Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu baba, shirika hili limekaa kipigaji.Nyie ni mtandao wa mjini tu, uku vijijini na ukubwa wenu wote mnatumia minara ya TiGo!! Speed ya internet konokono ana speed. Jichunguzeni mnakwama wapi?
Wapi tumekufokea?Msitufokee
Ndugu mteja Deceiver, Kibaha kuna ofisi ya TTCL maeneo ya Mkoani jirani na ilipo shule ya Kibaha Independent Pre & Primary School.1. TTCL mmeanza kua na customer care? Hongereni. Ila wajitahidi kufika kazini na kujibu hoja zetu.
2. Kibaha ni makao makuu ya mkoa lkn TTCL hamna tawi na pia hamatikani. Jee Kyle nyumbani Mahenge si itakua balaa?
Rudi Nyumbani KumenogaHata wangesema,karibu porini au. CHATO hatuji.
Nina laini yenu ila nataka kutupaaMkuu baba, shirika hili limekaa kipigaji.
Nadhani ni kijiwe cha mafisadi ambao Magufuli na sekeseke lake la kutumbua kashindwa kuwabaini hawa kwa sababu ya pazia la gawio!
Ushauri ulioutoa hapa, umekuwa ni zaidi ya ushauri bali ni mwangwi sasa unaovuma tokea kila kona ya nchi hii.
Siyo kwamba raia hawapendi kutumia huduma hii, bali uongozi na wafanyakazi wa shirika hili ndiyo hawapendi raia watumie huduma zao.
Kama faida yao inatokana na kuuza masafa kama nilivyomsikia siku1 Kindamba akieleza, basi sasa kuna haja gani kuendelea na hii biashara sumbufu ya mitandao ya simu kwa huduma za hovyo?
Wameshindwaje kuboresha minara yao, gharama za vifurushi vya data na voice nk nk ili kushindana na soko la mashirika mengine binafsi?
Ina maana hao staff wa Ttcl hawatumii mitandao ya simu zingine wakaona na kujifunza ubora wa huduma za wenzao?
Kwa utitiri huu wa mitandao ya simu nchini, mtu akiona internet haisomi ipo mkusuasua na vifurushi ghali basi muda huo huo hufyatua line hiyo na kuweka line nyngine.
Tuseme na hili nalo hawalijui?
Lakini niseme tu kwamba, ipo siku ukuritimba wao huu utakomeshwa kidhalilishaji ama kufirisika kabisa,kwani mara ngapi tumeona wakipumulia mashine?
Maana sasa wamekosa ubunifu wa kiushindani.
Yuko wapi Mchechu wa Nhc aliyejinasibu kubadilisha shirika kwamba anajenga na kuuza nyumba kwa bei nafuu, ukiangalia kiuhalisia ni za bei ya kutupwa ambapo mtu wa kipato cha chini hawezi kununua, alifurushwa kwenye mkutano wa hadhara!
Sasa na huyu bado kaziba nta za masega masikioni mwake, hapokei maoni ya wadau wala ushauri wowote wa kuboresha kutokana na soko linavyokwenda, ipo siku yake!
Ndugu AtropineTTCL mmeshakua wahuni tu, vifurushi vyenu vya sasa ni vyakinyonyaji.
Ni wivu tu.Hata wangesema,karibu porini au. CHATO hatuji.
Vifurushi vimebadilika kutokana na hali ya sasa ya soko, na siyo vyote ambavyo vimebadilika unaweza kuingia kwenye menu *148*30# kuona vifurushi vingine.Jibu maswali kwa nini mmetoe vifurushi husika? Kama liko nje ya uwezo wako sema acha kuzunguka zunguka!
Yaani amejibu baada ya wiki kadhaa!!!!Pitia vizuri comment utaona
Pole sanaKwakweli hawa zantel na TTCL mimi walinishinda niko zangu voda na airtel bora nilipe pesa zaidi ila nipate huduma ya uhakika, hawa bundle cheap unanunua speed E au hata hutumii kabisa wanakwambia limeisha.
Asantae yani hadi line nilivunja kabisaPole sana