TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

rudi nyumbani kumenoga..
niliwahi kwenda ofisini kwao maeneo ya kariakoo (zanzibar) kupeleka malalamiko juu ya kupatikana kwa huduma zao.
Niliambiwa ifikapo mwezi oktoba 2018 takribani maeneo yote ya zanzibar yatafikiwa na huduma ya TTCL.
leo ni febuary 2020 hakuna kilichobadilika.
nikiwa mjini natumia TTCL vizuri sana ila nikivuka mji natoa line yao naweka halotel.​
Hatua za kuboresha huduma zetu zinaendelea kufanyika ili kuwapatia wateja wetu huduma iliyobora.
 
Huu mtandao ni utopolo wa hali ya juu.
1.Picha linaanza simu ina bando ila kuperuzi haiwezekani ama usubiri usiku sanaaaa
2.Kupiga simu customer care muda wowote wakipokea katambikie mizumu ya kwenu
3.*148*30# ukachagua INTERNET then ukaenda kwny T-connect plus unakutana na vifurushi vya siku
-Tsh500=300mb
-Tsh1000=750mb
-Tsh2000=2gb
Yani vifurushi vya siku vina gharama kubwa kuliko mitandao mengine yote niliowai kutumia afu bila kusahau kuwa net yao ni pasua kichwa ukitoka mitaa ya posta tu hupati kitu
4.Ukitumia T-Pesa huwe tayari na ela ya akiba mana uwezekano wa muamala kutokukamilika ni mkubwa afu ukiwapigia simu ata wiki nzima hawapokei
5.Makato ya T-Pesa kuenda sambamba na mitandao pendwa mingine huu nao ni uzwauzwa wa kiwango cha PhD.
6.Taarifa za TCRA zinasema wateja kama laki 6 wanatumia huu mtandao maajabu ni kuwa wanashindwa kuudumia wateja laki 6,je wataweza wateja 10M+ km voda na tigo
7.Mtandao ambao ukitoka Dar kwenda mikoani simu yako inageuka kuwa Calculator mana hakuna mtandao tena hapo
8.Mtandao ambao nikiweka jero napata dakika 10 tu usawa wenyewe huu wa magu
9.Mwisho nilikuwa mteja mtiifu wa huu mtandao kipindi unaanza ila nilishatupilia mbali line yao mana ni zaid ya utopolo aseee

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaishi wapi kaka mbona mi ndo natumia na haijawahi kunisumbua?
 
Hili shirika litatia sana aibu mara vocha inagoma kuingia,mara meseji haziendi,ukija kwenye Internet ndio hovyo kabisa mara 3G,mara E na saa nyingine hamna herufi yoyote,
View attachment 1354508
Pole kwa changamoto hiyo,tafadhali tufahamishe unapatikana maeneo gani ili tufuatilie na kutatua.Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
 
Hili shirika litatia sana aibu mara vocha inagoma kuingia,mara meseji haziendi,ukija kwenye Internet ndio hovyo kabisa mara 3G,mara E na saa nyingine hamna herufi yoyote,
View attachment 1354508
Pole kwa changamoto hiyo,tafadhali tufahamishe unapatikana maeneo gani ili tufuatilie na kutatua.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
 
TTCL wa hovyo mwezi uliopita niliunga kifurushi cha mwezi lakini do zenyewe sikutumia vizuri network inakata katikati ya mazungumzo na hapo Nipo city centre sipati picha huko vijijini.
 
TTCL kwenye upatikanaji wa huduma za vocha na bundle na T-Pesa ni shida sana.

Ukienda kwa wakala anakwambia sina hiyo huduma [emoji87][emoji87]

Sasa sababu ni nini?

Je kwa kuwa mna wateja wachache? Kwa hiyo wakala anaona akinunua kuja kuuza zitamdodea zitakuwa hazinunuliki?

Kama ndivyo , Je mnamkakati wowote wa kutumia mkakati wa “market penetration “?

Kuhusu mkakati wa ku “increase market share hali ikoje?

Je mna watu wazuri wa markets strategies?

Mjitahidi vinginevyo hata tuliopo tutaweza kufikiria kuwahama.


Sent using Jamii Forums mobile app
Pole kwa changamoto hiyo,tafadhali tufahamishe unapatikana maeneo gani ili tufuatilie na kutatua.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
 
Hakuna laini yenye unafuu tz , ni kwenda nazo hivyo hazieleweki unahamia halotel utakutana na vimbwanga vya huko .

Mm naipenda ttcl Ila ndo ipo slow hivyo tunabembelezana nilikitoka nje network haikamati .
Voda mb ndo hazikai na ipo fasta ,Tigo vifurushi ni bei ,Airtel sijui nisemaje hawapo vizuri internet kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Pole kwa changamoto hiyo,tafadhali tufahamishe unapatikana maeneo gani ili tufuatilie na kutatua.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
 
Pole kwa changamoto hiyo,tafadhali tufahamishe unapatikana maeneo gani ili tufuatilie na kutatua.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Habari..!
Nina changamoto ya t-pesa yaani nimesahau password (nywila) yangu sasa nimejaribu kupiga makao makuu mara mbili lakini bado maelekezo nayopewa hayasaidi na nakua
siwezi kufungua akaunt yangu naomba unisaidie

Pili, ktk vifurushi vya boom pack bundle mgeongeza muda wa maongezi kwenda mitandao yote maana dakika 50 ni chache kwa mwezi mngeonngeza
 
Kwanin msifunge minala ya mawasiliano nchi nzima?
Mtandao kama halotel walifanikiwa, sisi tunashindwaje?
Tunajua ni gharama kubwa, lakini ndio biashara inataka hivyo
Tunashukuru kwa kutuandikia,Hatua za kuboresha huduma zetu zinaendelea kufanyika ili kuwapatia wateja wetu huduma iliyobora.
 
Kwanin msifunge minala ya mawasiliano nchi nzima?
Mtandao kama halotel walifanikiwa, sisi tunashindwaje?
Tunajua ni gharama kubwa, lakini ndio biashara inataka hivyo
Tunashukuru kwa kutuandikia,Hatua za kuboresha huduma zetu zinaendelea kufanyika ili kuwapatia wateja wetu huduma iliyobora.
 
Tunashukuru walao mmeanza kujibu komenti zetu mlikaa kimya kama vile hamnazo kwa vile mnakula kodi zetu boresheni huduma ss wa Dar tu tunakosa mtandao hao wa pembezoni je? Hakuna haja ya kuuliza unakaa wapi huduma ni mbovu.
Nilitembelea ofisi iliyopo nyerere road mara mbili naambiwa eti cha kujisajilia kwa alama za vidole ni kibovu. Mawakala nao wananiambia nina special namba hawawezi kunisajili. Are u people serious au mmebweteka kwa vile muuze au la mshahara mnapata.Mnajua wasio na ajira wanavyoteseka kweli? Mnajua hizh laina tumetaka kusajili baada ya wito wa Mh turudi nyumbani kumenoga?
Mh tunakuomba hebu pangua safu hapo kwanza ili watu watie akili, wanazunguka kwenye viti tu .Tupo wengine ambao tunajua unachotaka ukituhitaji tuko tayari mkuu.
Nchi hii inataka wenye moyo.
NAWASILISHA
 
Back
Top Bottom