KERO TTCL ni sikio la kufa! Haiwezekani kwa zaidi ya miezi sita nimeomba huduma ya fiber nyumbani wananizungusha tu

KERO TTCL ni sikio la kufa! Haiwezekani kwa zaidi ya miezi sita nimeomba huduma ya fiber nyumbani wananizungusha tu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Uaomba fiber mtaani kwako imepita? TTCL wamewaaminisha watanzania popote unapata finer lakini kiuhalisia kuna maeneo hayana miundombinu ya fiber, so inabidi wakuungie mtu mmoja na hapo ndio ugumu unaanzia.
 
Kama huduma ya fiber haijapita mtaani uungwana ni kumjulisha muombaji ili musisumbuane.
 
Sina hamu na hawa jamaa TTCL, Mimi nilitoa gharama zote za nguzo kama 4 hivi na hapo nikampa kitu tech wao na huko ofisini wakanila karibia million yote nifanyiwe haraka, nikaja kupata mwisho wa siku sasa changamoto za huduma zikaanza haipiti wiki Net down nianze kuwapigia na hapo pesa kidogo lazima umpe atakwambia shida tumeitatua kuna sehemu wire basi muhimu kila wiki kuna issue utasema wanafanya kusudi. Nikaamua kuachana nao na kusahau gharama nilizoingia na toka wakati huo sitaki hata kuwasikia.
 
Inategemea na ulipo, isije ikawa upo km 5 toka ilipopita ikawa ni gharama sana kukufikia. Sisi tuliopo dodoma tunaenjoy tu
Kwa upande wangu cable ya fiber imepita na kugusa juu ya bati la nyumba yangu. Lakini nina zaidi ya mwaka mmoja toka nimeomba sijapata huduma.
 
Habari za muda huu Wanajamvi,

Hii Kampuni ya TTCL ni sikio la kufa na wala halisikii dawa tena, haifanyi vizuri kwenye mawasiliano ya simu kawaida wala kwenye Internet. Mimi nipo Dar es Salaam na nimeomba huduma ya kufungiwa internet nyumbani (fiber) na sasa yapata miezi sita ila sijafungiwa wala hakuna kitu cha maana kinachoeleweka kutoka kwao.

Ukihitaji Internet wanasema inabidi uombe kupitia website yao na ukifanya hivyo kwa kweli ni kwa haraka tu maombi yako yanapokelewa na kuambiwa yanafanyiwa kazi. Unataarifiwa mara moja kwa ujumbe mfupi (sms) na hapo hapo kwenye website yaani unaweza kusema kweli hawa jamaa ni top-notch na nitapata huduma fasta kabisa.

Ila hapo sasa ndio mchezo unapoanza, utazungushwa hadi ujute mwenyewe. Nimepiga simu zaidi ya mara 5 kwenye namba yao ya huduma kwa wateja wanapokea na jibu lao mara zote linakuwa "Ni kweli umeomba fiber, ombi lako tunaliona na tunalifanyia kazi. Mafundi wetu wa eneo lako watakupigia simu ili waje kukuunganishia". Baada ya hapo nimekuwa nikuliza kwamba hao mafundi watakuja lini atleast mnipe muda kabisa nijue au nifanye taratibu nyingine, hapo utajibiwa "Tafadhali kuwa mvumilivu, mafundi wetu watakutafuta"

Hata hivyo, baadhi ya watu wanasema TTCL hawaji kufunga internet hadi wapate shinikizo kutoka kwa Wakubwa zao. Yaani utafungiwa Internet ukiwa unawajua hao wakubwa ambapo hili ni jambo la ajabu kabisa kwa Taasisi ya Serikali kama ile inayoendeshwa kwa kodi za Wananchi.

TTCL kwa sasa sitaki tena huduma yenu hii, nitafunga internet ya watu wengine na kwa mtindo huu hamtakuja kuwa shirika la maana na hata nashangaa lile gawio mnatoa kwa Serikali huwa mnatoa wapi. Hii Kampuni inakufa hata Wakurugenzi wabadilishe kwa namna gani.

Pia soma;
1. Kuchelewa kupatikana kwa huduma ya internet ( fiber) TTCL

2. Huduma ya TTCL ya kutoa Internet nyumbani ni mbovu sana
Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,

Unakuta mtu yupo madongo kuinama A miundombinu ipo Madongo kuinama C na ili kumfikia inahitaji km kama 6 za waya na mteja ni mmoja, sasa kweli Shirika litaweza kumfikishia kila mtu ilhali bado na mhusika unaweza kuta yupo peke yake


Ndio maana wanasogeza taratibu ili iwafikie kwa ujumla
 
Mkitaka kujua hili tatizo ni kubwa kiasi gani, tembelea page zao za instagram, tafuta post zinazoitangaza fiber mlangoni kwako. Nimechukua chache mjionee. Wengine wameamua hadi kuwatag wahusika mbalimbali wenye dhamana akiwamo waziri so there is no way viongozi hawana taarifa juu ya uzembe huu.

