Trump apewe nuclear codes

Trump apewe nuclear codes

Sasa huo u hater uko wapi ? Yaani kupishana mawazo imekuwa tabu ? Kwa hiyo kuandika hicho kingereza umeona unanikomoa sio ? Hivi sio mimi niliyekuwa nafurahia mahusiano yenu na kuwatikia kila la kheri kadri niwakutapo ? Yaani ni hate nini kwa mfano ,ni kipi cha ajabu ulicho kuja nacho kwenye hizo makala ? Au unafikiria hazipatikani kwingine kwamba kila mtu anategemea The bold wa jf ndio alete ?

Kiburi hakijengi jitahidi kuwa muungwana ,ni hayo tu

Nani anataka kuwa invited kwenye ma group ya Whatsapp ? Im too old for that crap Sir
Mkuu potezea bwana, haya mambo yakuzogomana humu sio, mnaishusha hadhi jf na kuna watu wanapumua wakiona mnapigana vigimbi nyie kwanyie, mkuu potezea, tumuepuke sheitwaaaani
 
ok,nilikuwa naipita thread yako ya kipepeo,leo nikaona niingie nikacheki first post pale,kumbe umegeuza njia ya kujipatia kipato,
sio mbaya nawe wajitafutia,

anyway mimi binafsi sisomagi story zako kwani kwangu hizo infor unazoweka sio kitu kigeni na siwezi poteza mda kurudia kusoma kitu ambacho nina taarifa nacho.
Time is money,
ila hongera kwa kubuni njia ya kujipatia kipato mkuu
Mkuu Elungata tusiaibushane huju, potezeeeni haya mambo yakugombana sio, mpisheni sheitwani apite
 
Mkuu potezea bwana, haya mambo yakuzogomana humu sio, mnaishusha hadhi jf na kuna watu wanapumua wakiona mnapigana vigimbi nyie kwanyie, mkuu potezea, tumuepuke sheitwaaaani
Mkuu ni swala la kuelimishana tu ,niki log off Jf haya yanabaki hapa
 
juzi karibia siku nzima nilikuwa nimekaa mbele ya televisheni kushuhidia hatua kwa hatua tukio la kihistoria la kuapishwa kwa Rais wa 45 wa Marekani ambaye anakuwa ndiye Rais wa kwanza wa nchi ambaye hana historia ya kuwa mwanasiasa hata kuwa "mwenyekiti wa mtaa" au kutumikia jeshi la Marekani.

Baada ya Rais Donald John Trump kumaliza kutamka maneno 35 ya kiapo cha kushika ofisi ya Urais maneno ambayo yanaishia na sentensi inayosema "... so help me God!" Karibia watu laki tisa waliokusanyika Capitol Hill kushuhudia tukio hili la kihistoria walilipuka kwa shangwe na vifijo kuwa sasa ni rasmi Trump amekuwa Rais.

Lakini binafsi yangu, mara baada ya Trump kumaliza kutamka maneno hayo ya kiapo, wazo moja tu likanipitia kichwani mwangu; "kwahiyo now Trump has the nuclear codes"!!

Katika kipindi chote cha kampeni watu kadhaa wazito akiwemo mama Clinton na hata Rais Obama wamekuwa wakikaririwa wakisema kuwa "Trump hana utashi, busara wala utulivu wa ndani wa kumfanya aaminiwe kupewa 'nuclear codes'".
Maneno hayo yalikuwa yakirudiwa mara kwa mara kiasi kwamba yakawa kama wimbo kwamba "Trump sio mtu wa kuaminika na kuuweka ulimwengu wote rehani kwa kumkabidhi nuclear codes"

Sasa swali la kujiuliza, je hofu hii yote ni kwasababu gani?? Na je, baada ya kuapa ameshapewa hizo 'codes' au bado?? Na je hizo 'codes' ni kitu gani haswa??

