MR UNINFORMED
JF-Expert Member
- Sep 8, 2013
- 1,069
- 1,209
Mpaka nitakapokua tayari Financial sector itakua stable.Financial sekta ya Tanzania bado iko chini mnoo
Unachukua kila mwaka au nusu mwakaMtamba wa Panya,
Kuweka mtaji kwenye hati fungani ile faida ina ongezeka kwenye mtaji je nayenyewe ina pigiwa hesabu ya faida yake au utaruhusiwa kuwa unaichukua faida kila mwaka mtaji unabaki pale pale
Kuna Calculation wanafanya kwa kiwango cha iyo bond uliyoweka. Banks hawafanyi bihashara za asala, wao wanaangalia faida zaidiunaichukulia mkopo halafu unalipa ndani ya miaka 10 au
Huwezi kukopa zaidi ya 50% ya T-Bond uliyowekaWataalam wa uchumi wanasema "Compound interest is eighth wonder of the world" wengi wanaoenda kuwezeza kwenye hizi bond hawana elimu ya kutosha unakuta mtu anachukua 50m ana nunua gov-bond kwa 10yrs for 12%cp-interest. akipewa ile certificate anaenda kuficha kwenye droo yake ya chuma huko chumbani ana subiri miaka kumi iishe hajui kua anaweza kuitumia hiyo hiyo kupata mkopo hadi 75% invested money(50m). hamna kitu kinalipa kama investiment kwenye Money market, capital market na stock market.
Hata mm kunakitu nimepamga kufanya juu ya hii sector, sema haitabiriki
Na ndio maana ili soko la apa Tanzania wengi wanaogopa. Maana financially MTU kama anakopa kwa zaidi ya 80% ikitokea kashindwa kurejesha mkopo inakuaje na kashakaa na fedha kama miezi 6 au kutakuwa na term and condition ambazo wanaweza kucheki unamiliki assets gani nyingineHiyo inflation haiathiri faida ya hiyo biashara?
Mzeee unaandika kirahisi sana ...yani kma unakunywa maji vileMfano nimewekeza 700M maana yake kila mwaka nina 108M
Kwa miaka 20 nitakuwa nimetengeneza 108 kila mwaka
Swali je nikiwekeza 700M ninaweza tengeneza 108M?
Look kid
Ni bora niwekeze kwenye hizo Hati fungani
Sasa 108M nitaanzisha Ranch business
Mwaka wa kwanza 108M nanunua shamba lenye deed katavi huko lets say 50K per acre nanunua 2,000 acres natulia
Mwaka wa pili napata 108M napanda majani na irrigation system
Mwaka wa 3 napata 108M najenga nyumba na miundo mbinu ya kwenye ranch hiyo
Mwaka wa 4 nanunua ngombe sasa natafuta mbegu Bora naweza kuanza na ngombe 200
Mwaka wa 5 108M nunua eneo jingine la 2,000 acres
Yaani after 15 years
Nina mashamba ya acres 10,000 yenye ng'ombe 2,000
Sasa value ya kampuni ambayo inamiliki acres 10,000 na ng'ombe 2,000 kwa mwaka huo acha tu
Halafu 700 bado imetulia
Kaitaja Milioni 700 kama Tshs 700Mzeee unaandika kirahisi sana ...yani kma unakunywa maji vile
Kaitaja Milioni 700 kama Tshs 700
Vijana wetu bongo movie zinawaaribu Sana Akili
Mzeee unaandika kirahisi sana ...yani kma unakunywa maji vile
Fanya kunipa mbili tatu kutokana na uzoefu wako mkuu.Naongea sababu haya ndio maisha ninayoishi siongei sababu ni maisha ninayoyahisi
Hii statement ukiieleww ina fumbo kubwa sana la kimaisha
Hapa kikubwa kinachowasukuma wafanyabiashara ni ule msemo wa "usiweke mayai yote kwenye kapu moja" mkuu..... BIASHARA ni wazo zuri ila kama una pesa ya ziada inabidi kuipeleka kwingine na sio tu kuitegemea hio biashara ulionayo Ili kuongeza mifereji yako ya kipato.Hati fungani ni biashara "kichaa" na watu pekee ambao wanawekeza kwenye hii biashara ni wale waoga wakupoteza thamani ya mitaji ya pesa zao. Mabenki, mashirika ya bima, mifuko ya mafao pamoja na mashirika mengine bila shaka hutumia njia hii ya uwekezaji ili kutunza mitaji yao pengine ni kutokana na ukubwa wa mitaji ambao ni vigumu kuwekezwa kwenye sekta zenye "Higher Risk but greater return".