Screenshot_2024-05-21-07-06-06-444_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-05-36-367_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-04-29-362_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-03-13-804_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-02-09-516_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-01-03-741_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-05-21-07-00-20-487_com.instagram.android-edit.jpg
 
Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,

Unakuta mtu yupo madongo kuinama A miundombinu ipo Madongo kuinama C na ili kumfikia inahitaji km kama 6 za waya na mteja ni mmoja, sasa kweli Shirika litaweza kumfikishia kila mtu ilhali bado na mhusika unaweza kuta yupo peke yake


Ndio maana wanasogeza taratibu ili iwafikie kwa ujumla
Hivi si anatakiwa aje mpimaji ili kuona miundo mbinu imekaaje then ndio wafanye maamuzi na wakujulishe juu ya maamuzi yao? Sasa hata mpimaji haji hadi miaka inapita watajuaje juu ya miundo mbinu ya eneo lako? Na walalamikaji wengine wanadai nguzo zipo mbele ya nyumba zao na baadhi ya majirani wanapatiwa huduma. Unasemaje juu ya hilo?
 
Upo wapi? Na je miundombinu ya fiber ipo karibu nawe? Ujue vitu vingine tutailaumu TTCL bure tu,

Unakuta mtu yupo madongo kuinama A miundombinu ipo Madongo kuinama C na ili kumfikia inahitaji km kama 6 za waya na mteja ni mmoja, sasa kweli Shirika litaweza kumfikishia kila mtu ilhali bado na mhusika unaweza kuta yupo peke yake


Ndio maana wanasogeza taratibu ili iwafikie kwa ujumla
Hii huduma inaombwa online kwa website yao. Mfano mimi awali ya yote niliwaambia sehemu nilipo na wakasema wapo wamefika na pia wanasema ukiona mtaa wako haupo wakati wa kujaza kwenye website basi hawajafika. Lakini nimejaza na hadi nyumba number niliikuta ile leo ni karibia mwaka hawajaja.

Halafu uungwana mwingine mteja anapopiga simu na kuuliza ni vema kusema kuwa huko hatujafika tarajia siku fulani, wanapokuwa wanasema tutakutafuta wanalenga nini?

Kama ndio utetezi mmeambiana mje kusema hapa, fikirieni upya.
 
Ndugu zao na DAWASA, wavivu sana wa kufikiri. Ni karibia mwaka sasa huduma ya maji hatujapata tangu tufanye maombi ya kuunganishiwa. Hovyo kabisa.
Mkuu hao penyeza rupia ndio maana rushwa haishi kwa sababu kama hizi. Hizo taasisi za umma nao waanze kulipwa mishahara kutokana na faida wanayozalisha
 
Haitakaa seriall iendeshe biashara.watebdaji hawana uchungu. Private sector is the best solution
 
Rewards zisipokuwa tied na performance ndio mashirika yanakuwa hivi.

Tigo Fiber nimeunganishwa ndani ya siku 1.... sijasaini hata paper moja, nimelipa pesa; kesho fiber ndani ya nyumba. Nimeletewa mkataba baada ya mwezi.

Kama upo eneo lina Tigo Fiber, nenda huko, achana na hao TTCL. Kwanza huduma yao yenyewe ni kimeo.
 
Baada ya hapo nikaja kuambiwa kuwa eneo langu kifaa cha kuunganishia fiber kimejaa hivyo engineer wao yupo kwenye process ya kutengeneza kingine.

Hiyo ilikuwa ni Septemba mwaka jana.

Mpaka leo hicho kifaa bado engineer anakitengeneza.

Nikaona bora nichukue Router ya Airtel ambayo mpaka sasa naweza kusema ndio option bora kwasababu inakupa extra benefit ya kuweza kuitumia popote lakini advantage nyingine ni kuwa na uhakika wa kupata huduma hata pale umeme unapokuwa umekatika kwasababu ina battery yenye reserve ya ku store charge kwa masaa zaidi ya 8.
Inasikitisha sana
 
Hakuna shirika la umaa linalotoa huduma inavyostahiki.

Serikali inajisumbuwa na kutia chooni pesa za walipa kodi kuendelea kuyalea haya mashirika ya umma, hayana faidia yoyote.
you meant faida? sure.
 
Nchi ya kitu kidogo hii.
Hivi mlienda na shati la mikono mirefu huko au mlienda mikono mitupu.

Walishaambiwa wale urefu wa kamba zao.
 
Mimi nimejaza form zaidi ya mara 10, nikaenda mpaka ofisini kuuliza kulikoni nikajibiwa vifaa hakuna lakini vikija nitapigiwa simu, kimya, nikajaza tena hola, nikaandika email nikajibiwa nikaunganishwa na masavea kwenye email nikawasiliana nao wakaishia mitini.
Nikaenda voda siku 3 nikapewa huduma japo ni gharama lakini afadhali.
Kama unataka fiber kwa sasa halotel ni wa moto🔥 sana na bei chee mno.
TTCL ni 🚮
 
Back
Top Bottom