Ni kwamba, wakati ambapo jana watu wote akili yao ilikuwa ikisubiria tukio kubwa la kuapishwa kwa Trump na labda wale wenye kupenda kufuatilia habari walifurahia kuangalia jinsi Familia ya Trump ilivyowasili Washington, walivyohudhuria ibada kanisani pale DC, na baadae kujumuika na familia ya Obama kupata kifungua kinywa Whitehouse lakini watu wengi hawafahamu moja ya tukio muhimu zaidi lililofanyika jana ambalo hili haliwezi kurushwa CNN, BBC, Fox au chombo chochote kile cha habari ingawa naamini walikuwa wanajua.

Mnamo majira ya saa tatu asubuhi ndani ya ikulu ya Marekani kilifanyika kikao maalumu amabacho kilihudhuriwa na Rais Barack Obama, Rais Mteule Donald Trump, Makamu wa Rais Joe Biden na Makamu wa Rais Mteule Mike Pence na kikao hiki kilisimamiwa na kamandi maalumu ya jeshi la marekani inayoitwa Strategic Command ambao ndio wanaosimamia sehemu zote za siri zenye kuhifadhi silaha za Nuclear (Strategic Nuclear Arsenal). Pia kikao hiki kilikuwa na muwakilishi wa ofisi ya jeshi ndani ya White House (Whitehouse Military Office).

Kikao hiki kilihusu makabidhiano ya "nuclear codes" kutoka kwa Obama kwenda kwa Trump.

Miaka ya nyuma Rais mpya alikuwa anapewa hizi codes Mara baada ya kuapishwa lakini mwaka 1973 utaratibu huu ukabadilishwa ambapo kabla ya Rais mpya kula kiapo kinafanyika kikao cha siri ambacho Rais Mteule anakabidhiwa nuclear codes.

Swali, je hizi codes ni kitu gani?? Ni kama namba ya mpesa au tigo pesa au atm ambayo unakuwa umeikariri kichwani??

Jibu ni kwamba, hizi tunazozisikia zikizungumzwa kila siku "nuclear codes" ni msululu wa vifaa maalumu vya kijeshi vinavyomuwezesha Rais wa Marekani kutumia uwezo wake kama Amiri Jeshi mkuu kufanya shambulio la kinyuklia pale anapoona inafaa kufanya hivyo.
Na ukisikia wanaongelea "nuclear codes" ni kwamba wanaongelea mkoba maalumu ambao mda wote unakuwa umebebwa na Mwanajeshi wa Marine sehemu yoyote ile ambayo Rais wa Marekani anakuwepo.

Sehemu yoyote ile ambako Rais wa marekani anakuwepo ndani ya nchi yake au nje ya nchi.. Mtaani au whitehouse, yaani popote pale alipo..
Watu wengi huwa wanaelekeza akili yao kushangaa wale 'secret service', but next time jaribu kupepesa macho (hata kama unaangalia kwenye TV) utaona kuna Mwanajeshi amevaa sare za Marine (au mara chache sana anavaa suti) amebeba mkoba mweusi uliotuna. Huu mkoba wenyewe wanauita "The Football" na ndani yake ndimo kuna "nuclear codes" na nyenzo nyingine muhimu za kumuwezesha Rais kufanya shambulio la nyuklia.

Ndani ya huu mkoba unaoitwa "The Football" au kama unavyojulikama kwa jina rasmi la kiofisi "The Presidential Emergency Satchel" kuna vifuatavyo;

- kuna kifaa kinafanana kama na laptop
- kuna simu ya kijeshi ya satelaiti
- kijitabu kama kipeperushi chenye maelezo ya namna ya kutumia vifaa vyote ndani ya The Football
- kuna kijitabu chenye maelezo ya hatua za kijeshi na sehemu za kuzilenga kwa mashambulio (retaliatory options)
- kuna kadi ya pembe nne kama kadi ya benki yenye namba za siri. Hii kadi maarufu inaitwa "The Biscuit".

