Trump aongeza kodi kwa bidhaa za China, Canada na Mexico. Aitishia Japan

Trump aongeza kodi kwa bidhaa za China, Canada na Mexico. Aitishia Japan

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Rais Trump ameendeleza ubabe na kuendelea kupunguza mahusiano ya Marekani na mataifa mbalimbali:

Marekani, chini ya Trump, kwa muda mfupi imejenga mazingira ya kupunguza mashirikiano dhidi ya mataifa ya Ulaya, Asia, America na Afrika.

1. Kwa Afrika, Trump amefuta misaada.

2. Kwa Ulaya, Trump amejiondoa kuisaidia Ukraine kwenye vita yake dhidi ya Mvamizi Russia.

3. Kwa Asia, Trump aliongeza kodi kwa 10% kwa bidhaa zote toka China, na sasa ameongeza tena 10%; kwa hiyo ni ongezeko la 20%. China imesema ipo tayari kujadiliana na USA kuhusu kodi, lakini haitakubali kuburuzwa. Trump pia ameionya Japan kuwa inashusha thamani yake ya fedha, na hiyo inasababisha bidhaa za Marekani kuonekana aghali sana. Japan imekataa kuwa huwa haishushi thamani ya pesa yake.

4. Kwa America, ameweka kodi ya 25% ya bidhaa kutoka Canada na Mexico. Canada imesema na yenyewe italipiza kisasi.

5. Kwa Dunia, Trump ameiondoa USA kwenye uwanachama wa WHO, anafikiria kuiondoa USA kwenye Umoja wa mataifa na taasisi zake zote.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuna dalili ya Trump na Putin kutengeneza umoja wao. Lengo ni kuifanya Dunia nzima kuwa chini ya mataifa haya yenye nguvu za kijeshi, Marekani na Russia.

Dunia ijiandae kwa mpangilio huu mpya wa Dunia unaoweza kutokea ambao utakuwa wa block ya mataifa makubwa mawili ya Dunia, dhidi ya China na mataifa madogo madogo.
 
Trump ana akili sana. Hivyo ambavyo USA walikuwa wanafanya havikuwa na sustainability ya muda mrefu. Anaondoa ujinga kuja kwenye ukweli. Ila mijinga itasema eti uhusiano hahaha. Let America nayo aifanye iwe yenye ushindani
 
Shida ni kwamba wenzake wanamzoom tu maana tofauti na Russia ambako Urais ni wa milele ila huko USA Baada ya miaka yake 4 kupita wanakuja kuondoa uchafu wake wote.

NJE YA MADA: Tulikuwa tunaambiwa USA inaendeshwa na katiba/taasisi na siyo mtu sasa mbona Trump mmoja tu anajifanyia atakavyo?
 
Trump kuna sehemu naona fuse zimeanza kukatika upande wa rejeta na taa za kumulika
Punguza ukali wa maneno. The guy is so good at what he's doing.

Trump anaisafisha dunia. Trump anatufundisha Afrika kujitegemea wenyewe.

Ukreni inaelekea kusalimisha rasilimali zake kwa sababu ya kuishi kwa kushikiwa akili na mataifa mengine.
 
Tunatoka kwenye milindimo ya mwambao wa pwani, bongo Flava na wabanapua wote na kurejelea boom bap... Hip to Hop... ni mwendo wa Moooove b*tch... get out of the way....
 
Marekani kuumgana na Russia hiyo haipo na haitakuja kutokea.

Baada ya Trump Marekani itakua na kazi ngumu sana kushawishi na kurejesha mahusiano yake na mataifa mengine.

Kuhusu kuondoa misaada Africa, hiyo ni safi.
 
Anafanya jambo jema kwa nchi yake, sisi tukae kwa kutulia tusubiri nini dunia inataka kufanya, hatuna la kufanya.
 
Trump yuko sahihi, kaukubali ukweli, kupambana na China kiuchumi ilipofikia na mwenendo wa US ulivyokua, ilikuwa nimiaka michache tu mbeleni US inapigwa K.O... ngoja tuone kama hizi juhudi zitazaa matunda..
 
Rais Trump ameendeleza ubabe na kuendelea kupunguza mahusiano ya Marekani na mataifa mbalimbali:

Marekani, chini ya Trump, kwa muda mfupi imejenga mazingira ya kupunguza mashirikiano dhidi ya mataifa ya Ulaya, Asia, America na Afrika.

