Treni ya Abiria ya TRC yaanguka Kigoma, Watu kadhaa wajeruhiwa

Treni ya Abiria ya TRC yaanguka Kigoma, Watu kadhaa wajeruhiwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
f26f2849-cd9d-40d6-a9c6-04a49ead0a10.jpg



15a00ccf-a042-49b7-9e3e-fbcdf2345add.jpg
Shirika la Reli Tanzania TRC linautaarifu umma kuwa treni ya abiria namba Y14 ikiwa na kichwa cha treni namba 9002, mabehewa 12 ya abiria, behewa moja la vifurushi (parcel) na behewa moja la breki imepata ajali kati ya Stesheni ya Kazuramimba na Uvinza mkoani Kigoma majira ya Saa 7.30 usiku tarehe 28 Agosti 2024.

Ajali imetokea baada ya mabehewa sita (6) ya treni kuacha njia na kupelekea majeruhi 70, wanawake 26 na wanaume 44. Treni ilikuwa na jumla ya abiria 571 wakisafiri kutoka Kigoma kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

TRC kwa kushirikiana na Kitengo cha Afya cha Mkoa wa Kigoma walifanikiwa kuwapeleka majeruhi katika hospitali ya Wilaya ya Uvinza kwaajili ya matibabu. Hali za afya za abiria zinaendelea kuimarika, majeruhi 57 tayari wameruhusiwa, nane (8) wanaendelea na matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Uvinza na watano (5) wamehamishiwa Hospitali ya Maweni kwaajili ya matibabu. Treni iliendelea na safari kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

Shirika linawapa pole majeruhi na linaendelea na jitihada za kuwahudumia. Hakuna taarifa ya vifo vilivyotokana na ajali, taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.
 
Itakuwa kuna watoto wametega sindano kwenye reli

poleni sana ndugu
 
Hik sgr inayotembea 170km/h inahitaji uangalzinwa kina sana la sivyo linaeza tokea jambo
 
Shirika la Reli Tanzania TRC linautaarifu umma kuwa treni ya abiria namba Y14 ikiwa na kichwa cha treni namba 9002, mabehewa 12 ya abiria, behewa moja la vifurushi (parcel) na behewa moja la breki imepata ajali kati ya Stesheni ya Kazuramimba na Uvinza mkoani Kigoma majira ya Saa 7.30 usiku tarehe 28 Agosti 2024.

Ajali imetokea baada ya mabehewa sita (6) ya treni kuacha njia na kupelekea majeruhi 70, wanawake 26 na wanaume 44. Treni ilikuwa na jumla ya abiria 571 wakisafiri kutoka Kigoma kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

TRC kwa kushirikiana na Kitengo cha Afya cha Mkoa wa Kigoma walifanikiwa kuwapeleka majeruhi katika hospitali ya Wilaya ya Uvinza kwaajili ya matibabu. Hali za afya za abiria zinaendelea kuimarika, majeruhi 57 tayari wameruhusiwa, nane (8) wanaendelea na matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Uvinza na watano (5) wamehamishiwa Hospitali ya Maweni kwaajili ya matibabu. Treni iliendelea na safari kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

Shirika linawapa pole majeruhi na linaendelea na jitihada za kuwahudumia. Hakuna taarifa ya vifo vilivyotokana na ajali, taarifa zaidi zitaendelea kutole
Duuuh!! Chanzo????
 

Treni ya abiria ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) iliyokuwa ikitokea mkoani Kigoma kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam imepata ajali.

Watu 70 wamejeruhiwa katika ajali hiyo kati ya 571 waliokuwa wakisafiri kwa treni hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TRC, Jamila Mbarouk katika taarifa kwa umma leo Agosti 28, 2024 amesema treni hiyo namba Y14 ikiwa na kichwa namba 9002, mabehewa 12 ya abiria, behewa moja la vifurushi (parcel) na behewa moja la breki imepata ajali kati ya Stesheni ya Kazuramimba na Uvinza mkoani Kigoma saa 7.30 usiku wa Agosti 28, 2024.

“Ajali imetokea baada ya mabehewa sita ya treni kuacha njia na kusababisha majeruhi 70, wanawake 26 na wanaume 44. Treni ilikuwa na jumla ya abiria 571 wakisafiri kutoka Kigoma kuelekea mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam,” imeeleza taarifa hiyo.
Snapinsta.app_457154123_909486101013757_6025060399019240545_n_1080.jpg
 
Poleni Sana
Hili Linaanguka Tu SGR Tutaiweza Kweli
 
Poleni Sana
Hili Linaanguka Tu SGR Tutaiweza Kweli
Kama wewe ni mtaalamu wa reli hiyo reli ya Kigoma ni narrow gauge,tena narrow gauge ya zamani sana toka enzi ya mkoloni.
Reli ilipotanduliwa na kutandikwa mpya ambayo ni continuos welded ilitandikwa mwisho Tabora.
Kutoka Tabora kwenda Katavi,Mwanza,Kigoma bado hakujatanduliwa kuwekwa reli mpya.
Na pia upande wa Tanga Arusha nao haujatandikwa reli mpya.
Uchakavu wa reli ndio chanzo cha hizo ajali.
Width ya standard gauge huwezi kufananisha na width ya narrow gauge.

Hivyo usifananishe hivyo vitu mkuu.
 
Back
Top Bottom