Sasa ikitokea Rais anataka kutumia nyuklia kushambulia mahali fulani.. Huu mkoba unafunguliwa kisha kitufe maalumu kinabonyezwa ambacho inatuma taarifa maalumu inayoitwa "watch alert" kwenda kwa kamati ya Majemedari wa Vikosi vya majeshi ya Marekani (Joint Chiefs of Staff). Na wao wanamshauri Rais namna bora ya kutekeleza shambulio hilo.

Hapa niseme kwamba huu ushauri wa hawa Joint Chief of Staff ni protokali tu kwani Marekani inao mpango maalumu wa kijeshi unaoonyesha namna ya kufanya shambulizi lolote la nyuklia kutegemea na lengo lolote ambalo Rais atakuwa nalo. Mpango huu unaitwa OPLAN 8010 (zamani ilikuwa inaitwa Single Integrated Operational Plan) ndio hii ipo kwenye kile kijitabu kimoja wapo nilichoeleza hapo juu kuwa kipo ndani ya The Football.

Baada ya hapo The Football inatuma signal kwenda National Military Command Center ambayo itampa Rais 'access' ya mizinga yote ya nyuklia ipatayo 4,500.

Baada ya hapo kwa kutumia kile kifaa kama laptop ndani ya The Football atachagua 'location' anayotaka kuishambulia na kisha ataingiza 'codes' zilizopo kwenye kile kikadi kinachoitwa The Biscuit. Na baada ya hapo, booooommb.!! Shambulio linakuwa limetekelezwa.

Nchi nyingine pia zenye nguvu kubwa za kijeshi kama Urusi na China pia wameiga mfumo huu.

Hiki nilichoeleza ndizo "nuclear codes" ambazo walikuwa wanapiga kelele Trump asipewe. Lakini mpaka hivi tunavyoogea tayari anazo na mwanajeshi wa Marine anambebea huo mkoba kila Trump alipo, kwa sababu yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu kwa sasa.

Mizinga hii 4,500 ya nyuklia ina uwezo wa kuisambaratisha dunia yote kama ikirushwa sehemu tofauti tofauti za dunia, na ndio maana mara baada ya Trump kumaliza kile kiapo cha Urais cha maneno yale 35 pekee.. Na kumaliza kwa ile sentensi maarufu ya kwenye kiapo "…. so help me God!", Trump amekuwa ndiye binadamu mwenye nguvu zaidi kwa sasa juu ya huu uso wa dunia.

bc89b6c51b006e22b68391093ef270fc.jpg
like Hollywood movie, calculated lie
 
Ila tukiwa wakweli bila kuengemea upande wowote jamaa The bold anafanya kazi kubwa sana tena sana

Fikiria unajipinda kumtunza demu then anakuja kidume kinakuja kumkunja demu wako sijui unajiskiaje

Kama mnaona kazi ku translate ni kazi ndogo
muwe mna translate basi na nyie
The bold ndio kakopi kwa mtoa mada
 
Mkuu wewe inaezekana ulikuwa na nia njema tu ya kumchangia The bold ili anapoandaa makala zake awe anapoza hata kwa sharubati lakini kitendo cha kuanzisha group na wengine kulipia ili wapate makala mie naona kinanyima fursa ya wale wasio na fedha/shekeli kupata hizo makala.

Na huu ndiyo ugomvi unaoonekana humu, wengine wanabeza kwamba wanazijua hizi makala lakini kwanini nao hawaziweki humu ili watu wazisome pia? Lakini hawa wanaona tu kuwa wamekosa hiyo fursa ya kuendelea kusoma makala ambazo sasa zinalipiwa huko kwa group.

Mie sio muumini wa fedha lakini ni MUUMINI WA UTU NA HAKI na nafahamu kuwa fedha sio kila kitu katika maisha ya binadamu.

