Tshabalala amemdhalilisha meneja wake, Henry Mzozo

Tshabalala amemdhalilisha meneja wake, Henry Mzozo

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
23,566
Reaction score
24,891
Kitendo cha Tshabalala kuongeza mkataba wa kuitumikia Simba SC bila kumshirikisha meneja wake, Henry Mzozo, hakuna namna nyingine ya kukielezea zaidi ya kusema ni udhalilishaji wa hali ya juu wa mchezaji kwa meneja huyo.

Mzozo katika siku za hivi karibuni amekuwa akizungumza katika vyombo vya habari kwa ujasiri mkubwa kwamba safari hii hakuna chaguo la 'mchezaji wake' kusalia Simba, na kwamba uamuzi walioufikia ni kuondoka kabisa Simba hata kama ikibidi kwenda Gwambina, kwa kile alichoeleza kuwa ilikuwa mchezaji huyo asisaini Simba hata kipindi cha miaka miwili iliyopita ila waliivumilia tu, lakini safari hii hawatasaini kabisa.

Kabla hata masaa 24 hayajapita, taarifa ya maandishi, picha na video ikatolewa katika mitandao rasmi ya kijamii ya klabu ya Simba zikimuonyesha na kumnukuu Tshabalala akikiri kusaini mkataba mpya na klabu hiyo, tena bila ya uwepo wa 'meneja wake' ambaye amekuwa akimpamba mchezaji huyo katika vyombo vya habari

Jambo hilo mimi binafsi nimelitafsiri kama ni dharau na udhalilishaji wa mchezaji kwa meneja wake, na hivyo kuwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakifuatilia sakata hili, kufanya dhihaka na kejeli kwa meneja huyo pamoja na waliokuwa wakimuunga mkono, hasa baadhi ya wachambuzi wa soka la Tanzania

Tshabalala asiishie hapo, amuombe radhi meneja wake, na pia asimsahau moja kwa moja hasa kwa mgao walau kidogo wa dau alilotengewa na Simba
 
Kitendo cha Tshabalala kuongeza mkataba wa kuitumikia Simba SC bila kumshirikisha meneja wake, Henry Mzozo, hakuna namna nyingine ya kukielezea zaidi ya kusema ni udhalilishaji wa hali ya juu wa mchezaji kwa meneja huyo.

Mzozo katika siku za hivi karibuni amekuwa akizungumza katika vyombo vya habari kwa ujasiri mkubwa kwamba safari hii hakuna chaguo la 'mchezaji wake' kusalia Simba, na kwamba uamuzi walioufikia ni kuondoka kabisa Simba hata kama ikibidi kwenda Gwambina, kwa kile alichoeleza kuwa ilikuwa mchezaji huyo asisaini Simba hata kipindi cha miaka miwili iliyopita ila waliivumilia tu, lakini safari hii hawatasaini kabisa.

Kabla hata masaa 24 hayajapita, taarifa ya maandishi, picha na video ikatolewa katika mitandao rasmi ya kijamii ya klabu ya Simba zikimuonyesha na kumnukuu Tshabalala akikiri kusaini mkataba mpya na klabu hiyo, tena bila ya uwepo wa 'meneja wake' ambaye amekuwa akimpamba mchezaji huyo katika vyombo vya habari

Jambo hilo mimi binafsi nimelitafsiri kama ni dharau na udhalilishaji wa mchezaji kwa meneja wake, na hivyo kuwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakifuatilia sakata hili, kufanya dhihaka na kejeli kwa meneja huyo pamoja na waliokuwa wakimuunga mkono, hasa baadhi ya wachambuzi wa soka la Tanzania

