwa jamii.

Na ndo maana hata serikali imekaa kimya kwa Kodi za pango zinazotozwa.

Maana wenye nyumba kwa bongo hii, ni kama tu wanaisaidia serikali jukumu lake la kuhakikisha Rai wake wanaishi makazi Bora.

Na laiti Kama serikali ikiamua kuwakandamiza wenye nyumba,

Hilo zigo lote anabeba mpangaji mwenyewe.

Maana anachokifanya mwenye nyumba

Ni kupandisha TU Bei ya pango ili kufidia Kero za serikali.

Na kwa maana Hamna Bei elekezi kwenye pango la nyumba(Bei ni maelewano)

Basi hawawezi kuingilia unaeumia ni wee mpangaji
 
Nauli ya kuzunguka kukutafutia nyumba nzuri dalali huwa unamlipa wewe?

Kutumia dalali hujalazimishwa katafute mwenyewe basi hujazuiwa pita kila nyumba gonga hodi uliza Kama wanapangisha Kama unaona kazi ya dalali haina maana

Si kila dalali hupewa kazi ya kutafuta mpangaji na mwenye nyumba .Yeye aweza tu kukutafutia ukampa chake Kodi yote ukamalizana na mwenye nyumba yeye hapati hata Mia toka kwa mwenye nyumba

Siku ukihamia mji mgeni na wewe humjui mtu Ndipo utakapojua umuhimu wa dalali iwe utatafuta nyumba ya kupanga ,fremu au kiwanja

Hata akipata pesa kote kote shida iko wapi so ndio kujiajiri kwenyewe? Inaposemwa watu wajiajiri maana yake Nini?
Acha ujuaji babu kuna hoja za msingi za jamaa hujajibu, yaani kwa kutumia gharama zangu mwenyewe nitafute nyumba, nimepata mwenye nyumba kasema anapangisha kwa mwezi laki2 na nusu kwa mwezi, ila kabla sijafunga naye mkataba analazimisha dalali wake awepo na nimlipe laki2 na nusu huyo dalali kwa kazi gani aliyofanya? Huu ndo upumbavu tunaukataa sie.
 
Back
Top Bottom