Trafiki 8 wafukuzwa kazi, 84 waonywa wengine wahamishwa vituo

Trafiki 8 wafukuzwa kazi, 84 waonywa wengine wahamishwa vituo

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Askari wa usalama wa barabarani 168 wamechukuliwa hatua zikiwamo kushtakiwa kijeshi, kuhamishwa vitengo na kufukuzwa kazi, kutokana na makosa ya kinidhamu ikiwemo rushwa katika kipindi cha kuanzia Juni 2023 hadi Juni 2024.

Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama wa Barabarani, Deus Sokoni ameeleza hayo wakati wa uzinduzi wa wiki ya usalama wa barabarani, inayoambatana na sherehe za miaka 50 tangu kuanzisha kwa Baraza la Usalama wa Barabarani.

Sokoni ameyasema hayo baada ya kuulizwa maswali na Makamu wa Rais Dk Philip Mpango wakati akikagua mabanda yaliyopo katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Dk Mpango alihoji ni askari wangapi na hatua gani wamechukua.Akijibu swali hilo, Sokoni amesema wamewakamata askari 168 ambapo wengine wameondolewa katika utumishi wa usalama wa barabarani, huku wengine wakichukuliwa hatua za kushtakiwa kijeshi na wengine wakipewa onyo.

Amesema askari wanane kati ya hao walifukuzwa kazi, 84 walionywa huku waliobakia wakihamishiwa katika vitengo vingine.

MWANANCHI
 
Mmewaonea, badala ya ku deal na watekaji- hawa wa barabarani hawanaga shida ni marafiki zetu tunajuana namna ya kuishi.

Afu sijakagulisha gari yangu..
 
Askari wa usalama wa barabarani 168 wamechukuliwa hatua zikiwamo kushtakiwa kijeshi, kuhamishwa vitengo na kufukuzwa kazi, kutokana na makosa ya kinidhamu ikiwemo rushwa katika kipindi cha kuanzia Juni 2023 hadi Juni 2024.

Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama wa Barabarani, Deus Sokoni ameeleza hayo wakati wa uzinduzi wa wiki ya usalama wa barabarani, inayoambatana na sherehe za miaka 50 tangu kuanzisha kwa Baraza la Usalama wa Barabarani.
Majizi matupu!!!
Wawataje majina hao waliochukuliwa hatua hizo kama siyo ngonjera tu
 
Askari wa usalama wa barabarani 168 wamechukuliwa hatua zikiwamo kushtakiwa kijeshi, kuhamishwa vitengo na kufukuzwa kazi, kutokana na makosa ya kinidhamu ikiwemo rushwa katika kipindi cha kuanzia Juni 2023 hadi Juni 2024.

Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama wa Barabarani, Deus Sokoni ameeleza hayo wakati wa uzinduzi wa wiki ya usalama wa barabarani, inayoambatana na sherehe za miaka 50 tangu kuanzisha kwa Baraza la Usalama wa Barabarani.

Sokoni ameyasema hayo baada ya kuulizwa maswali na Makamu wa Rais Dk Philip Mpango wakati akikagua mabanda yaliyopo katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Dk Mpango alihoji ni askari wangapi na hatua gani wamechukua.Akijibu swali hilo, Sokoni amesema wamewakamata askari 168 ambapo wengine wameondolewa katika utumishi wa usalama wa barabarani, huku wengine wakichukuliwa hatua za kushtakiwa kijeshi na wengine wakipewa onyo.

Amesema askari wanane kati ya hao walifukuzwa kazi, 84 walionywa huku waliobakia wakihamishiwa katika vitengo vingine.

MWANANCHI
Kama ni kweli hiyo ni hatua nzuri wasidhani wakiwa kwenye sare hawagusiki.
 
Back
Top Bottom