TRC - SGR waongeze Treni za kwenda Dodoma kwa siku

TRC - SGR waongeze Treni za kwenda Dodoma kwa siku

Nkamu

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2007
Posts
226
Reaction score
91
Habari zenu wajumbe wenzangu wa jukwaa hili adhimu!

Nimekutana na changamoto hii kwa mara tatu sasa. Unaingia kwenye mtandao wa kukata tiketi wa SGR kutoka Dar kwenda Dodoma unakuta treni zimejaa siku mbili mbele. Hivyo kama una safari ya ghafla kwenda au kutoka Dodoma huwezi kutumia treni sababu linakuwa limejaa siku mbili kabla ya safari.

TRC ni shirika la kibiashara ambalo msingi wake ni kucheza kati ya mahitaji ya huduma na upatikanaji wake (Demand and Supply) ili uweze kupata faida kubwa. Kinachonisikitisha ni kwamba mahitaji ya huduma yapo ya kutosha lakini mfanyabiashara anayetafuta faida analala badala ya kuchangamkia biashara.

Kama treni zinajaa siku mbili kabla ya safari, maana yake ni kwamba watu wanahitaji TRC waongeze treni kwa ajili ya safari hizo. Inasikitisha kuona treni inafika Dar saa 3 asubuhi inaegeshwa mpaka saa 12 jioni ili iende Dom. Muda wote huo, watu wanatafuta usafiri hawapati, wanaishia kupanda mabasi kwa safari ya masaa 7 mpaka 8! Kama TRC wangeongeza angalau treni moja ya mchana ingeweza kuongeza uzalishaji kwa shirika na pia kuwapatia huduma wananchi wanaotafuta usafiri wa haraka.

Naiomba managementi ya TRC na wataalamu wao wa biashara, waache kazi za mazoea wasije wakawa kama UDART. Biashara ipo na wateja wapo wa kutosha wa kuifanya treni isafiri kila baada ya masaa manne kutoka na kwenda Dodoma.

Naomba kuwasilisha kwenu wanabodi!

1725060625356.jpeg

Pia soma:
 
Habari zenu wajumbe wenzangu wa jukwaa hili adhimu!

Nimekutana na changamoto hii kwa mara tatu sasa. Unaingia kwenye mtandao wa kukata tiketi wa SGR kutoka Dar kwenda Dodoma unakuta treni zimejaa siku mbili mbele. Hivyo kama una safari ya ghafla kwenda au kutoka Dodoma huwezi kutumia treni sababu linakuwa limejaa siku mbili kabla ya safari.

TRC ni shirika la kibiashara ambalo msingi wake ni kucheza kati ya mahitaji ya huduma na upatikanaji wake (Demand and Supply) ili uweze kupata faida kubwa. Kinachonisikitisha ni kwamba mahitaji ya huduma yapo ya kutosha lakini mfanyabiashara anayetafuta faida analala badala ya kuchangamkia biashara.

Kama treni zinajaa siku mbili kabla ya safari, maana yake ni kwamba watu wanahitaji TRC waongeze treni kwa ajili ya safari hizo. Inasikitisha kuona treni inafika Dar saa 3 asubuhi inaegeshwa mpaka saa 12 jioni ili iende Dom. Muda wote huo, watu wanatafuta usafiri hawapati, wanaishia kupanda mabasi kwa safari ya masaa 7 mpaka 8! Kama TRC wangeongeza angalau treni moja ya mchana ingeweza kuongeza uzalishaji kwa shirika na pia kuwapatia huduma wananchi wanaotafuta usafiri wa haraka.

Naiomba managementi ya TRC na wataalamu wao wa biashara, waache kazi za mazoea wasije wakawa kama UDART. Biashara ipo na wateja wapo wa kutosha wa kuifanya treni isafiri kila baada ya masaa manne kutoka na kwenda Dodoma.

Naomba kuwasilisha kwenu wanabodi!


