True story: Jinsi nilivyopambana kutafuta mali za Mjerumani mkoani Morogoro, mauzauza na vimbwanga nilivyokutana navyo

True story: Jinsi nilivyopambana kutafuta mali za Mjerumani mkoani Morogoro, mauzauza na vimbwanga nilivyokutana navyo

Huyu jamaa na story zake kule makete sijui njombe kulee

Akaingia misituni huko, mara wakapotea akakutana na minyoka.. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sasa analeta hadithi zile zile za kutafuta mali za wazungu.

Aisee.
 
IMG_20210815_121212_407.JPG

LUWALE utanikuta pangoni nakusubiri....
 
SEHEMU YA 4
Baada ya kufahamu formula zao, nikapanga siku kuingia katika mapango yale. Ila kabla sijaingia nikaenda ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro maana nilisikia kama ukiwa wa kwanza kutoa taarifa ya kuwepo kwa madini eneo fulani basi ukigundua wewe unapewa fungu kubwa sana na serikali.

Ukweli nilifika kwa mkuu wa mkoa na nikaandikisha jina la kwenye kitabu cha watu waliofika kumuona. Nashukuru sna baada ya kumueleza nia yangu ya kutafuta mali hizo alinitia nguvu sana na kuniambia taarifa za kuwepo kwa madini katika mkoa wangu yapo sehemu nying sana hivyo kama utahitaji msaada wowote basi uje na nitakupatia. Miaka ile Moro walipata mkuu wa mkoa mwelevu sana.

Aliniamasisha sana basi safari yangu ilianza siku ya pili yake huku nikiwa na ndoo ya lita 20, nyundo imara ya kuvunjia jiwe lenye mercury pamoja na tochi. Maana nilivyoelezwa mercury inatokea kwenye jiwe

Nikaona haina haja ya nyimbo wala ngoma, ngoja niiingie mchana kweupe kwenye yale mapango. saa 2 asubuhi nikafika mlimani pale nikisikia sauti za ndege na wala hilo joka sikuliona. nikapanda mlima kidogo nikaona pango, nikafurahi sana nikaona leo nimeshapata mali.

kwa nje pango lilionekana dogo mwanamme nikaingia.... huku nikiwa makini sana kutafuata jiwe nilitegemea litakuwa kwa juu
nilivyosogea mbele kidogo huku mwanga ukianza kupotea nikakuta kuna mapango matatu, hapa nilijilaumu sana kwa nini sikuuliza vizuri, sasa hapa naingia pango lipi leneye mali?

mawazo yakanipa niingie hili la kati kati... mwanamme nikajitosa hapo huku nikiwa nimewasha tochi yangu.... ndani ya lile pango kulikuwa kimya sana na kadri nilivyotembea nilihisi hata mchanga unabadirika. lile pango lina kipengo kikubwa sana na kulikuwa na ubaridi ndani ya lile pango. nikaanza kumulika tochi kwenye ule mchanga ni kweli upo tofauti kwani weneyewe ni laini sana na kuna sehemu unang'aaa sana nikasogea zaidi na zaidi huku nikitafuta jiwe... nilitembea kama urefu wa kiwanja cha mpira ndani ya pango....mbele nikaona niaona vitu sikuelewa vinaruka ruka ni mithili ya kundi kubwa la ndege.

Nitaendelea
Hii chai kabisa na ishapoa mapema kabisa
 
SEHEMU YA 5

Naomba niendelee kidogo leo kwa wale wanaofuatilia. Maisha usikate tamaa. Jaribu kila linalowezekana ingawa tu kiwe ni cha halali na usizulumu mtu. Mungu si athumani. Mgaa na upwa hali wali mkavu..

