Treni zote za SGR Kupewa majina ya Viongozi

Itafika wakati nitaweza kushuka uwanja wa ndege wa Nyerere, nikapita barabara ya Nyerere, nikavuka daraja la Nyerere, na kwenda chuo cha Nyerere kisha nikaenda ukumbi wa mikutano wa Nyerere, nikapanda treni la Nyerere mpaka Mwanza, nikapita barabara ya Nyerere, nikafanya shughuli zangu na kumaliza, nikapanda ndege mpaka bwawa la Nyerere, nikaenda kupumzika mbuga ya Nyerere.
 
toa mbadala, unataka nini kifanyike
 
Kupitisha mizigo kwenye rail inayopitisha train ya abiria ni kuua hiyo reli haraka sana,gharama za matengenezo ya reli itakuwa kubwa sana,na reli ikishaanza kuharibika wajuwe kuwa hata speed ya train itakuwa ndogo kwa kukosa uimara.Pia kutakuwa na maswala ya kusubiria kupishana hili nalo litasababisha kuchelewa kwa hizi train kila wakati......
 
Hizi kelele zenu siyo majina, Kuna kitu/vitu vingine vimewakwaza jichunguzeni na mjihoji, kwani hata likiitwa kimya kimya kama Mimi shida iko wapi? Kwani litreni la umeme linapiga kelele, Mimi sijawahi kuliona huku Kahe station sijui ni rais awamu ya ngapi atatuletea
 
Tuna milima maziwa mito hata migodi kwanini tusitumie majihayo mfano Kilimanjaro shelui Victoria Serengeti selu nk nk mbona itapwndeza zaidi.
 
Hao ni wapuuzi, majina ya mbuga za wanyama yameisha, milima, mito na maziwa hawayaoni? Angalau itasaidia kutangaza utalii!
 
Watu wengine kujidhalilisha hawajui yaani anatangaza hadharani kabisaa sasa majina ya viongozi wa nini kwa mfano
Wanaona marehemu wanafaidi sana kuandikwa majina yao sehemu mbalimbali.
Ukiona mtu anamuonea wivu hata marehemu ujue huyo hata kuwa kiongozi hafai.
Wasubili itafika zamu yao wataandikwa.
 
Maneno mengiiiii

Huko mbeleni sasa

Ova
 
Wanaona marehemu wanafaidi sana kuandikwa majina yao sehemu mbalimbali.
Ukiona mtu anamuonea wivu hata marehemu ujue huyo hata kuwa kiongozi hafai.
Wasubili itafika zamu yao wataandikwa.
Mie nakubali majina yote ila samia express hili hakuna kabisa treni ise geuka chura kiziwi
 
Ondo upuuzi wako hapa mkuu.
Kunawatu hawastahili majinayako kukumbukwa kabisa na yanatia kinyaasana.
Nyerere ni Baba wa Taifa, na Kikwete ndio mwanZilishi wa project ya SGR Tanzania, upuuzi hapa ni upi ? Twende na facts tafadhali.
 
Usipotoshe, reli ina kiwango cha tani zinazotakiwa kupita juu yake bila kujali ni watu au mizigo.
Kumbuka mizigo inayopakiwa kwenye treni inapimwa ili kutozidisha kiwango cha tani zinazotakiwa kupita juu ya reli.
 
Ulivyo mnafiki likiandikwa jina la Mbowe au Lisu utakuwa wa kwanza kukata mauno ya pongezi.
Watu kama wewe mnaendeshwa na chuki ambazo mnazificha nyuma ya mgongo wa siasa.
Wananchi tunachotaka ni huduma bora hayo mengine ni upuuzi.
 
Bora isiwepo tu lot ya Isaka-Rwanda badala yake Isaka pawepo Bandari Kavu ya mizigo ya Rwanda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…