TRC watoa majibu kuhusu uwapo wa Treni zenye Vichwa vilivyochongoka

TRC watoa majibu kuhusu uwapo wa Treni zenye Vichwa vilivyochongoka

Tanzania Railways Corp

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2018
Posts
251
Reaction score
595




TRC wakiwa kwenye ukaguzi wa Vichwa Nchini Korea Kusini wametoa ufafanuzi wa uwapo wa treni ambazo Vichwa vimechongoka kutokana watu kuhoji utofauti wa picha zilizopo kwenye matangazo ya TRC kutofautiana na Vichwa vilivyoonekana wiki iliyopita. Soma: Vichwa vya Treni za SGR vyawekwa hadharani

Zaidi ya hayo, Wataalamu na watengenezaji wameonekana wakiendelea kufanya matengenezo ya Vichwa hivyo pamoja na kutoa ufafanuzi wa namna Vichwa hivyo vitafanya kazi.
---
Muonekano wa maendeleo ya utengenezaji wa moja kati ya seti 10 za treni za Kisasa (EMU) kwa ajili Reli ya kisasa (SGR), zinazotengenezwa na kampuni ya Hyundai Rotem ya Korea ya Kusini, ambapo kazi za utandazaji wa nyaya za umeme, mfumo wa usambazaji hewa ndani ya treni na ufungaji wa vifaa vya kielektroniki zinaendelea.

Soma pia: Uzi mkuu unaoonesha yaliyojiri kwenye mradi wa SGR tangu kuanza kwake mpaka mradi ulipofikia hivi sasa

Kampuni hiyo ilipewa zabuni na Serikali ya Tanzania ya kutengeneza vichwa 17 vya treni vya umeme na seti 10 za treni za kisasa EMU.

Pamoja na kazi za utengenezaji wa treni hizo za kisasa, Hyundai Rotem kwa kushirikiana na Wataalam kutoka TRC wanaendelea na majaribio ya mifumo mbalimbali katika vichwa vya treni vya umeme, mjini Changwon, Korea ya Kusini.
 
Na hivyo vichwa vingine vya escape from sobibo mtavipeleka wapi?
Kaka vile kwa ajili ya freight train mbona ipo wazi. Angalia hata Transnet (South Africa) wanatumia kama vile ila hiyo video inaonyesha kabisa hizo ni EMU.
 
Kasema ni mjinga tu ndio ataweza kuamini kaweka hii picha
FB_IMG_1690217489268.jpg
 
Kaka vile kwa ajili ya freight train mbona ipo wazi. Angalia hata Transnet (South Africa) wanatumia kama vile ila hiyo video inaonyesha kabisa hizo ni EMU.
Nipe/ tupe elimu Mkuu kwanini serikali wanaleta vichwa vya aina mbili na vitatumikaje.
 
Nipe/ tupe elimu Mkuu kwanini serikali wanaleta vichwa vya aina mbili na vitatumikaje.
Huwezi tumia electric locomotives ambazo ni mahususi kuvutia treni za mizigo kwa treni hizo za seti (EMU train).

Unaweza tumia kuvutia mabehewa ya abiria kama yale yaliyopokelewa yenye ghorofa au mizigo tu.

Hizo unazoziona katika video ni treni za set ambazo zina vichwa mbele na nyuma na huwa mara nyingi na mabehewa 8 huwa si ndefu kwasababu zinakwenda kasi kubwa ndiyo kizungu wao huita Electrical Multiple Unit (EMU).

Nimejaribu kiasi si taaluma yangu.
 
🌍TRENI YA UMEME (SGR) SETI YA KWANZA YAFIKIA ASILIMIA 40.

Kwa kurejea Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2020-2025 Sura ya Pili inayoeleza juu ya Mapinduzi ya Uchumi kwa Maendeleo ya Watu, inaonyesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika miaka mitano kitaielekeza Serikali kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya Kimkakati. Miundombinu hiyo inajumlisha ya Reli, Viwanja vya ndege, na bandari, pia kuboresha huduma za usafiri wa anga, baharini na kwenye maziwa kwa kununua vyombo vipya vya usafiri na kukarabati vyombo vilivyopo.

Hii ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ambapo Serikali ya awamu ya Sita Chini ya Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imenunua treni ya Umeme yaani (SGR) ili kuongeza ufanisi na kasi katika usafirisha nchi kavu kupitia reli, ambapo ujenzi wa Seti ya kwanza umefikia 40% kati ya 10 zinazotengenezwa.

CCM inatekeleza kwa vitendo.

Imetolewa na;
Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM-Taifa.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-07-25 at 14.36.13.mp4
    23.1 MB
Back
Top Bottom