TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Ni HERI MARA 1000 usumbufu wa TTCL kuliko WIZI wa VODACOM. nilichokuja kugundua ni kwamba TTCL kuna maeneo inasumbua ila kama eneo nilipomimi

YAANI mpaka nikiona mtu anaiponda TTCL naona kama ametumwa na VODACOM hapa jamii forum. ila Muda wa kazi ukipita , yaani kuanzia saa 11 jioni huwa internet inakuwa slow sana. ila kusema kweli mnyonge mnyongeni ila kwa VIFURUSHI vinavyojali kipato cha mtanzania, hapana kwa kweli, TTCL bei rahisi sana , yaani mimi Tsh. 3000 natumia wiki zima, kuna siku jioni nilipoona mtandao uko slow, nikaweka kifurushi cha VODA cha Tsh.1000, yaani hazikupita dakika 25.
 
Sio siri ngoja niende kwenya mada moja kwa moja.

Huu mtandao una matatizo mengi sana kama yafuatayo:

1. Huduma ya T PESA
Aisee huu mtandao kama utatuma hela siku ya Ijumaa usiku ghafla litokee tatizo wallah utakuja kuhudumiwa siku ya Jumatatu.

Hili tatuzo limenipata juzi hapa Ijumaa tarehe 7 yaani nilitamani kulia wallah.

2. Vifurushi
Hawa majamaa ukitaka uende nao sawa kwenye masuala ya MBs nakushauri tafuta kitambulisho cha chuo.

Aisee yaani GB 5 kwa Tsh 5000 mwezi mzima.

3. Vocha
Asikwambie mtu, TTCL hawana vocha aisee. Jana nimeenda pale Makao Makuu niliulizia vocha ya 500 hakuna wanasema zipo za 1,000.

Aisee ukienda kuulizia madukani yaani muuzaji anaweza akashangaa maana hiyo vocha ya TTCL ndiyo kwanza anaisikia kwako.

Kilichonipata jana
Nilijiapiza nikaonane na Afisa Masoko pale Makao Makuu pale Posta ili nimshauri kitu kimoja tu. Yaani nikafika mapokezi nikaonane na bwana Kindamba lakini nikazuiliwa.

Yule mama wa mapokezi aliongea sana mpaka wakati naondoka nimeinamishwa kichwa chini kwa masikitiko. Maana shida yangu nilitaka kuonana na Afisa Masoko au CEO wao.


Nilitaka niwambie kama vocha mtaani ni ngumu basi katika option ya kununua bando mteja achague alipe upitia T PESA au salio la kawaida.
Na wewe mkuu yaani unahatarisha maisha yako kipindi cha corona kwenda kuulizia TTCL makao makuu vocha ya 500,hivi siku hizi bado kuna watu mnakwangua vocha? unakwangua na ukijukuta umekwangua namba ya vocha ,mwishowe unabaki huna vocha.
 
Hakuna nmtandao wa hovyo Tanzania kama Ttcl. Bando langu la 5000 ntawaachia na laini nimeivunja.
 
Kampuni mlioingia nayo mktaba(BWW COMPANY LIMITED)kwa ajili ya kusisimamia freelancer ni wababishaji au mtaji hawana. Walichowafanyia vijana wale wanaosajili laini hakivumiliki, si kwa pesa zile walizowatumia jana usiku.

Kwa mwezi mzima mtu anatumiwa elfu hamsini kwa laini 100 wakati kabla ya hapo hiyo ilikuwa pesa ya fomu kwa kila mteja mpya aliyeweka vocha kuanzia 500 wanakulipa 500 kwa laini 100 una elfu hamsini nje na commission ikilinganisha na mitandao kama Tigo, Voda, Airtel wao wanalipa 1000 au 800 kwa kila mteja mteja na bonus juu na vifaa wanavyotumia vya kusajilia laini za TTCL wengi wamenunua kwa pesa zao mfukoni.

Mbaya zaidi imewalipa kwa MPesa badala TTCL na mkataba wao mpaka mwaka 2021 ndio unaisha na huu mwezi NNE ndio mwezi wao wa kwanza tayari wameonyesha udhaifu kuwa mtaji hawana wanategemea pesa za TTCL zinazoletwa na wale vijana kwa kila mteja mpya wanayemsajili.

Anayehusika awasaidie hawa vijana wapate haki yao
 
TTCL inaongozwa kutoka Chato, no creativity, no professionalism.

Unapelekaje tangazo la biashara TBC tv station ambayo haina watazamaji kabisa?
Kwa namna hiyo unadhani utakuwa?

Kwenye huu ulimwengu wa soko la ushindani, TTCL mnashindana na Nani?
 
Mkuu pole sana kwa yaliyokukuta. Pambana utatoboa. Kinachouma zaidi ni kuchomw na jua, kula kwa shida, maneno ya kukatisha tamaa kutoka kwa wateja n.k. Hapo bado baby wako hajakupiga kizinga na kodi ya nyumba.
 
Back
Top Bottom