Ushauri wako wa kuchangia fedha umeleta tafrani humu sasa kwani kama shida ya The bold ni pesa mie nipo tayari kumchangia ili aendelee kutuletea makala humu.
Kupitia makala zake tunajifunza na tunaburudika.
Nimekuelewa mkuu lakini ile thread ya humu si kama imefutwa no lipo na linaendelea na ratiba yake kama kawaida tofauti ni kwamba kule itakuwa (hajaanza kutuma) 4times/week sasa labda kiherehere changu ndo kimeleta yote haya hesabu ni kiasi gani tunapoteza kwa vitu vya kipuuzi? mm ni mpenzi wa kwenda bar lakini nimepiga hesabu kule hadi nipate stimu natumia 20000 per day kwa week naenda mara hata 3 siku za kawaida weekend ndo bili inaongezeka..
Huoni kuwa nasave chochote nikikaa home najisomea mwezi mzima au napiga vyombo mara 2 kwa wiki tena kwa spdi ndoogoo maana nipo bize na simu kwa mtonyo wa buku 5 tu?
Please mtumie jamaa namba akuunge ili twende pamoja
 
Kwanza ujue inatakiwa tuwe na uhakika kuwa dogo kaitoa kwa the bold, je kama yeye alikuwa second hand!!? Kama naye alifowardiwa watsapp.
Yaan jambo dogo limekuwa kubwa kweli kweli
Ningemuona The bold ana hekima kama angemuuliza mleta mada ''Mkuu mbona huja ni acknowledge kama mtunzi wa story?'' au angesema chochote kuonesha mwandishi wa story ni yeye na sii kufura povu kama alivyofanya.
 
Ukitaka kujua kama ni big deal au sio big deal, siku ukiwa chuo hasa chuo kikuu either degree au master, copy reseach ya mtu bila kucredit uliyemcopy, hapo ndo utajua kama ku copy ni big deal au small deal. Tena atakayekutoa machozi sio aliyeandika hicho ulichocopy bali aliyegundua kuwa umecopy somewhere tena kwa mtu ambaye hata yeye hajawahi kumuona.
Nikuulize swali yeye the bold alisema anandika hiyo makala kwa msaada wa vyanzo gani!!?

Mi nisha kuwepo chuo kikuu, na hata kazi ya the bold kwa kichuo chuo tungesema ame pragialize kwa kuwa lazima kafanya literature review, na hakuna sehem anayo acknowledge.

Mimi sina shda na yoyote na the bold wala mwandishi, kwani kilicho tokea ni kosa kweli ila ni kosa la kawaida hasa kwa jf. Na naona ililetwa kwa lengo la kupeana elim.

Whether i can write it or not, sioni haja ya kumshambulia jamaa utafikiri the bold ali alizitoa info sayari ya Mars. Huyo dogo mwenyewe hakuleta kwa lengo baya wala nn, ila nikashangaa anaanza tu kushambuliwa.

Na sina wivu wowote pia sina unafiki natoa maoni yangu kwa nilivo iona situation.
 
Ningemuona The bold ana hekima kama angemuuliza mleta mada ''Mkuu mbona huja ni acknowledge kama mtunzi wa story?'' au angesema chochote kuonesha mwandishi wa story ni yeye na sii kufura povu kama alivyofanya.
Yes
Aliwaka sana na ile haikuwa poa, pia the bold ni mtu mzuri tu, ila ameshindwa ku handle criticism. Jambo ambalo mi sjaona kama ni poa.
 
Yes
Aliwaka sana na ile haikuwa poa, pia the bold ni mtu mzuri tu, ila ameshindwa ku handle criticism. Jambo ambalo mi sjaona kama ni poa.
Ukisema hivyo atakwambia wewe ni hater, yaani huyu jamaa hatofautiani sana na Mtukufu wetu. Inaonekana hapendi kukosolewa ila ni kusifiwa tu.

Kuna maendeleo ya mtu yanakuja bila kukosolewa? watu wamem-criticize kwa maana amereact kwa jazba sana kwenye issue ndogo kama hii......BTW naamini atakuwa kajifunza kitu.
 
Hahahahahaha!! Ndio uone maajabu ya walimwengu mpwa..


Sitasema kitu kingine chochote kuhusu hili, Mungu awe hakimu katika hili..