1. Kwa Afrika, Trump amefuta misaada.

2. Kwa Ulaya, Trump amejiondoa kuisaidia Ukraine kwenye vita yake dhidi ya Mvamizi Russia.

3. Kwa Asia, Trump aliongeza kodi kwa 10% kwa bidhaa zote toka China, na sasa ameongeza tena 10%; kwa hiyo ni ongezeko la 20%. China imesema ipo tayari kujadiliana na USA kuhusu kodi, lakini haitakubali kuburuzwa. Trump pia ameionya Japan kuwa inashusha thamani yake ya fedha, na hiyo inasababisha bidhaa za Marekani kuonekana aghali sana. Japan imekataa kuwa huwa haishushi thamani ya pesa yake.

4. Kwa America, ameweka kodi ya 25% ya bidhaa kutoka Canada na Mexico. Canada imesema na yenyewe italipiza kisasi.

5. Kwa Dunia, Trump ameiondoa USA kwenye uwanachama wa WHO, anafikiria kuiondoa USA kwenye Umoja wa mataifa na taasisi zake zote.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuna dalili ya Trump na Putin kutengeneza umoja wao. Lengo ni kuifanya Dunia nzima kuwa chini ya mataifa haya yenye nguvu za kijeshi, Marekani na Russia.

Dunia ijiandae kwa mpangilio huu mpya wa Dunia unaoweza kutokea ambao utakuwa wa block ya mataifa makubwa mawili ya Dunia, dhidi ya China na mataifa madogo madogo.
Wamuwahi huyo kichaa kabla hajaivua nguo kabisa marekani
 
Tunatoka kwenye milindimo ya mwambao wa pwani, bongo Flava na wabanapua wote na kurejelea boom bap... Hip to Hop... ni mwendo wa Moooove b*tch... get out of the way....
zaid ya yote tunairudisha hip hop kwenye misingi yake, akina kendrick lamar wajipange.
 
Nchi za ulaya nazo tunawaomba pia wafute misaada yote Kwa Africa.... haiwekani pesa za misaada nitumike kwenye upuuzi wa birthday ya mama
 
Rappers wote watataga, Mcee Donald Trump anachana kama KRS one, Rakim, Talib Kweli, Guru....
muongezee na pac, nakupa nafasi ya kulala kwenye kochi langu halafu unaninyanyulia bega??, kenge wahed.
 
Rais Trump ameendeleza ubabe na kuendelea kupunguza mahusiano ya Marekani na mataifa mbalimbali:

Marekani, chini ya Trump, kwa muda mfupi imejenga mazingira ya kupunguza mashirikiano dhidi ya mataifa ya Ulaya, Asia, America na Afrika.

1. Kwa Afrika, Trump amefuta misaada.

2. Kwa Ulaya, Trump amejiondoa kuisaidia Ukraine kwenye vita yake dhidi ya Mvamizi Russia.

3. Kwa Asia, Trump aliongeza kodi kwa 10% kwa bidhaa zote toka China, na sasa ameongeza tena 10%; kwa hiyo ni ongezeko la 20%. China imesema ipo tayari kujadiliana na USA kuhusu kodi, lakini haitakubali kuburuzwa. Trump pia ameionya Japan kuwa inashusha thamani yake ya fedha, na hiyo inasababisha bidhaa za Marekani kuonekana aghali sana. Japan imekataa kuwa huwa haishushi thamani ya pesa yake.

4. Kwa America, ameweka kodi ya 25% ya bidhaa kutoka Canada na Mexico. Canada imesema na yenyewe italipiza kisasi.

5. Kwa Dunia, Trump ameiondoa USA kwenye uwanachama wa WHO, anafikiria kuiondoa USA kwenye Umoja wa mataifa na taasisi zake zote.

Wachambuzi wa mambo wanasema kuna dalili ya Trump na Putin kutengeneza umoja wao. Lengo ni kuifanya Dunia nzima kuwa chini ya mataifa haya yenye nguvu za kijeshi, Marekani na Russia.

Dunia ijiandae kwa mpangilio huu mpya wa Dunia unaoweza kutokea ambao utakuwa wa block ya mataifa makubwa mawili ya Dunia, dhidi ya China na mataifa madogo madogo.
HUyu
Mwehu
Chizi

Naturahia kuona wamarekan wamejua wamechagua mtambooo
 
Republicans wwlimchagua kwa hili
MAGA
Naona wanafurahia sana labda wataondokana na kulala barabarani
Ila ana mikakati mikubwa na ata save hela nyingi sana

Acha sisi tuendelee kupiga miayo tu
 
Back
Top Bottom