Trump Amuondolea Joe Biden Haki Ya Kupatiwa" Taarifa Za Siri/Classified Informations "Kama Ilivyotakiwa Kwa Maraisi Waliotangulia Wa Marekani

Teh teh 😃 😃 😃 kisasi hiki... Trump ni kituko cha wamarekani.

Kiranga Yoda
 
Kuna vitu Yuko sawa lakini vingine vingi anakurupuka
hakuna analolifanya ambalo halikuwa kwenye mpango wake. Hata kwenye kampeni zake alikuwa akiyasema. Na usisahau Trump ameingia madarakani mara ya pili, hivyo anayajua mengi. Huwa ninawakubali sana watu wasio wanafiki. "They say what they mean, and they mean what they say"
 
Namkubali sana lakini Kuna mambo kama haya ya kutaka kuzichukua Greenland, Canada na Gaza naona kama vile anataka kuleta sintofahamu na pia kumuingiza mtu kama Elon Musk kwenye serikali yake ni kama vile anaishusha hadhi heshima ya serikali yake
 
Teh teh 😃 😃 😃 kisasi hiki... Trump ni kituko cha wamarekani.

Kiranga Yoda
Katika security kuna principle ya "need to know". Yani unapewa information kama tu una haja maalum ya kujua.

Sasa ex president kashastaafu, ana haja gani ya kujua ma siri ya usalama ya nchi ya kila siku?

Moja ya sababu za kustaafu ni kupumzika kutoka kwenye mzigo wa kazi za kulitumikia taifa. Sasa mtu akistaafu halafu mkiwa mnampa ripoti za security kila siku si mnaondoa maana ya kupumzika hapo, mtu anakuwa anapata ma pressure ya kujua matatizo ya security kama yupo kazini wakati kashastaafu.

Pia, katika security kuna kitu kinaitwa "attack surface reduction", yani unapunguza nafasi ya habari kuweza ku leak kwa kupunguza wanaokuwa na hizo habari (by using the principle of "need to know"). Hapa walichofanya ni "attack surface reduction". Ma ex president ni wazee, wanaweza kujisahau wakaacha sensitive information zika leak bila kutaka.

Hawana haja ya kuwa na hizi habari.

Wangewaondolea mzigo huu ex presidents wote tu.
 
Sababu yenye uzito zaidi ni Biden kuwa na matatizo ya kusinzia sana, shida ya kukumbuka mlango ulipo, shida ipo hadi anasahau anachoongea, n.k. itakuwaje akipewa taarifa sensitive za ulinzi wa nchi
Atazisahau mezani sio?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…