Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Utawala mpya wa Rais wa Marekani Donald Trump umesitisha na kuzuia misaada ya kimarekani kwa nchi za kigeni.
Marco Rubio ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameripotiwa kutuma barua kwenye balozi zote duniani kusitisha miradi ya maendeleo ambayo inafadhiliwa na Marekani ndani ya siku 90.
Barua ya Marco Rubio imedokeza kuwa ndani ya siku hizo 90, uongozi mpya wa Trump utafanya uchambuzi kuhusu namna ambavyo Marekani itakuwa inatoa misaada yake kwa nchi nyingine ambapo Rais Trump alidokeza kuwa misaada yote inayotolewa nchi za nje lazima ijibu maswali matatu rahisi:
Kwa hiyo ndni ya siku 90 iwapo kuna mradi wowote kutoka Marekani ambao hautajibu hayo maswali matatu muhimu kuna uwezekano mkubwa mradi huo ukafutwa kabisa
Uamuzi wa Trump utakavyoiathiri Tanzania
Kwa nchi za Kiafrika na dunia ya 3 kwa ujumla, uamuzi wa Trump ni pigo kubwa kwa taasisi na miradi ya maendeleo inayotegemea msaada kutoka Marekani.
Ukweli mchungu ni kwamba hata baada ya mapitio hayo, hakuna uhakika kuwa mambo yatarejea kama kawaida.
Hatua hiyo imeshaanza kuleta athari na kusababisha wasiwasi miongoni mwa wafanyakazi wa miradi inayofadhiliwa na Marekani, wengi wao wakiwa hawana uhakika wa ajira zao.
Gazeti la Mwananchi lilipata wasaa wa kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi ambao baadhi ya miradi yao inafadhiliwa na Marekani wakieleza wasiwasi yao juu ya uamuzi huo wa Rais Trump.
Esther Jackson (sio jina lake halisi), meneja wa mradi wa elimu ya afya ya uzazi jijini Dar es Salaam, amesema kuwa tangazo hilo limeathiri miradi yao moja kwa moja.
"Baada ya maagizo yale, tulitangaziwa ofisini kuwa miradi tuliyokuwa tunaitekeleza itasimama kwa muda. Kwa sasa tumeambiwa hatuna haja ya kwenda kazini mpaka pale tutakapofahamishwa vinginevyo," amesema Jackson.
================================================================
Secretary of State Marco Rubio ordered an immediate stop to the flow of almost all U.S. foreign assistance Friday pending a review, according to an internal State Department cable obtained by NBC News.
The directive sent to all consular and diplomatic posts follows President Donald Trump’s executive order Monday pausing new obligations and disbursements of foreign aid pending reviews "for programmatic efficiency and consistency" with U.S. foreign policy, within 90 days of the order.
The memo stipulates that U.S. departments, agencies and entities “shall not provide foreign assistance funded by or through the Department and USAID without the Secretary of State’s authorization or the authorization of his designee."
Source: Financial Times, Mwananchi
Utawala mpya wa Rais wa Marekani Donald Trump umesitisha na kuzuia misaada ya kimarekani kwa nchi za kigeni.
Marco Rubio ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameripotiwa kutuma barua kwenye balozi zote duniani kusitisha miradi ya maendeleo ambayo inafadhiliwa na Marekani ndani ya siku 90.
Barua ya Marco Rubio imedokeza kuwa ndani ya siku hizo 90, uongozi mpya wa Trump utafanya uchambuzi kuhusu namna ambavyo Marekani itakuwa inatoa misaada yake kwa nchi nyingine ambapo Rais Trump alidokeza kuwa misaada yote inayotolewa nchi za nje lazima ijibu maswali matatu rahisi:
- Je, misaada hiyo inachangia kuifanya Marekani kuwa salama?
- Je, inaiimarisha Marekani kama taifa lenye nguvu?
- Je, inachangia ustawi wa kiuchumi wa Marekani?
Kwa hiyo ndni ya siku 90 iwapo kuna mradi wowote kutoka Marekani ambao hautajibu hayo maswali matatu muhimu kuna uwezekano mkubwa mradi huo ukafutwa kabisa
Uamuzi wa Trump utakavyoiathiri Tanzania
Kwa nchi za Kiafrika na dunia ya 3 kwa ujumla, uamuzi wa Trump ni pigo kubwa kwa taasisi na miradi ya maendeleo inayotegemea msaada kutoka Marekani.
Ukweli mchungu ni kwamba hata baada ya mapitio hayo, hakuna uhakika kuwa mambo yatarejea kama kawaida.
Hatua hiyo imeshaanza kuleta athari na kusababisha wasiwasi miongoni mwa wafanyakazi wa miradi inayofadhiliwa na Marekani, wengi wao wakiwa hawana uhakika wa ajira zao.
Gazeti la Mwananchi lilipata wasaa wa kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi ambao baadhi ya miradi yao inafadhiliwa na Marekani wakieleza wasiwasi yao juu ya uamuzi huo wa Rais Trump.
Esther Jackson (sio jina lake halisi), meneja wa mradi wa elimu ya afya ya uzazi jijini Dar es Salaam, amesema kuwa tangazo hilo limeathiri miradi yao moja kwa moja.
"Baada ya maagizo yale, tulitangaziwa ofisini kuwa miradi tuliyokuwa tunaitekeleza itasimama kwa muda. Kwa sasa tumeambiwa hatuna haja ya kwenda kazini mpaka pale tutakapofahamishwa vinginevyo," amesema Jackson.
================================================================
Secretary of State Marco Rubio ordered an immediate stop to the flow of almost all U.S. foreign assistance Friday pending a review, according to an internal State Department cable obtained by NBC News.
The directive sent to all consular and diplomatic posts follows President Donald Trump’s executive order Monday pausing new obligations and disbursements of foreign aid pending reviews "for programmatic efficiency and consistency" with U.S. foreign policy, within 90 days of the order.
The memo stipulates that U.S. departments, agencies and entities “shall not provide foreign assistance funded by or through the Department and USAID without the Secretary of State’s authorization or the authorization of his designee."
Source: Financial Times, Mwananchi