Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa upande wangu cable ya fiber imepita na kugusa juu ya bati la nyumba yangu. Lakini nina zaidi ya mwaka mmoja toka nimeomba sijapata huduma.Inategemea na ulipo, isije ikawa upo km 5 toka ilipopita ikawa ni gharama sana kukufikia. Sisi tuliopo dodoma tunaenjoy tu
Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,Habari za muda huu Wanajamvi,
Hii Kampuni ya TTCL ni sikio la kufa na wala halisikii dawa tena, haifanyi vizuri kwenye mawasiliano ya simu kawaida wala kwenye Internet. Mimi nipo Dar es Salaam na nimeomba huduma ya kufungiwa internet nyumbani (fiber) na sasa yapata miezi sita ila sijafungiwa wala hakuna kitu cha maana kinachoeleweka kutoka kwao.
Ukihitaji Internet wanasema inabidi uombe kupitia website yao na ukifanya hivyo kwa kweli ni kwa haraka tu maombi yako yanapokelewa na kuambiwa yanafanyiwa kazi. Unataarifiwa mara moja kwa ujumbe mfupi (sms) na hapo hapo kwenye website yaani unaweza kusema kweli hawa jamaa ni top-notch na nitapata huduma fasta kabisa.
Ila hapo sasa ndio mchezo unapoanza, utazungushwa hadi ujute mwenyewe. Nimepiga simu zaidi ya mara 5 kwenye namba yao ya huduma kwa wateja wanapokea na jibu lao mara zote linakuwa "Ni kweli umeomba fiber, ombi lako tunaliona na tunalifanyia kazi. Mafundi wetu wa eneo lako watakupigia simu ili waje kukuunganishia". Baada ya hapo nimekuwa nikuliza kwamba hao mafundi watakuja lini atleast mnipe muda kabisa nijue au nifanye taratibu nyingine, hapo utajibiwa "Tafadhali kuwa mvumilivu, mafundi wetu watakutafuta"
Hata hivyo, baadhi ya watu wanasema TTCL hawaji kufunga internet hadi wapate shinikizo kutoka kwa Wakubwa zao. Yaani utafungiwa Internet ukiwa unawajua hao wakubwa ambapo hili ni jambo la ajabu kabisa kwa Taasisi ya Serikali kama ile inayoendeshwa kwa kodi za Wananchi.
TTCL kwa sasa sitaki tena huduma yenu hii, nitafunga internet ya watu wengine na kwa mtindo huu hamtakuja kuwa shirika la maana na hata nashangaa lile gawio mnatoa kwa Serikali huwa mnatoa wapi. Hii Kampuni inakufa hata Wakurugenzi wabadilishe kwa namna gani.
Pia soma;
1. Kuchelewa kupatikana kwa huduma ya internet ( fiber) TTCL
2. Huduma ya TTCL ya kutoa Internet nyumbani ni mbovu sana
Hivi si anatakiwa aje mpimaji ili kuona miundo mbinu imekaaje then ndio wafanye maamuzi na wakujulishe juu ya maamuzi yao? Sasa hata mpimaji haji hadi miaka inapita watajuaje juu ya miundo mbinu ya eneo lako? Na walalamikaji wengine wanadai nguzo zipo mbele ya nyumba zao na baadhi ya majirani wanapatiwa huduma. Unasemaje juu ya hilo?Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,
Unakuta mtu yupo madongo kuinama A miundombinu ipo Madongo kuinama C na ili kumfikia inahitaji km kama 6 za waya na mteja ni mmoja, sasa kweli Shirika litaweza kumfikishia kila mtu ilhali bado na mhusika unaweza kuta yupo peke yake
Ndio maana wanasogeza taratibu ili iwafikie kwa ujumla
Hii huduma inaombwa online kwa website yao. Mfano mimi awali ya yote niliwaambia sehemu nilipo na wakasema wapo wamefika na pia wanasema ukiona mtaa wako haupo wakati wa kujaza kwenye website basi hawajafika. Lakini nimejaza na hadi nyumba number niliikuta ile leo ni karibia mwaka hawajaja.Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,
Unakuta mtu yupo madongo kuinama A miundombinu ipo Madongo kuinama C na ili kumfikia inahitaji km kama 6 za waya na mteja ni mmoja, sasa kweli Shirika litaweza kumfikishia kila mtu ilhali bado na mhusika unaweza kuta yupo peke yake
Ndio maana wanasogeza taratibu ili iwafikie kwa ujumla
Mkuu hao penyeza rupia ndio maana rushwa haishi kwa sababu kama hizi. Hizo taasisi za umma nao waanze kulipwa mishahara kutokana na faida wanayozalishaNdugu zao na DAWASA, wavivu sana wa kufikiri. Ni karibia mwaka sasa huduma ya maji hatujapata tangu tufanye maombi ya kuunganishiwa. Hovyo kabisa.
Inasikitisha sanaBaada ya hapo nikaja kuambiwa kuwa eneo langu kifaa cha kuunganishia fiber kimejaa hivyo engineer wao yupo kwenye process ya kutengeneza kingine.
Hiyo ilikuwa ni Septemba mwaka jana.
Mpaka leo hicho kifaa bado engineer anakitengeneza.
Nikaona bora nichukue Router ya Airtel ambayo mpaka sasa naweza kusema ndio option bora kwasababu inakupa extra benefit ya kuweza kuitumia popote lakini advantage nyingine ni kuwa na uhakika wa kupata huduma hata pale umeme unapokuwa umekatika kwasababu ina battery yenye reserve ya ku store charge kwa masaa zaidi ya 8.
you meant faida? sure.Hakuna shirika la umaa linalotoa huduma inavyostahiki.
Serikali inajisumbuwa na kutia chooni pesa za walipa kodi kuendelea kuyalea haya mashirika ya umma, hayana faidia yoyote.
Mhandisi Peter UlangaMkurugenz mkuu wa TTCL Customer Care yupo humu
Hilo ni tatizo, pole sanaKwa upande wangu cable ya fiber imepita na kugusa juu ya bati la nyumba yangu. Lakini nina zaidi ya mwaka mmoja toka nimeomba sijapata huduma.