Trump ataja maeneo na kiasi ambayo mafisadi waliyatumia kuiba pesa za Marekani kwa kisingizio cha kusaidia nchi za nje

Shotocan

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2023
Posts
6,650
Reaction score
12,711
Trump ataja maeneo na kiasi ambayo mafisadi wa Marekani waliyalitumia kuiba pesa za Marekani kwa kisingizio cha kusaidia Africa

Msikilikilize kuanzia dakika 1:20 akianza kutema cheche

Your browser is not able to display this video.
 
Mambo Haya yalishasemwa sana. Alianza kufanya mzilankende mmoja kwa kutafuta wafanyakazi hewa, wastaafu hewa, wanufaika hewa nk. Trump ashikilie hapohapo na nchi zetu zipone na mambo ya hovyo yanayoletwa kutoka ulaya. Tazama kwenye kilimo kwa mfano, Mbegu zetu zinakwisha na tunabakiwa na mbegu za kisasa karibia kwa kila zao mambo ya hovyo kabisa haya.
 
Kwenye ile nchi ya kusadikika inayoongozwa na kile chama chakavu, hizi fedha walizitumia kutengeneza kofia, t-shirt, khanga na vipeperushi vyenye rangi ya kijani na njano. Ndio maana Trump kakasirika na huu ujinga wa chama chakavu
 
Kwenye ile nchi ya kusadikika inayoongozwa na kile chama chakavu, hizi fedha walizitumia kutengeneza kofia, t-shirt, khanga na vipeperushi vyenye rangi ya kijani na njano. Ndio maana Trump kakasirika na huu ujinga wa chama chakavu
Hizo pesa za USAID hadi huko Chadema zilifika ujue kwa kisingizio cha kuimarisha demokrasia nk
 
Trump ataja maeneo na kiasi ambayo mafisadi wa Marekani waliyalitumia kuiba pesa za Marekani kwa kisingizio cha kusaidia Africa

Msikilikilize kuanzia dakika 1:20 akianza kutema cheche


Hii audio ni ya kweli? sio AI audio kweli?

Kuna habari kataja hapo ya machoko Lesotho na tohara Msumbiji ni kama feki hivi, nimeishia hapo kusikiliza
 
Hujui chochote kuhusu kilimo,mbegu zetu zinakwisha!?..saro ni mbegu ya nani?.. hakuna mbegu zetu kwenye mahindi?..hujui hata kuwa tuna taasisi ya kutafiti na kuzalisha mbegu!?..hizo mbegu unazodai ekari moja zinatoa gunia 25, mbegu mpya ekari moja gunia 40,zitumike zipi?
 
Trump ataja maeneo na kiasi ambayo mafisadi wa Marekani waliyalitumia kuiba pesa za Marekani kwa kisingizio cha kusaidia Africa

Msikilikilize kuanzia dakika 1:20 akianza kutema cheche

Let's wait and see, the aftermath is what will justify whatever the means and procedures his government is doing.
 
Kwenye ile nchi ya kusadikika inayoongozwa na kile chama chakavu, hizi fedha walizitumia kutengeneza kofia, t-shirt, khanga na vipeperushi vyenye rangi ya kijani na njano. Ndio maana Trump kakasirika na huu ujinga wa chama chakavu
Hakuitaja Tanzania lakini. Endelea kuunga.
 
Mkuu, kwani kuna kosa lolote kufadhili juhudi za kuimarisha demokrasia?
Ndio. Zinachochea uasi. Kitu ambacho Trump amekiita....mambo ya hovyo.

Hata hivyo swali hilo lingemfaa Trump. Kwanini anakata misaada ya kuunga juhudi za kuimarisha Democrasia?
 
Ndio. Zinachochea uasi. Kitu ambacho Trump amekiita....mambo ya hovyo.

Hata hivyo swali hilo lingemfaa Trump. Kwanini anakata misaada ya kuunga juhudi za kuimarisha Democrasia?
Ameeleza kuwa hilo dirisha linatumika kuiba pesa za walipa kodi wa marekani kupitia mafisadi ya marekani

Mfano ilishaelezwa siku nyingi zinatolewa pesa zinazoitwa za kuimarisha demokrasia haziendi cash bali zinatumika kifisadi kununua silaha kampuni za washikaji zao au zao na kuwapa waasi wa nchi husika waangushe serikali zao

Badala ya nchi kuwa ya kidemokrasia inakuwa ya vurugu tupu ikitawaliwa kwa mkono wa chuma hakuna cha demokrasia wala nini

Ndio maana kafuta.Miaka nenda rudi zinatolewa hizo pesa za kuimarisha kinachoitwa demokrasia na hakuna cha maana chochote zilicho achieve hizo hela
 
Kidogo kwa afya bora na kingi kwa kusababisha madhara makubwa kiafya, kipi kitumike hapo?
 
Kwanza pamoja na mapungufu yake, ninashukuru sana uwepo wake.

Anafunguka na kutumwangalia.

It vindicates alot that has been said all along. Wanafadhili uasi.

Juzi pia nimemsikia mmoja wa waandamizi wa USAID akihojiwa na kamati moja ya bunge la marekani.

nIkiri tu, sikuona maswali na majibu yote, ila swali moja aliloulizwa ni

"kwahiyo unataka kusema fedha zilikuwa zikutumwa na kutumiwa na Boko Haram"?

Akajibu, 'Ndio'

nikiunga na ulichosema kwamba zinatumika huko huko kununulia silaha, napata jibu.

ila nilishangaa na kushangazwa kwa kweli.

Wacha tu afute hiyo misaada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…