Tshabalala asiishie hapo, amuombe radhi meneja wake, na pia asimsahau moja kwa moja hasa kwa mgao walau kidogo wa dau alilotengewa na Simba
AIsee andiko jepesi saana kaka umeandika...nikuulize maswali madogo tu umejuaje kama Kasaini bila kuwepo Manager wake leo?. Isije ikawa umedanganywa na picha zilotumwa mitandaoni ambazo pia haziwaonyeshi watendaji wa simba pia. Pili hivi kwa akili za darasa la nne tu unajua ni nani kasababisha Simba kwa mara ya kwanza tokea kufanya mabadiliko kuamua kukurupuka na kuwasainisha wachezaji Boko na shabalala upesi tena bila mbwembwe tulizozoea za kutoa taarifa mapema? kajibu kwanza hayo maswali kisha uje ufute huu ujinga ulioandika
 
Mohammed Husein Hana uwezo wa kusain karatasi lolote la mkataba bila ya uwepo wa meneja wake. Izo stori zako ni za vijiwe vya kahawa.
Meneja wa mchezaji alizungumza uhalisia wa vilabu vya Simba na Yanga kuwaheshimu wachezaji wa nje kuliko wa ndani, na ni kweli Sakata la Chama Simba walikosa usingizi ili kulifanikisha alafu mzawa unamsainisha mkataba umebaki chini ya miezi miwili.
 
Mohammed Husein Hana uwezo wa kusain karatasi lolote la mkataba bila ya uwepo wa meneja wake. Izo stori zako ni za vijiwe vya kahawa.
Meneja wa mchezaji alizungumza uhalisia wa vilabu vya Simba na Yanga kuwaheshimu wachezaji wa nje kuliko wa ndani, na ni kweli Sakata la Chama Simba walikosa usingizi ili kulifanikisha alafu mzawa unamsainisha mkataba umebaki chini ya miezi miwili.
kama washa sign pre contract ya mamilioni yanga watu kama hawa hawakutaka halafu tena wanaleta kelele simba si ujuha huo?kama mchezaji yanga wamefika dau wewe unakazania kubaki simba unajielewa kweli?

Zimbwe ni mchezaji anayehitaji matusi na mikwara ya meneja redioni ili kupata contract extension kweli na kiwango kizuri namna ile? mbona boko kasaini bila makelele?

soma hii posts ya shafih dauda yaani hiyo mechi ya tarehe 8 vs yanga kama kapombe na zimbwe wakicheza chini ya kiwango hii post ya shafih dauda itawahukumu sana sana tu
DAUDAAAA.JPG
 
kama washa sign pre contract ya mamilioni yanga watu kama hawa hawakutaka halafu tena wanaleta kelele simba si ujuha huo?kama mchezaji yanga wamefika dau wewe unakazania kubaki simba unajielewa kweli?

Zimbwe ni mchezaji anayehitaji matusi na mikwara ya meneja redioni ili kupata contract extension kweli na kiwango kizuri namna ile? mbona boko kasaini bila makelele?

soma hii posts ya shafih dauda yaani hiyo mechi ya tarehe 8 vs yanga kama kapombe na zimbwe wakicheza chini ya kiwango hii post ya shafih dauda itawahukumu sana sana tu
View attachment 1767007
Izo story za vijiwen.
 
Izo story za vijiwen.
za kijiweni wakati huyo shafih dauda ni mojawapo ya attck dogs wa zimbwe junior ? dogo kachukua hela kiugumu sana ki gangsta kama movie la hollywood mbona boko kachukua hela kistaarabu tu bila makelele ya kujua anahitaji sh ngapi?

kama attack dog wake keshasema walisign pre contract yanga na wao hawajakanusha tunawasubiri tarehe 8 kwa hamu tutaona pafomansi yao kama advance waliyopewa itahusika kuhujumu simba na kufungisha siku hiyo ama la
 
Boko Hana shida mkataba wake hauwezi kuzidi mwaka mmoja kwakua ana pancha nyingi. Boko ni mstaafu anaye kula penshen yake pale msimbazi.
 
