TRA yaanza kufanya ukaguzi wa risiti nchi nzima

TRA yaanza kufanya ukaguzi wa risiti nchi nzima

Scaramanga

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2020
Posts
490
Reaction score
704
Naona lile zoezi la TRA la kamata wote kumbe kweli du, kumbe wapo kweli kazini naona matukio jana walikuwa Jangwani na Kariakoo yaani ukiwa hujatoa risiti au hujaomba risiti unao.
1643960701002.png

1643960746816.png#TEGETA Maafisa wa TRA Mkoa wa kodi wa Tegeta leo 03/02/2022 wameendelea na zoezi la ukaguzi wa risiti za #EFD kwa Wafanyabiashara na wanunuzi ikiwa ni kampeni maalum ya #KAMATAWOTE yenye nia ya kuhamasisha utoaji na kudai risiti za EFD.
1643960784154.png

#MTWARA Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mtwara leo imeendeleza kampeni ya #KAMATAWOTE ambapo baadhi ya wateja wasiodai risiti za EFD walisisitizwa kudai risiti halali ikiwemo wauzaji kutoa risiti kulingana na mauzo walioyafanya kwa wateja wao.
1643960846289.png

#KARIAKOO Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bi. Janeth Mtimba (kulia) akichukua taarifa za mzigo wa mfanyabiashara ambaye hakua na risiti za #EFD za mzigo alonunua na kupakia katika lori wakati wa kampeni ya #KAMATAWOTE Jangwani, jijini Dar es Salaam.
WhatsApp Image 2022-02-04 at 8.16.11 AM.jpeg
WhatsApp Image 2022-02-04 at 8.16.42 AM.jpeg
 
Huku kwetu "tipa" zinazobeba mchanga na mawe lazima wawe na mashine ya EFD.
 
Zoezi kama hilo ilitakiwa wasitangaze iwe operesheni ya kimya kimya sasa walitangaza feb1 wanaanza sasa hivi ukimwambia mtu leo nakuja kwako kuiba huyo mtu atalala kweli usiku?

Sema January wamefulia acha watafute hela za kula na kulia bata madudu yao tunayajua yote.
 
Nawashauri TRA waweke bonus kwa wateja/wanunuzi. Mfano, mteja akinunua bidhaa na kudai receipt, then atume reference number za receipt kwenda TRA ili apate angalau commission ya 3% na TRA wabaki na 15%.
 
Wakajenge Magereza za kutosha hilo zoezi ni haliwezekani ba sijaliona hapa Afrika ya Mashariki.
 
Pongezi kwa TRA huo ulikuwa udhaifu mkubwa sana kwenye suala la kodi pia risiti ina umuhimu wake kwa mnunuzi wa bidhaa.
 
Nawashauri TRA waweke bonus kwa wateja/wanunuzi. Mfano, mteja akinunua bidhaa na kudai receipt, then atume reference number za receipt kwenda TRA ili apate angalau commission ya 3% na TRA wabaki na 15%.

Wazo zuri
 
Sema bado tunawazidi ujanja, maana kama mauzo ya million 8 jioni mtu umetoa risti za million 4.5 .. waongeze nguvu
 
Nawashauri TRA waweke bonus kwa wateja/wanunuzi. Mfano, mteja akinunua bidhaa na kudai receipt, then atume reference number za receipt kwenda TRA ili apate angalau commission ya 3% na TRA wabaki na 15%.
3% ya Kodi yote nchini ni kiasi gani?!!
 
Naona lile zoezi la TRA la kamata wote kumbe kweli du, kumbe wapo kweli kazini naona matukio jana walikuwa Jangwani na Kariakoo yaani ukiwa hujatoa risiti au hujaomba risiti unao.
View attachment 2107391
View attachment 2107392#TEGETA Maafisa wa TRA Mkoa wa kodi wa Tegeta leo 03/02/2022 wameendelea na zoezi la ukaguzi wa risiti za #EFD kwa Wafanyabiashara na wanunuzi ikiwa ni kampeni maalum ya #KAMATAWOTE yenye nia ya kuhamasisha utoaji na kudai risiti za EFD.
View attachment 2107393
#MTWARA Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mtwara leo imeendeleza kampeni ya #KAMATAWOTE ambapo baadhi ya wateja wasiodai risiti za EFD walisisitizwa kudai risiti halali ikiwemo wauzaji kutoa risiti kulingana na mauzo walioyafanya kwa wateja wao.
View attachment 2107395
#KARIAKOO Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bi. Janeth Mtimba (kulia) akichukua taarifa za mzigo wa mfanyabiashara ambaye hakua na risiti za #EFD za mzigo alonunua na kupakia katika lori wakati wa kampeni ya #KAMATAWOTE Jangwani, jijini Dar es Salaam.
View attachment 2107224View attachment 2107225
Nimeshangaa jana nilipita Uhuru Road kuanzia maeneo ya Ilala mpaka Buguruni niliona maduka mengi yamefungwa sikuelewa nini sababu.Kumbe inawezekana wanaogopa hii ya kamata wote
 
Jamaa yangu walimpigia rada kwenye kituo Cha kuuza mafuta ya gari, akaondoka hawakuona Kama amepewa risiti jamaa wakamfukuzia na Toyo wanakuja Kama sio maofisa baada ya kujitambulisha wakaomba risiti aliyopewa baada ya kununua mafuta.

Jamaa alipowaonyesha wakaingia upepo wakasanda. Yaani hapo ingekuwa hana receipt inhemtoka hela ya rushwa hapo balaa.

Tudai receipt kwa maendeleo yetu na Taifa letu.
 
Back
Top Bottom