Traffic wanabambikia watu faini, unaletewa meseji kwenye simu kwamba umepigwa faini na gari halijaenda popote

Traffic wanabambikia watu faini, unaletewa meseji kwenye simu kwamba umepigwa faini na gari halijaenda popote

Brazaj una ila,uchaguzi ushakwisha
Wewe siyo tila lila,kurejea yaloisha
Lissu huko anakula,anayaponda maisha
Nchi tujenge pamoja,ya namba tusiyakuze

Nawe Mrangi sikia,usizidi kuchongea
Siku wakikupatia,usije kutugongea
Akili zitakwishia,uanze kunyong'onyoe
Nchi tujenge pamoja ya namba tusiyakuze

Sefu yeye kabaini,lazima tushikamane
Ametilia maanani,Nchi kwanza si mengine
Makandokando ya nini,Hatuna kwenda kwingine
Nchi tujenge pamoja ,ya namba tusiyakuze.
Mimi nakula pesa zangu,mimi sio nzi wa kijani kama wewe.
Subiria teuzi utapewa hata viti maalum uwt
 
Brazaj una ila,uchaguzi ushakwisha
Wewe siyo tila lila,kurejea yaloisha
Lissu huko anakula,anayaponda maisha
Nchi tujenge pamoja,ya namba tusiyakuze

Nawe Mrangi sikia,usizidi kuchongea
Siku wakikupatia,usije kutugongea
Akili zitakwishia,uanze kunyong'onyoe
Nchi tujenge pamoja ya namba tusiyakuze

Sefu yeye kabaini,lazima tushikamane
Ametilia maanani,Nchi kwanza si mengine
Makandokando ya nini,Hatuna kwenda kwingine
Nchi tujenge pamoja ,ya namba tusiyakuze.

Ya namba mbona madogo, kwani hata yanakuzwa?
Ngoma meno na mandongo, watapolima mazwazwa!
Kwani wala ni uongo, tuko kama tumeuzwa,
Ndiyo ukweli mchungu, wapora haki si watu.

Vipi tuafikiane, na wezi na wauaji,
Hata tubaki wanne, si mwenzetu mporaji,
Hata ipite karne, ipo siku tutahoji,
Senzighe utuelewe, tuna machungu moyoni.

Sefu ameweka wazi, ICC yawahusu,
Kule kunachapwa kazi, yasubirini ya Lissu,
Mlidhani sisi mbuzi, tutatishika kwa visu?
Hii ngoma bado mbichi, kwa sisi Sefu na Lissu!
 
Ya namba mbona madogo, kwani hata yanakuzwa?
Ngoma meno na mandongo, watapolima mazwazwa!
Kwani wala ni uongo, tuko kama tumeuzwa,
Ndiyo ukweli mchungu, wapora haki si watu.

Vipi tuafikiane, na wezi na wauaji,
Hata tubaki wanne, si mwenzetu mporaji,
Hata ipite karne, ipo siku tutahoji,
Senzighe utuelewe, tuna machungu moyoni.

Sefu ameweka wazi, ICC yawahusu,
Kule kunachapwa kazi, yasubirini ya Lissu,
Mlidhani sisi mbuzi, tutatishika kwa visu?
Hii ngoma bado mbichi, kwa sisi Sefu na Lissu!
Usitutishe lolote,hiyo court kangaruu
Hakuna kwenda popote,Lissu ni mwoga kunguru
Mtaimba nyimbo zote,mwishowe mtakufuru
Brazajei subiri,mitano ipite kwanza
 
Usitutishe lolote,hiyo court kangaruu
Hakuna kwenda popote,Lissu ni mwoga kunguru
Mtaimba nyimbo zote,mwishowe mtakufuru
Brazajei subiri,mitano ipite kwanza

Kutisha si hulka yangu, wala ya wapambanaji,
Watishaji wa marungu, si nyie wakamataji?
Tumeyaonja machungu, kote hadi kwenye paji,
Pelekeni taarifa, tuko imara kinoma!

Kangaruu ya dunia, siyo hizi Tanzania?
ICC waijua, au unaisikia?
Achana na vya dunia, hali yako pambania,
Wazitaka kangaruu, hizo zimejaa kwetu!
 
Kumekuwa na hali ambayo haileweki ndani ya jeshi la polisi upande wa usalama barabarani ambapo unaletewa meseji kwenye simu kwamba umepigwa faini na unaandikiwa na kosa lako wakati huo wewe upo Dar es salaam na gari halijaenda popote siku nzima wewe upo nyumbani.

Ukiingia kwenye mtandao wao wa tms.tpf.go.tz unasachi gari yako unaona kweli umeandikiwa kosa kwa muda huo lakini unakuta kosa hilo limefanyikia mkoani. Ukienda kuripoti tatizo hilo unaelekezwa uende traffic Central ili tatizo lako liweze kushughulikiwa na kitengo kinachohusika na malalamiko kama hayo.

Hapo sasa unaanza kuzungushwa kwani unaambiwa uache namba ya simu watalishughulikia na wanakueleza uwapigie kuwakumbushia. Sasa ukishaondoka hapo baada ya siku chache ukimpigia yule mhusika hapokei tena simu yako na ukitazama kwenye mtandao deni liko palepale.

Tunaomba wakuu wanaohusika ndani ya Jeshi letu la Polisi walitazame jambo hili la kubambikiwa faini kwani linawanyima raha wananchi wanaotumia vyombo hivi na kuwafanya wakose imani na jeshi lao la polisi ambalo tunaamini kuna maeneo wanafanya kazi vizuri sana.
Leo nimekamatwa na traffic eti gar yangu Ina den imepigwa fain tar 31 wakat mwezi wa 11 wakat gar yangu ipo ndan sijaitumia now wiki Tatu natumia gar ya mke wangu
 
Kumekuwa na hali ambayo haileweki ndani ya jeshi la polisi upande wa usalama barabarani ambapo unaletewa meseji kwenye simu kwamba umepigwa faini na unaandikiwa na kosa lako wakati huo wewe upo Dar es salaam na gari halijaenda popote siku nzima wewe upo nyumbani.