Tukichukulia mfano wa Hati fungani za miaka 20 za serikali zinazotoa riba ya 15.49% p.a: Angalia mtiririko ufuatao;
Tuchukulie umewekeza kiasi cha Tsh x kwa muda wa miaka hiyo 20, jumla kuu ya malipo utakayopata baada ya miaka 20 ni Tsh;
lakini kumbuka kuna kitu kimoja ambacho huzikumba FIAT Currency zote duniani, nacho ni Inflation au Mfumuko wa bei . Tukichukulia wastani wa 3.7% p.a (kwa mujibu wa takwimu za NBS [1], hapa naomba tusifikirie suala la "kupikwa" takwimu na naomba tuunge mkono juhudi) kwa muda wa miaka 20 hiyo ya uwekezaji wako. Then mtaji wako wa Tsh x baada ya miaka hiyo 20 utakuwa na thamani ya Tsh;
Hii inamaanisha faida ya uwekezaji wako kwa muda wa miaka 20 ni Tsh;
ambayo ni faida ya asilimia 100 kwa muda wa miaka 20; ambayo yenyewe kiuhalisia ni Tsh;
yaani kwa mahesabu ya "pesa yako ya kweli" ya miaka 20 iliyopita, faida yako ni asilimia 48.4 tu.
Hebu tuangalie mfano mwingine, iwapo mtu atawekeza kiasi kilekile cha Tsh x kwa muda wa miaka 20. Tukichukulia wastani wa faida ya asilimia 10 kwa mwaka, then baada ya miaka 20 mtaji wake utakuwa ni Tsh;
ambapo faida yako itakuwa ni Tsh;
yaani mara 4.659 ya mtaji wako wa awali, ambayo kiuhalisia ni faida ya Tsh;
yaani asilimia 225.3 kwa mahesabu halisi ya miaka 20 iliyopita.
sasa unaweza kuona kwamba kwa wastani wa faida ya asilimia 10 tu kwenye biashara yako kwa miaka 20 faida unapata asilimia 225.3 wakati kama utakuwa umewekeza kwenye hati fungani utakuwa umepata faida asilimia 48.4 tu japo utakuwa kwenye "risk free investment".
Je, kama utafanikiwa kupata faida ya wastani wa asilimia 20 kwa muda wa miaka 20 unaweza kupiga hesabu ni kwamba utapata faida kubwa zaidi. Yaani;
Baada ya miaka 20 mapato yatakuwa ni Tsh;
kumaanisha faida yako itakuwa ni Tsh;
ambayo kiuhalisia ni Tsh;
yaani faida ni mara 17.538 ya mtaji ulioanza nao "miaka 20 iliyopita"
Sasa unaweza kuona kwa faida ya kufanya biashara ukapata wastani wa 20% profit kwa miaka ishirini ni 1753.8% wakani hati fungani ni 48.4%.
Hakuna mfanyabiashara anayeelewa biashara akawekeza kwenye hati fungani labda kama hakuna namna na yeye anataka kulinda mtaji wake usishuke thamani.
Ahsanteni.
Treasury bonds ni hati fungani za serikali kwa maana kwamba unaikopesha serikali na yenyewe inakulipa taratibu kwa riba(kawaida huwa ni baada ya miezi sita au mwaka) ila mutual funds ni mfuko wa uwekezaji wa pamoja(kwa kwetu Tanzania ipo UTT-Amis) ambao sasa wenyewe unasaidia sisi wenye vipato vya chini na vya kati kuweza kuwekeza sehemu mbalimbali ikiwemo hizo hati fungani(Treasury bonds), akaunti za muda maalum(fixed deposit accounts), hisa(stocks) kwa wepesi na pia kupata faida na gawio(ama kimoja wapo) zuri zaidiHii treasury bonds na mutual funds tofauti yake ni nini?
Kwa mwakaiyo interest rate ya 12% ni kwa mwezi au kwa mwaka au kwa iyo miaka kumi? jibu