Boko Hana shida mkataba wake hauwezi kuzidi mwaka mmoja kwakua ana pancha nyingi. Boko ni mstaafu anaye kula penshen yake pale msimbazi.
nakuhakikishia hao vijana wako hiyo advance ya GSM itawatokea puani tunawasubiri kwa hamu wafungishe hiyo tarehe 8 KAMA HAWAJA SIGN WAJITOKEZE HADHARANI KUKANUSHA MANENO YA SHAFFIH DAUDA
Boko pia ni gentleman hawezi chukua rushwa ya gsm kama walivyofanya zimbwe na kapombe
 
Mohammed Husein Hana uwezo wa kusain karatasi lolote la mkataba bila ya uwepo wa meneja wake. Izo stori zako ni za vijiwe vya kahawa.
Meneja wa mchezaji alizungumza uhalisia wa vilabu vya Simba na Yanga kuwaheshimu wachezaji wa nje kuliko wa ndani, na ni kweli Sakata la Chama Simba walikosa usingizi ili kulifanikisha alafu mzawa unamsainisha mkataba umebaki chini ya miezi miwili.
mwambie
 
KAMA YEYE NA KAPOMBE HAWATAKANUSHA KUCHUKUA ADVANCE PAYMENT YA GSM KAMA ILIVYOANDIKWA NA CHAWA WAKE AITWAYE SHAFIH DAUDA TUTAWASUBIRI SIKU YA TAREHE 8 AU MECHI MUHIMU ZA CAF NINA HAKIKA WATAHUJUMU TU SABABU PRE CONTRACT WASHAKULA HELA KAMA HAWAJALA WAKANUSHE
 
Gadiel aanzekupangwa,akiperform vizuri game mbilitatu hivi aendelee ili kumuonyesha Mzozo akuna mchezaji mkubwa kushinda klabu ya Simba.
 
Kama Simba Inge waongezea mikataba mapema aya yote yasingetokea mnatakiwa muwahoji viongozi wenu si kuwalaumu wachezaji. Wachezaji mpira ni maisha yao.
 
Unaajitiwa ili ufukuzwe, yawezekana Tshabalala kaona meneje anamletea mapicha picha kamfukuza kijanja
 
Mohammed Husein Hana uwezo wa kusain karatasi lolote la mkataba bila ya uwepo wa meneja wake. Izo stori zako ni za vijiwe vya kahawa.
Meneja wa mchezaji alizungumza uhalisia wa vilabu vya Simba na Yanga kuwaheshimu wachezaji wa nje kuliko wa ndani, na ni kweli Sakata la Chama Simba walikosa usingizi ili kulifanikisha alafu mzawa unamsainisha mkataba umebaki chini ya miezi miwili.

Kwani hujaona meneja akilalamika kuwa hajashirikisha ila kaona tu taarifa mitandaona kuwa jamaa kasaini
 
Aliyelalamika NI mchezaji?
Kama Simba Inge waongezea mikataba mapema aya yote yasingetokea mnatakiwa muwahoji viongozi wenu si kuwalaumu wachezaji. Wachezaji mpira ni maisha yao.
 
kama washa sign pre contract ya mamilioni yanga watu kama hawa hawakutaka halafu tena wanaleta kelele simba si ujuha huo?kama mchezaji yanga wamefika dau wewe unakazania kubaki simba unajielewa kweli?

Zimbwe ni mchezaji anayehitaji matusi na mikwara ya meneja redioni ili kupata contract extension kweli na kiwango kizuri namna ile? mbona boko kasaini bila makelele?

soma hii posts ya shafih dauda yaani hiyo mechi ya tarehe 8 vs yanga kama kapombe na zimbwe wakicheza chini ya kiwango hii post ya shafih dauda itawahukumu sana sana tu
View attachment 1767007
Dauda ni simba,watu wa mikia awajajua tu km dauda alikua anawashtua na yeye hao wachezaji mwisho wa msimu wangekua wachezaji wa Yanga,mikia mumshukuru sana mkia mwenzenu sio wa kumlaumu kabisa
 
Back
Top Bottom