Tetesi: Trump afadhaika kukatazwa kutumia simu zake

Tetesi: Trump afadhaika kukatazwa kutumia simu zake

Mmmmh hiyo kunyang'anywa simu mbele za watu umetunga tu na pamoja na usalama wa rais lakini anakuwa na mambo yake binafsi na kwa marekan rais anaruhusiwa kuchagua mtu yeyote wa karibu yake,anaitwa first officer kama sikosei.
Hiyo kauli ilitolewa na Obama mwenyewe, kwamba alinyang'anywa simu mbele ya other officers alipotaka kuitumia. Yeye alikabidhiwa simu ya kutumia na akaelezwa kwamba atakua akitumia simu hiyo kuanzia siku hiyo. Alipotaka kufanya mawasiliano na marafiki zake, akaamua kuchukua katia ya simu zake binafsi ndipo akanyang'anywa mbele ya maofisa wa Ikulu. Sasa kama Obama alidanganya, hilo ni suala lingine.
 
Hii mbona sio siri mkuu.Sema kwa kuwa WaTz kusoma ni kama kituo cha polisi.Ninalosema nimelihakikisha.Hebu google "Trump agrees to pay US $ 25 million in Trump University Settlement." Usipende sana ukawa kipofu mkuu.
Acha kupotosha wewe, rudi kasome chanzo cha yeye kulipa faini alafu irudi tena
 
Iwe kweli ama uongo,huyu mzee ana vituko sana...Si ajabu kumkuta twitter anajibizana na watu ''disaini'' ya Rosie O'donnell..
 
Mkuu Miungu ipo mingi inategemea tu yeye kamkusudia Mungu yupi maana hata Ng'ombe na sanami ni Mungu kwa imani zingine na anahitaji ulinzi.
Duh ni kweli mkuu umenikumbusha kama ni wa upande huo yuko sahihi.
 
Nakumbuka Obama naye alilalamika sana. Alisema anakatzwa kila kitu na kubadirishiwa kila kitu, na kwamba ni kama amekatazwa maisha aliyoyazoea na watu aliozea kuwasiliana nao. Na kuna siku alitaka kutumia simu tofauti jama wa secrete service alimnyang'anya mbele ya watu.
Duuhh jama wako serious na kazi yao sana!!!
Kwa mantiki hii hata kazi zingine wanazifanya kwa umakini wa aina hii, na kama ni hivi maendeleo sisi tusahau kwa havi karibuni!!!
Je wa kwetu wanaujasiri wa kumnyang'anya rais wetu pale anapo potoka kidogo?
 
kwa nin backberry na sio iphone[/QUOTE
Blackberry ni simu ya kufinyafinya ya kawaida kama zile za namba na herufi. Na zinamilikiwa na kampuni maalumu toka Canada.
Mawasiliano mengi kupitia humo yanawapa kibarua maafisa wa KI USALAMA duniani kujua ni nini mtu anaongea na ni ujumbe gani ameandika!

Serikali za Marekani miongoni mwa serikali zingine duniani ZILIISIHI sana CANADA iwape namna ya kuweza KUPENYA utaalamu wao kwa ajili ya usalama wa nchi zao.Zikiwemo India na nchi za Uarabuni kama Saudi Arabia. Canada ilikataa. Na kila nchi inajaribu kupenya hiyo technolojia. Sina uhakika kama Canada wamewasaidia.

Lakini kwa ufupi ni SIMU SALAMA SANA isiyopenyezwa na MTU MWINGINE!! Kwa nchi ya Canada hapo ni Kiboko yao.

Hizi simu za kupangusa hazina USALAMA wowote YEYOTE anaweza kuingia na KUIBA DATA zako ikiwa ni pamoja na contact na SIRI zako zote!
Simu hizi za kisasa kama iphone na zote za kupangusa Android hazina USALAMA!
 
Kama ilivyo kila wakati Rais mpya anapoingia madarakani huko Marekani hupewa masharti ya kiusalama ambayo ni LAZIMA ayazingatie.

Rais mteule Donald Trump amekatazwa na wataalamu wa kiusalama wa WHITE HOUSE kwamba hataruhusiwa kuitumia simu yake simu zake za SMARTPHONE -za Kupangusa (Android) akiwa IKULU na hata kaba hajaingia IKULU ya White House!

Badala yake ameambiwa atumie Blackberry na simu maalumu atakazo pewa na wataalamu wake wa kiusalama kama vile Obama naye alivyokatazwa na kuanza kutumia Blackberry mara tualipochaguliwa kuwa rais!

Backberry inadaiwa ni salama.Maana iko ENCRYPTED - Mawasilano yaliyovurugwa.
Mtu mwingine hawezi kuelewa mnachoongea ila ni yule tu anayepigiwa simu ndo ataelewa.
Hii ni kuzuia USIRI wa Rais Trump na Ikulu ya White.

Tukio hili limemfadhaisha sana Trump na kulalamika akisema atapoteza marafiki zake aliozoea kuongea nao.
Na unajua Marekani watu wa usalama wa Rais -SECRET SERVICE nk ndo walio na usemi wa mwisho kuhusu usalama wake

Swali Trump atawezaje mambo ya utawala na biashara zake bila simu zake hizo?
Maana amehuzunika sana!
Kwani phone book imefutika si ahamishie namba huko
 
Kwani phone book imefutika si ahamishie namba huko
Akiiweka ON Majasusi wataingilia simu yake.
Hana namna ila ku comply.
Rais wa zamani wa Misri Mubarak kabla hajaondoka madarakani aliwahi kusema. "Maisha ya URAIS ni kama JELA wale wanaotamani kiti hiki hawajui kifungo kilichoko katika URAIS.Huna muda wako wa binafsi ni tabu kubwa"
 
Back
Top Bottom