TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Niliwakimbia mlikuwa mnaendesha biashara kama mnatusaidia. Vocha linakwanguka vibaya mnapigiwa mnaleta lugha gongana nikatupilia mbali laine yenu ilikuwa 2021 huko.

Nataka kuwajaribu tena kwenye home internet, vipi mmebadilika?
 
Mkuu kama uko DSM na unahitaji line ya TTCL pita maeneo ya chuo cha usafirishaji (NIT).

Jana katika safari zangu nimeziona pale.
Achana na kuwauliza huku hao wacheleweshaji.
Nimeomba huduma ya fiber mlangoni kwako tangu mwezi wa 7 2022 hadi leo January sijaona simu yao.

Eh! Kumbe?
 
Niliwakimbia mlikuwa mnaendesha biashara kama mnatusaidia. Vocha linakwanguka vibaya mnapigiwa mnaleta lugha gongana nikatupilia mbali laine yenu ilikuwa 2021 huko.

Nataka kuwajaribu tena kwenye home internet, vipi mmebadilika?
Karibu sana nyumbani
 
Sina uhakika kama TTCL watajibu.. Ila yangu ni haya:

1. Meneja Masoko wenu TTCL ameshindwa kazi.. Hampo popular. Yaani kuna siku niluamua hadi kupiga simu kuulizia menu ya T-pesa.

2. Kuna kipindi nilienda Jijini Mbeya kikazi.. Kule ukinunua kifurushi cha internet ya TTCL basi ujue umeamua kutoa sadaka.. Hutatumia hata Mb 1. Ile ni extremely slow.

3. Hamna utaratibu wa kuwachombeza wateja.. Wenzenu wana vi sms au call kukbushia jambo
Duh nilitaka nipate line Yao nitumie kwenye net ila basi
 
kastama kea wa kampuni ya HALOTEL 13/2/2023 saa 7:35 usiku wanatuma sms yenye kichwa cha UTAPELI. Maelezo yake sasa "katika msimu huu wa valentine tunakushukuru kwa kutumia huduma zetu. Tunatoa surprise kwa wateja wetu watakao tembelea maduka yetu na kupata huduma. Asante!"

SWEET AFRICA
 
Nina kumbukumbu mbaya sana na huduma za TTCL. Huduma mbovu sijawahi kuona yaani ilibidi nicheke badala ya kusikitika. Okay ilikuwa mwaka mmoja uliopita. Siku hizi wamebadilika? Maana nataka wanieletee home internet.
Now TTCL wamebadilika, mambo ni byuti byuti,

#RudiNyumbaniKumenoga
 
  1. Kwanini vocha zenu zinapatikana dukani kwenu tu na mtaani zinapatikana kwa nadra sana?
  2. Kwani customer care yenu ipo inferior sana ukiwapigia customer care baada ya saa za kazi hawapokei simu, wakipokea wanakuambia tupigie kesho
1. Vocha za kukwangua zinapatikana Tanzania nzima, lakini unaweza pia kununua vocha kupitia TigoPesa, M-Pesa, HaloPesa na AirtelMoney, pia unaweza kununua kupita kwa wakala wa Selcom au kupitia benki.

#RudiNyumbaniKumenoga
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (T-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)

- Maeneo gani? (Tukifahamu maana ulipo, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate msaada toka kwa wakala wetu aliye karibu nawe)

- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?

- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza.

- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.


Zifuatazo ni ofisi zetu za huduma kwa wateja ndani ya jiji la Dar es Salaam.


1. POSTA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Samora, jengo la Extelecom ghorofa la Chini.


2. KARIAKOO
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Makamba/Msimbazi, jengo la Akamba Bus Service.

3. UPANGA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Magole/Maliki, karibu na Diamond Jubilee.


4. MAGOMENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Minaki/Fundiki, karibu na Manispaa ya Kinondoni.


5. KIJITONYAMA
[emoji654][emoji654][emoji654]Kijitonyama Sayansi, barabara ya Ali Hassan Mwinyi/ Rose Garden.


6. OYSTERBAY
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Haile Selassie.


7. UBUNGO
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Ubungo Plaza/ Ghorofa la chini.


8. MBEZI BEACH
[emoji654][emoji654][emoji654]Mbezi Makonde/ Jengo la Shamo Tower.


9. TABATA
[emoji654][emoji654][emoji654]Tabata Bima, barabara ya Segerea karibu na kanisa la Romani Katoliki.


10. CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
[emoji654][emoji654][emoji654]Jirani na tawi la benki ya NBC, jirani na kilipo kituo cha polisi cha UDSM.