Ukiingia kwenye mtandao wao wa tms.tpf.go.tz unasachi gari yako unaona kweli umeandikiwa kosa kwa muda huo lakini unakuta kosa hilo limefanyikia mkoani. Ukienda kuripoti tatizo hilo unaelekezwa uende traffic Central ili tatizo lako liweze kushughulikiwa na kitengo kinachohusika na malalamiko kama hayo.

Hapo sasa unaanza kuzungushwa kwani unaambiwa uache namba ya simu watalishughulikia na wanakueleza uwapigie kuwakumbushia. Sasa ukishaondoka hapo baada ya siku chache ukimpigia yule mhusika hapokei tena simu yako na ukitazama kwenye mtandao deni liko palepale.

Tunaomba wakuu wanaohusika ndani ya Jeshi letu la Polisi walitazame jambo hili la kubambikiwa faini kwani linawanyima raha wananchi wanaotumia vyombo hivi na kuwafanya wakose imani na jeshi lao la polisi ambalo tunaamini kuna maeneo wanafanya kazi vizuri sana.
Mimi nimefanyiwa hivyo makosa matatu na penati laki na themanini uzuri trafiki alipiga faini kimakosa namuandama kila siku ayalipe yeye ameshalipa mawili bado moja
 
Nilishawah kukamatwa na zile mashine zao za kudai maden kimara pale jamaa wakanipa deni la 60000 na leseni sio yangu ila gar yangu na sijawah kumpa mtu gar jamaa walidandia pale mpka nikalipa ndo nikatoka yan upumbavu mtupu
 
Kutisha si hulka yangu, wala ya wapambanaji,
Watishaji wa marungu, si nyie wakamataji?
Tumeyaonja machungu, kote hadi kwenye paji,
Pelekeni taarifa, tuko imara kinoma!

Kangaruu ya dunia, siyo hizi Tanzania?
ICC waijua, au unaisikia?
Achana na vya dunia, hali yako pambania,
Wazitaka kangaruu, hizo zimejaa kwetu!
Mnatishwa na vibwengo,vinakaa uholanzi
Zimepanda zao shingo,kazi yao makamuzi
Wamepanuka maungo,kusikiza upuuzi
Waende na Marekani,kukamata wauaji.
 
Hawa polisi JPM Keshabariki maovu yao. Hata useme vipi hawachukuliwi hatua yoyote. My take jihadhari na polisi vitengo vyote kadiri unavyoweza, epuka sana kutumia private means of transport. Zile POS walizopewa ni majanga unabambikwa kosa ukilalamika unaambiwa wamepewa malengo ya makusanyo. Ukiuliza mbona hiyo kazi ya kukisanya mapato siyo ya polisi ni ya Tra unaambiwa twende kituoni ukaseme hayo matusi mbele ya OCD. ukifika huko unawekwa ndani. Chezea polisi ya magu wewe!
Umesema sahihi kabisa.

Polisi wa sasa wanakusanya fedha kwa njia halali na haramu.
 
Sasa we presha ya nini?

Namba ya leseni sio yako, basi tulia!

Presha inakuwapo kwani gari huwezi kutembeza wakisema inadaiwa.

Wanapenda kufunganisha leseni na magari kwani hayo kwao ni rahisi kupiga pesa kuliko leseni.

Kwao leseni hazina maslahi bali namba za magari.
 
Mnatishwa na vibwengo,vinakaa uholanzi
Zimepanda zao shingo,kazi yao makamuzi
Wamepanuka maungo,kusikiza upuuzi
Waende na Marekani,kukamata wauaji.

Wakoloni tumeona, weupe hata weusi,
Ubaya wanafanana, baba lao ni jeusi!
Bila Hague kuyabana, tungepumua je sisi?
Udumu sana beberu, mbona yangetumaliza!
 
Wakoloni tumeona, weupe hata weusi,
Ubaya wanafanana, baba lao ni jeusi!
Bila Hague kuyabana, tungepumua je sisi?
Udumu sana beberu, mbona yangetumaliza!
Hao ni watu laghai,wasumbufu Afrika
Wakisha kuvaa tai,hujiona malaika
Husingizia jinai,kuwalinda vibaraka
Na wakome wakomeke,kuifuata Tanzania.
 
Jamaa angu juzi kati kaandikiwa faini mara 4 sehemu tofauti mkoani na gari ipo ndani hapa Dar miezi mitatu haijatoka.

Alivyowafata wakamfutia wakasema walikosea
Me waligoma ikabidi nilipe nikawa mbia nileteyeni huyo dereva wakasema sio kazi yao tunapitia magumu sana 😭
 
Sasa we presha ya nini?

Namba ya leseni sio yako, basi tulia!
Atulie!!!?
wata mlipisha me nilienda adi kituoni nikawa mbia wanileteye mwenye leseni me simjui wakasema sio kazi yao tupo nchi ya kusadikika 😭
 
Hao ni watu laghai,wasumbufu Afrika
Wakisha kuvaa tai,hujiona malaika
Husingizia jinai,kuwalinda vibaraka
Na wakome wakomeke,kuifuata Tanzania.

Wakadumu Mabeberu, watupao kupumua,
Hamnaga kushukuru, hamtoki mtaua?
Bila yao Mabeberu, kwani mngejitambua?
Mnajiita majiwe, beberu saizi yenu!
 
Back
Top Bottom