Pia soma:
Mlisema tumepigwa kumbe ulikuwa unafiki tu eeh?
 
serikalini hakuna wabunifu wamejaa vilaza tupu, hawatumii ubongo wao vizuri. wataita waandishi waongee eti kuna abiria analipa buku anapanda dom hadi dar...hawawezi kubuni njia za kudhibiti wanazidiwa na wahudumu wa kwenye mabasi yaani. hawawezi kuendesha hilo treni...wanasogeza hadi mwakani waombee kura za urais wakipita treni itakufa tutaendelea na mabasi yetu...wahovyo sana tusiwaamini na huduma zao. mimi kuna siku sikuwa na tiketi na nilikuwa na safari ya kutoka dar kwenda dom...tiketi mtandao zilikuwa zimejaa...nikaenda tu station masaa matatu (3) kabla ya safari kuanza...nikawaeleza wahudumu kwamba nataka tiketi yaa dom..wakasema subiri...ipo ya moro....ukate uende moro alafu ukifika moro waeleze wahudumu wa ndani kwamba nilikata ya moro ila nataka fika dom ..yaani ushauri wananipa wenyewe eti utalipia nauli nyingine ya moro dom...na utaendelea na safari. Nikatulia mchuma hadi moro, moro hadi dom...sijui walizitafuna hela zangu zingine
 
Nilisikia walikuwa wanasema Dar-Mor.Treni 8 kwa siku,4 kwenda 4 kurudi,na Dar-Dom Treni 4 kwa siku,2 kwenda 2 kurudi,sasa sijui akili zao ndio zimegota au ni vipi,naona ni masuala ya kuadjust to hapo...
 
Jana nimesafiri na PM majaliwa, nikawa nasema Waziri wangu anaenjoy matunda ya mawazo yake na muasisi na mtekelezaji jembe JPM ila nikawa nawaza usikute anadondosha chozi kwamba angekuwepo boss wake JPM afaidi matunda ya kazi za mikono yake.
Ngoma saa mbili na dk 50 tupo Dar mapemaaaaaa
 
ama kwel chuma inakata upepo. kwa kweli naiwah had chai na karanga za Nyerere square.
mukaze hivo hivo hakuna kupanda na mamikate, wengine matenga ya kuku, wengine sijui maviroba ya magindi. Noo ile kama ndege ipewe eshima yake. Saf sana ili iwe safi muendelee ku monitor mamizigo yasioleweka.matenga sijui ya nyanya hapan.la. juz nimeambiwa oya acha chupa hapa nje. safi sana
 
Kabla ya kuongeza safari una monitor trend kwanza. Sasa hivi ni ngumu kwasababu watu wengi wanapanda tu ile kutoa gundu, kwahio huwezi kutumia hesabu hii kupanga idadi yavtreni kwa siku. Utafika muda watajua idadi ya abiria halisi kwa siku
 
Mimi nashauri nauli iwe laki 2 ili wengine waendelee kutumia mabasi
 
serikalini hakuna wabunifu wamejaa vilaza tupu, hawatumii ubongo wao vizuri. wataita waandishi waongee eti kuna abiria analipa buku anapanda dom hadi dar...hawawezi kubuni njia za kudhibiti wanazidiwa na wahudumu wa kwenye mabasi yaani. hawawezi kuendesha hilo treni...wanasogeza hadi mwakani waombee kura za urais wakipita treni itakufa tutaendelea na mabasi yetu...wahovyo sana tusiwaamini na huduma zao. mimi kuna siku sikuwa na tiketi na nilikuwa na safari ya kutoka dar kwenda dom...tiketi mtandao zilikuwa zimejaa...nikaenda tu station masaa matatu (3) kabla ya safari kuanza...nikawaeleza wahudumu kwamba nataka tiketi yaa dom..wakasema subiri...ipo ya moro....ukate uende moro alafu ukifika moro waeleze wahudumu wa ndani kwamba nilikata ya moro ila nataka fika dom ..yaani ushauri wananipa wenyewe eti utalipia nauli nyingine ya moro dom...na utaendelea na safari. Nikatulia mchuma hadi moro, moro hadi dom...sijui walizitafuna hela zangu zingine
Wewe unahujumu shirika hakafu uko humu unasema viongozi vilaza. Viongozi hata wakiwa Malaika kwa wanachi kama wewe nchi haiwezi kuendelea.
 
Muitikio wa chuma ya dodoma ni mkubwa sana. Kama watasimamia vyema mambo yataenda vizuri
 
Back
Top Bottom