11. BARABARA YA PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Mwalimu Nyerere, karibu na Sigara.


12. WAGENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Uwanja wa ndege.


13. PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Quality Centre, ghorofa la chini.


14. KISUTU
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Mchafukoge/Libya jengo la Haad Plaza.


15. TEGETA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Kibo Complex, ghorofa la chini.


16. MWANANYAMALA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Mwananyamala A, barabara ya Mwinjuma yalipo makutano ya Mwananyamala A.


17. KURASINI
[emoji654][emoji654][emoji654]Kurasini Exchange Area, jirani na Chuo cha Diplomasia.


Wasiliana nasi:
[emoji337]022 210 0100
[emoji390] 0738 151 511
[emoji273]www.ttcl.co.tz


#RudiNyumbaniKumenoga
View attachment 1529645


Karibu.

Rudi Nyumbani Kumenoga
Hivi kwa nini ninyi mmekosa ubunifu kiasi hiki aisee?
Mtategemea hadi lini kwamba huo Mkonga wa mawasiliano ndio 80% ya revenue zenu, Why can't come na other creavity mpige hela mbona mnaweza, whats problem?

Staring with...
1. Facilitate internet kwenye mashule yote nchini kwa kuanza muanze na Tech. Sec school, baadae shule nyingine na kuhakikisha kila mwezi wanalipia hiyo huduma kwa shule zilivyo nyingi Bongo mbona kuna hela ya nje nje?

2. Hakikisheni walimu wamegaiwa vishkwambi, good, why cant u come up na bando lao hata la 500 wapate GB hata 1 mbona mtapiga hela sana hadi hvy vishkwambi vipitwe na wakati.

Mna fursa nyingi ila hamzitumii....... shirikianeni na eGA na CoStech mnaweza toboa..

By the way hivi mnajipangaje na Ujio wa Starlink, jitahidi hata muwe agency wa ku supply device zake or else mtakosa kbs kitu cha kfanya na shirika kwa mara nyingine inaenda kufa kwa uzembe wenu!!
 
Hivi kwa nini ninyi mmekosa ubunifu kiasi hiki aisee?
Mtategemea hadi lini kwamba huo Mkonga wa mawasiliano ndio 80% ya revenue zenu, Why can't come na other creavity mpige hela mbona mnaweza, whats problem?

Staring with...
1. Facilitate internet kwenye mashule yote nchini kwa kuanza muanze na Tech. Sec school, baadae shule nyingine na kuhakikisha kila mwezi wanalipia hiyo huduma kwa shule zilivyo nyingi Bongo mbona kuna hela ya nje nje?

2. Hakikisheni walimu wamegaiwa vishkwambi, good, why cant u come up na bando lao hata la 500 wapate GB hata 1 mbona mtapiga hela sana hadi hvy vishkwambi vipitwe na wakati.

Mna fursa nyingi ila hamzitumii....... shirikianeni na eGA na CoStech mnaweza toboa..

By the way hivi mnajipangaje na Ujio wa Starlink, jitahidi hata muwe agency wa ku supply device zake or else mtakosa kbs kitu cha kfanya na shirika kwa mara nyingine inaenda kufa kwa uzembe wenu!!
Mimi nipo MBINGA Mjini mtaa wa UZUNGUNI TOKA vibaka wamekata waya huu sasa mwezi 4 nimetoa ripoti Kwa fundi wenu haji na simu ya mezani KANISANI

Simu za kwanza mpaka mligawia watu wengine nashangaa.Mlinishawishi ninunue Ruta nimenumua situmii.

Nikilipia waya unakatwa fundi harudishi huduma.nimechangia tu nirudishieni japo simu
 
Nini kinashindikana kubalisha Sera inayotuma iliyopita na wakati na kutengeza Sera mpya (policy mpya) ili iendane na wakati tulionao Sasa ttcl bado inajiendesha kihenga Sana wako baadh ya wafanyazi wa ttcl wanajiaona bila wao ttcl haiwezi songa mbele ttcl imefika kufuliwa upya na kiwaweka wazoefu kwenye maswala mauzo ya mitandao ya sim Kama kina ally maswanya aliyemfanyia kazi Zaid miaka 20 halikadhalika tigo Zaid ya miaka 10 uzowefu ungesaidia Sana kuboresha shirika la ttcl ni letu wote watanzania tutaka kuona linafanya vizuri kiwanda hichi Cha mawasiliano nnchini
 
Back
Top Bottom