TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (T-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)

- Maeneo gani? (Tukifahamu maana ulipo, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate msaada toka kwa wakala wetu aliye karibu nawe)

- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?

- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza.

- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.


Zifuatazo ni ofisi zetu za huduma kwa wateja ndani ya jiji la Dar es Salaam.


1. POSTA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Samora, jengo la Extelecom ghorofa la Chini.


2. KARIAKOO
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Makamba/Msimbazi, jengo la Akamba Bus Service.

3. UPANGA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Magole/Maliki, karibu na Diamond Jubilee.


4. MAGOMENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Minaki/Fundiki, karibu na Manispaa ya Kinondoni.


5. KIJITONYAMA
[emoji654][emoji654][emoji654]Kijitonyama Sayansi, barabara ya Ali Hassan Mwinyi/ Rose Garden.


6. OYSTERBAY
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Haile Selassie.


7. UBUNGO
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Ubungo Plaza/ Ghorofa la chini.


8. MBEZI BEACH
[emoji654][emoji654][emoji654]Mbezi Makonde/ Jengo la Shamo Tower.


9. TABATA
[emoji654][emoji654][emoji654]Tabata Bima, barabara ya Segerea karibu na kanisa la Romani Katoliki.


10. CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
[emoji654][emoji654][emoji654]Jirani na tawi la benki ya NBC, jirani na kilipo kituo cha polisi cha UDSM.


11. BARABARA YA PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Mwalimu Nyerere, karibu na Sigara.


12. WAGENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Uwanja wa ndege.


13. PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Quality Centre, ghorofa la chini.


14. KISUTU
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Mchafukoge/Libya jengo la Haad Plaza.


15. TEGETA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Kibo Complex, ghorofa la chini.


16. MWANANYAMALA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Mwananyamala A, barabara ya Mwinjuma yalipo makutano ya Mwananyamala A.


17. KURASINI
[emoji654][emoji654][emoji654]Kurasini Exchange Area, jirani na Chuo cha Diplomasia.


Wasiliana nasi:
[emoji337]022 210 0100
[emoji390] 0738 151 511
[emoji273]www.ttcl.co.tz


#RudiNyumbaniKumenoga
View attachment 1529645


Karibu.

Rudi Nyumbani Kumenoga
nahitaji kuvuta ttcl kebo ili kupata huduma za internet katika ofisi yangu napataje hiyo huduma na ni kwa gharama gani
 
nahitaji kuvuta ttcl kebo ili kupata huduma za internet katika ofisi yangu napataje hiyo huduma na ni kwa gharama gani
Habari za mchana
Tuna huduma za aina mbili za cable, Copper na fiber, kuweza kuunganishwa na huduma hizi, inabidi kwanza tujue Ofisi yako ipo mkoa gani? eneo lipi? hii itatusaidia kujua kama hii huduma eneo ulilopo linapatikana, ili tuweze kukupa maelekezo sahihi ya kuweza kupata huduma hizi
 
Habari za mchana
Tuna huduma za aina mbili za cable, Copper na fiber, kuweza kuunganishwa na huduma hizi, inabidi kwanza tujue Ofisi yako ipo mkoa gani? eneo lipi? hii itatusaidia kujua kama hii huduma eneo ulilopo linapatikana, ili tuweze kukupa maelekezo sahihi ya kuweza kupata huduma hizi
nahitaji copper an how much is fiber mi nko mkoani tanga wilaya ya muheza actualy
 
nahitaji copper an how much is fiber mi nko mkoani tanga wilaya ya muheza actualy
Ndugu mteja, Fika duka la TTCL hapo Muheza kwa msaada zaidi kwani utapatiwa surveyor ambae atafika kwako kuangalia kama line yetu imefika au atakupa ushauli mbadala.
 
Ndugu mteja, Fika duka la TTCL hapo Muheza kwa msaada zaidi kwani utapatiwa surveyor ambae atafika kwako kuangalia kama line yetu imefika au atakupa ushauli mbadala.
Naomba kujua namna ya kutoa fedha kutoka kwenye Wakala Wallet (ile inayopokea commission), kwenda Wallet ya kuhudumia wateja.
 
Naomba kujua namna ya kutoa fedha kutoka kwenye Wakala Wallet (ile inayopokea commission), kwenda Wallet ya kuhudumia wateja.
*150*71# OK Kisha namba 7, kisha namba 2, kisha 1 mwisho 3, kiasi namba ya siri
 
Twenzetu kwa Mkapa, tukashuhudie mechi Simba vs Yanga.
Pata tiketi yako mapema kupitia T-PESA
#SalamanaNafuu
#RudiNyumbaniKumenoga
183651904_10159586821212884_275917029175544956_n.jpg
 
Nasikitika sana kuona TTCL mpo nyuma ya wakati sana.


Watanzania wanashindwa kupokea hela kupitia Paypal na Skrill kwa muda mrefu sasa huku majirani zetu SafaricomKenya wakitoa huduma hiyo, na hii inawafanya watu watumie line za simu za Kenya na kufaidisha nchi nyingine. Je hamuoni kwamba hiyo kwenu ni fursa ya kuingiza kipato huku mkiinua uchumi wa nchi na wananchi?
 
Nasikitika sana kuona TTCL mpo nyuma ya wakati sana.


Watanzania wanashindwa kupokea hela kupitia Payapla na Skrill kwa muda mrefu sasa huku majirani zetu SafaricomKenya wakitoa huduma hiyo, na hii inawafanya watu watumie line za simu za Kenya na kufaidisha nchi nyingine. Je hamuoni kwamba hiyo kwenu ni fursa ya kuingiza kipato huku mkiinua uchumi wa nchi na wananchi?
Wamekalia kuuza MB ghali wao ndio wanaona ndio chanzo rahisi cha mapato
 
Twenzetu kwa Mkapa, tukashuhudie mechi Simba vs Yanga.
Pata tiketi yako mapema kupitia T-PESA
#SalamanaNafuu
#RudiNyumbaniKumenogaView attachment 1777203
Hivi nyie mko serious kweli? Mnaulizwa na kupewa maoni hata kujitutumua kujibu tu mmenyamaza. Mtaweza kweli ushindani na akina Tigo na Voda na wengine?
Pathetic kabisa. Utakuta hii account ni ya kaji sister do flani Kako hapo kupitia undugunization hakajui A wala B. Shwaini kabisa. you guys forget about taking over the market if you continue with this mentality.
 
Sawa mlituhimiza tununue, tiketi tukanunua!
Sasa game ndio hivyo tena imeyeyuka! Hela zetu mnaturudishia ama na zenyewe zimeyeyuka? Tunaomba jibu tafadhali, msikalie kimya hapa!
mkuu mbona tena umeni quote mimi?
 
Back
Top Bottom