Trump akimwambia Paul Kagame out, Ni dhahiri nchi zetu si lolote kwa Kagame?

piyonerer

Member
Joined
Feb 5, 2025
Posts
36
Reaction score
77
Tarifa iliyopo huko X (Twitani) ni kwamba, muda wowote PK ataanza kuchezea vikwazo na ama kufurushwa kabisa ikuluni na hawa walezi wa dunia hii

Swali ni kwamba, nchi za Africa haziwezi kabisa kuadabishana mpaka tuingiliwe na watu dunia ya mbaali huko?

Kama ndivyo, Je, Africa inaouwezo sasa, kuzuia wazungu wasitutawale tena?

Kama tu migogoro yetu mpaka iamliwe na wazungu, tunalipi sasa?

Nguvu ya AU iko wapi?
 
ni kipi waafrika wanakiweza!? labda wizi wa mali ya umma
 
Swala la muda tu wakubwa watakaa kujadili bara lote la Afrika na nchi zote omba omba, watutawale vipi halafu kila kitu watatoa bure kwa masharti fulani.
 
Africa bado tunatawaliwa na wazungu kupitia ukoloni mambo leo. Ikitokea raisi wa nchi akaupinga huo mfumo maisha yake yanakuwa hatarini. Eg ibrahim traole n.k
 
DRC wamepigana na kuuana Tangu Kagame akiwa mtoto wa Mwaka 1.

Acheni visingizio kwa Kagame.
Tujikite Kutafuta namna ya kuborshe maisha ya watu wetu umasikini wa kutupwa, Huduma bora za afya. Elimu Duni Rushwa na ufisadi uliokithiri au na hivi vyote ni Kagame amesababisha?
 
Una hoja nzuri, ila umeamua kujiziba masikio usisikie kile Trump anasema kuhusu Kagame?

Umasikini kuuondoa, viendane na kutovamia hovyo nchi za wengine
 
Huu mfano wako mkuu, mbona haviendani na hoja iliyopo mezani?
 
Kila tendo la ndoa huwa na kondomu yake,hurudii kondomu
 
Kama wamekuwa wakipigana wenyewe kwa wenyewe , kwa nini PK aingilie kati huo ugomvi kwa kisingizio cha kutetea kabila lake lililo ndani ya nchi nyingine. Yeye amekuwa nani?
 
Waafrica wakikorogwa kidogo tuu wapo kama nyumbu haihitaji akili nyingi sana kujua kitu kitakacho tukuta sisi kama Waafrica. Na kama kuna kitu cha kujifunza japo wamechechelewa ni hizi mtu 4. SA, Burundi, Rwanda na DRC. Next time kama itakuwepo basi hawata pima kina cha maji kwa kuingia wazima wazima. Ndio maana nchi zenye kujielewa hawakutaka kutia pua zao huko. Angola kabembelewzwa sana ila hola, hakuna kitu kizuri kama kuwa na msimamo na kutetea bila kupepesa macho kile unachokiamini.
 
si nchi zote afrika zitaunga mkono kumuadabisha kagame...kuna nchi zitaungana na rwanda kitakachotokea hapo ni majuto ni mjukuu
 
Swala la muda tu wakubwa watakaa kujadili bara lote la Afrika na nchi zote omba omba, watutawale vipi halafu kila kitu watatoa bure kwa masharti fulani.
Na iwe hivyo hata leo, ni heri hao kuliko hawa wa kwetu, hao wa dunia ya mbali wanajali afya zetu, wanajali usalama wetu, wanajali uchumi wetu, wanatusaidia kwa vyote hivyo, halafu hawa wa kwetu wanaviiba na kutafuna na familia zao,kinachobaki wanakibeba na kukipeleka huko huko kwa waliotusaidia wakiomba wasaidiwe KUFICHA. What a mess?
 
Mkuu hakuna mtu anajali mtu pasipo maslahi mzungu anapokuja kwenye nchi kwa minajili ya kusaidia amenusa fursa au anaitafuta. Mtu anaeweza kusaidia nchi ni wananchi wakiweka nguvu zao pamoja na viongozi wao. Tatizo ninaloliona ni wananchi kuacha kuhoji mambo yanayowahusu kwa kudhani kuwa somebody will do it. Nchi zetu umma hauna nguvu ndio maana hata kiongozi wa ngazi ya chini anaweza kutamka kauli tata na watu wamebung'aa tuu bila kuhoji.
 
Muamar Gadafi aliambiwa na USA ajiuzulu akagoma nchi ikasambaratishwa. Charles Taylor wa Liberia aliambiwa ajiuzulu akajiuzulu nchi ikapona. Je Kagame atatii amri?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…