Basi mbele niakona kama kiza hivi na ilikuwa ni ishara ya kundi kubwa sana la ndege mbele yangu ndani ya pango. sikukata tamaa na wala sikuogopa kwani niliamnini nipo peke yangu mle ndani na nilijua wadudu watakuwepo, pamoja na huyo mlinzi niliyoambiwa. nikasogea kwenye lile kundi niliamni labda ndipo ilipo. kumbe pale mahala kwa chini kama bonde lenye mchanga mzuri sana yaani kama mtu unashuka bonde ndani ya pango na upandishe uwafikie popo ni kama mlima fulani hivi. basi kuangalia vizuri lile kundi ni kweli walikuwa ni popo wengi wamejaaa mahali pale kuangalia vizuri lile bonde ni kubwa na limeenda mbali kiasi kisha likapanda ni mlima mdogo hivi. mara mchanga ukaanza kama kuelekea bondeni na huku popo wakiruka ruka pale mahala walipo. wazo likanijia nitafikaje kwenye lile kundi la popo na hapa chini kama nikitembea uwenda nikaseleleka na mchanga mpaka bondeni lakini nitaweza kupanda na kufikia mahala pale. pale nilipo na popo walipo ni kama mita 20 hivi lakini kuna kama kaponde yaani mlima ushuke halafu upande ila ni michanga mitupu hakuna hata mawe ya kukanyaga.

niaona ngoja nirushe mchanga au nipige ukelele niwashtue wale popo wakimbie nione kama hilo jiwe la mercury lipo hapo. haraka likanijia wazo...nina plastic ya lita 20 basi labda nikiipiga kwa nguvu popo watatoweka pale halafu huyu bibi pia anapenda ngoma.....

Nilivyoanza kupiga ndoo yangu nikaanza kuhisi usingizi na nilijawa na hamasa ya kuendelea kupiga hiyo ndoo kwa lengo la kuwatimua wale popo...kadri nilivyofanya ndio usingizi ulizidi kunishika

Nitaendelea sehemu ya 6 na ndipo vimbwanga vilipoanza kama ni muoga quit....
 
SEHEMU YA 5

Naomba niendelee kidogo leo kwa wale wanaofuatilia. Maisha usikate tamaa. Jaribu kila linalowezekana ingawa tu kiwe ni cha halali na usizulumu mtu. Mungu si athumani. Mgaa na upwa hali wali mkavu..

Basi mbele niakona kama kiza hivi na ilikuwa ni ishara ya kundi kubwa sana la ndege mbele yangu ndani ya pango. sikukata tamaa na wala sikuogopa kwani niliamnini nipo peke yangu mle ndani na nilijua wadudu watakuwepo, pamoja na huyo mlinzi niliyoambiwa. nikasogea kwenye lile kundi niliamni labda ndipo ilipo. kumbe pale mahala kwa chini kama bonde lenye mchanga mzuri sana yaani kama mtu unashuka bonde ndani ya pango na upandishe uwafikie popo ni kama mlima fulani hivi. basi kuangalia vizuri lile kundi ni kweli walikuwa ni popo wengi wamejaaa mahali pale kuangalia vizuri lile bonde ni kubwa na limeenda mbali kiasi kisha likapanda ni mlima mdogo hivi. mara mchanga ukaanza kama kuelekea bondeni na huku popo wakiruka ruka pale mahala walipo. wazo likanijia nitafikaje kwenye lile kundi la popo na hapa chini kama nikitembea uwenda nikaseleleka na mchanga mpaka bondeni lakini nitaweza kupanda na kufikia mahala pale. pale nilipo na popo walipo ni kama mita 20 hivi lakini kuna kama kaponde yaani mlima ushuke halafu upande ila ni michanga mitupu hakuna hata mawe ya kukanyaga.

niaona ngoja nirushe mchanga au nipige ukelele niwashtue wale popo wakimbie nione kama hilo jiwe la mercury lipo hapo. haraka likanijia wazo...nina plastic ya lita 20 basi labda nikiipiga kwa nguvu popo watatoweka pale halafu huyu bibi pia anapenda ngoma.....

Nilivyoanza kupiga ndoo yangu nikaanza kuhisi usingizi na nilijawa na hamasa ya kuendelea kupiga hiyo ndoo kwa lengo la kuwatimua wale popo...kadri nilivyofanya ndio usingizi ulizidi kunishika

Nitaendelea sehemu ya 6 na ndipo vimbwanga vilipoanza kama ni muoga quit....
Mkuu mmh! Natamani kusema kitu ila Behaviourist atapata sababu ya kunisema 😃😃😃 acha ninyamaze.
 
Back
Top Bottom