Tuache kudanganyana, Ajira zina afadhali zaidi kuliko kujiajiri, watu wengi waliojiajiri ndio wapo kwenye utumwa

We jamaa hapa umefeli vibaya sana
Tatizo mnaangalia vitu hivi kwa jicho la wamarekani na ulaya ambako kuna mazingira mazuri sana ya kujiajiri.

Kibongo bongo iashara na kujiajiri sheria zimebana mno ndio maana waliotoboa wapo, lakini ni wachache

Ukiangalia hapa nchini watu wengi wenye magari, nyumba standard, wanaopeleka shule private watoto, n.k. ni waajiriwa.

waajiriwa sio matajiri lakini wengi wao at least wanaishi maisha standard ya uhakika, wafanyabiashara na waliokoakoro ni kundi lenye watu wengi zaidi lakini ndani yao wachache sana wameweza kuwa matajiri, wengi wanasota hawana uhakika (kufilisika, kufunga biashara, sheria kandamizi, task force, n.k.)
 

Uoga na mmetengenezwa hofu ya maisha ndo maana mnaogopa kujiajiri


Nchi inahitaji watu wakuthubutu Kama Fred vunja bei

Diamond n.k

Sasa kushauri vijana na kuua mind set kuwa wasijiajiri ni kukosa kuwa na vision.

Unafikiri kila MTU akipambania hizo Ajira hali itakuaje in future
 
Boss unatumia kampuni gani kubeti?
 
Mazingira hayapo stable kwa biashara hapa Tz.

Hilo ndio tatizo lililomfanya Fernandez ahamie Kenya.

idadi ya watu hao uliowataja ni ndogo sana
 
Kiufupi aliyejiajiri anauwezekano wa kufanikiwa zaidi na anauhuru kuliko mwajiriwa
 
Asikuw mtumwa dunia hii ni viumbe ambao sio binadamu

Kwa mfumo wa dunia yetu upande wa binadamu lazima tuwe watumwa wa kitu fulan ili kupata kitu cha kuendeshea maisha
 
Kujiajiri au kuajiriwa inategemeana na vitu vingi pamoja na kupata fursa na background y mtu

Mimi naona kama umejaariwa kujiajiri na unaweza mikiki yake basi nivizuri


Kuna waliojiajiri wana hali mbaya kuliko walioajiriwa , kujiajiri pekee sio kigezo cha kupata ukwasi

Ukijipata vzr kwenye kujiajiri unaweza pata hela nyingi kuliko anasubiri pension


Pia unaeza ajiriwa huku unamiradi yote sawa kiliko kutegemea kiinua mgongo ambacho kwa wengi hakizidi mil 150
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…