Wanaonifahamu wanajua unyenyekevu wangu,
Wanaonifahamu wanajua ni kiasi gani mimi mtu wa kujishusha siku zote,
Wanaonifahamu wanajua ni kiasi gani naheshimu kila mtu,

Wote mlionitukana kwenye huu uzi msiache kutukana, endeleeni kutukana..
Wote mliokejeli, zidisheni bidii..
Wote mliobeza, ongezeni ukali wa maneno zaidi..
Na wote wenye chuki na mmetumia hii kama dirisha la kujidhihirisha, nashukuru kwa maana nimewatambua..

Nawaahidi kitu kimoja, na mbingu na malaika wawe mashahidi katika hili.! Nawaahidi kuwa ipo siku inakuja mtasikia aibu kwa haya matusi, bezo na kejeli mlizoandika humu.. Ipo siku!

Najua kilichomo ndani yangu and nobody can take that away.. Siku zote na amini kuwa dhamira ya kweli inashinda mara zote! Na ndivyo nilivyoshinda vita kama hii 2014 (tena kwenye vyombo vya sheria) na ndivyo nikivyoshinda mwaka jana dhidi ya gazeti la kisiwa.. Hata siku moja, Mungu hamtupi mtu mwenye dhamira safi na ya kweli!

Naacha Mungu awe hakimu kati yangu mimi na nyinyi.. Ipo siku mtasikia aibu kwa matusi na kejeli mlizoandika humu!!

Sina chuki na wale wanaotukana humu, na nimewasamehe bure kabisa.!

Mbarikiwe..


The Bold.
Mkuu ingekuwa na ukimalizia na wale niliowakwaza wanisamehe kwani nami ni binadamu ingekuwa poa sana kamanda
 
Ukisema hivyo atakwambia wewe ni hater, yaani huyu jamaa hatofautiani sana na Mtukufu wetu. Inaonekana hapendi kukosolewa ila ni kusifiwa tu.

Kuna maendeleo ya mtu yanakuja bila kukosolewa? watu wamem-criticize kwa maana amereact kwa jazba sana kwenye issue ndogo kama hii......BTW naamini atakuwa kajifunza kitu.

Hapana mkuu naamini haja jifunza kitu na ata zidisha kuwa hivo alivo.
Yeye anaona kila alicho fanya ni sahihi, pia watu wanao mzunguka wana mjaza upepo
Nadhani hakuwahi kupingwa ana hisi tunao pinga reaction yake tuna wivu.
Bado naona the bold hajazoea kubishiwa, naona washabiki wake pia wanaharibu kiania fulani hapa.
 
Hapana mkuu naamini haja jifunza kitu na ata zidisha kuwa hivo alivo.
Yeye anaona kila alicho fanya ni sahihi, pia watu wanao mzunguka wana mjaza upepo
Nadhani hakuwahi kupingwa ana hisi tunao pinga reaction yake tuna wivu.
Bado naona the bold hajazoea kubishiwa, naona washabiki wake pia wanaharibu kiania fulani hapa.
Dah! jamaa kaonesha reaction kubwa kuliko stimuli, mbaya zaidi ni chain ya negative reactions.

Kwenye mind yake keshakariri kila anayempinga ni hater, mtu kama huyo unamwaacha tu.
 
Hapana mkuu naamini haja jifunza kitu na ata zidisha kuwa hivo alivo.
Yeye anaona kila alicho fanya ni sahihi, pia watu wanao mzunguka wana mjaza upepo
Nadhani hakuwahi kupingwa ana hisi tunao pinga reaction yake tuna wivu.
Bado naona the bold hajazoea kubishiwa, naona washabiki wake pia wanaharibu kiania fulani hapa.

Bu'yaka aliwahi kumkosoa kuhusu hayo mambo.

Jamaa [Bu'yaka] alikuwa na hoja ya msingi kabisa ila alichokosea ni namna ya kuiwasilisha.

Binafsi sikuona kama aliiwasilisha vyema. Lakini hoja yake ilikuwa na merit.

Ingia hapo uone: Top Secret: Nyaraka Namba 12333 kutoka Whitehouse
 
Back
Top Bottom