Tuache kudanganyana hakuna gesi iliyowahi kuuzwa na kusafirishwa kwa bomba kwenda nje ya Tanzania

Tuache kudanganyana hakuna gesi iliyowahi kuuzwa na kusafirishwa kwa bomba kwenda nje ya Tanzania

Kweli tayari nimeshachanganya naomba majibu sahihi ya maswali yangu kuhusu CNG na LNG ni ipi bora zaidi kwa magari ? gharama na pia magari ya CNG yataweza kutumia LNG ?
LNG ni gesi asilia iliyo katika kimiminika. CNG ni gesi asilia iliyo gandamizwa. Utofauti mkubwa wa LNG na CNG upo kwenye uzito katika ujazo (density). Kipino kimoja cha nishati ya LNG ni mara 3 chini ya ujazo kuliko kipimo kimoja cha CNG. Hii inamaanisha kuwa LNG ni nzito zaidi (yaani ina density kubwa), na hivyo hutoa nishati (energy) kubwa zaidi kwenye injini ikilinganishwa na CNG.

Lakini unapotumia LNG lazima uvae spacesuit, miwani ya macho, shati za mikono mirefu, suruali na gloves ili kujaza LNG kwenye tank kwasababu inakua katika hali ya baridi kali (-163°C).

CNG nifaa kwenye injini zinazofanya kazi za wastani katika umbali wa wastani. LNG ni bora kwa injini za masafaa marefu, kwa sababu tenki la LNG linajaza LNG mara 2.5 zaidi ya tenki kubwa ukubwa sawa la CNG.

CNG ni nzuri zaidi kwa magari aina ya lori, mabasi, mabasi ya shule, magari ya abiria, lori za mizigo, magari ya kubebea mizigo.

LNG nzuri zaidi kwa matrekta, meli za baharini kama vile vivuko vya pwani, lori za kubeba mizigo mizito ya migodini, vichwa vya treni.

Kwa kumalizia zaidi magari ya CNG yanaweza kutumia LNG
 
Hilo la kusema kuna bomba limechimbwa kutoka Mtwara hadi ulaya wala sishangai kwa Mtanzania kuamini maana Watanzania ni mabingwa wa kuamini visivyoaminika.

Kama unaweza kuwaaminisha nusu ya Watanzania kuwa kuna Mti ukikatwa unainuka tena, au kuna kaburi limegoma kuhamishwa ni lipi limebakia?.

hahahahaha kuna ile story ya mti wenye sura ya mwalimu Nyerere kule Tanga.
 
Nishakaribia naokota yaliyo mazuri,swali nje ya mada mkuu,oil,gas and ernegy quantity surveyor kibongo anaweza akawa anachukua Tzs ngapi kwa mwezi?
Inategemeana na kampuni au taasisi. Kama ni private company mfano zilizopo Kurasini huko nadhani wanaanzia 800k mpaka 1000k. Lkn kwa government itakua zaidi ya hapo tena sana.
 
Hapa ninajifunza mengi naomba na wale wanaosema gesi yetu imeuzwa wajitokeze hapa watufafanulie hiyo gesi yetu iliouzwa inasafirishwa kwa njia gani kwenda huko Ulaya?
 
Kwahiyo hizi story za kuwa gesi ya Mtwara imeuzwa itakuwa ni uzushi tu...
Ni hadithi tu hizo, iliwapasa wazungumzie kwa hali ya mkataba tulioingia production sharing agreement (PSA) ambao sisi hatuchangii hata shilingi kwenye uwekezaji.
Kawaida ya PSA humtaka mwekezaji azalishe gesi na kuuza mpaka atakapo rudisha gharama alizotumia kwenye uwekezaji ambayo huchukua muda fulani. Akisha rudisha ndipo mnaanza kugawana faida inayopatikana kutokana na mauzo ya gesi.

Na kiukweli mkataba tulioingia ndio mzuri zaidi ukilinganisha na mikataba mingine kama Joint Venture na Concession. Pia tunaangalia na hali ya uchumi wetu, mfano mkataba kama wa joint Venture ambao hutaka nawewe uchangie kwenye mtaji kiukweli kwa taifa lenye uchumi mdogo kama wakwetu ni risk endapo kama hatutoweza ipata gesi tuliyotarajia.

LNG plant pekee inahitaji Trillini 70 Tsh. Maana yake kama ukiamua kuingia moja kwa moja kushiriki join venture maana yake nawewe utoe Trillioni 30 au 20 kutoka kwenye bajeti yetu. Hapo ukiangalia ni risk kwa uchumi wetu.
 
Shukran kwa kutujuza, naomba kujua tuna aina ngapi za gas Mtwara ? Nasikia ipo LNG, kama ulivyotaja je hii inayojazwa kwenye magari huku Dar CNG inatoka wapi ? ni nini uhusiano wake LNG na CNG ?

Zote ni natural gesi (gesi asilia) na zinatajwa hivyo kutegemea na namna zilivyohifadhiwa...

LNG - Liquefied Natural Gas, yaani gesi ya asili imebadilishwa na kuwa kimiminika na kuhifadhiwa kwenye mitungi midogo au mikubwa,

CNG - Compressed Natural Gas, yaani ni gesi ya asili nyingi iliyokandamizwa ili iweze kuenea ndani ya mtungi au tanki, hali yake haijabadilishwa na kuwa kimiminika

Kama ulisoma somo la fizikia ya form 1 nadhani unaweza ukawa unakumbuka kuwa "matter can never be destroyed nor created, but it can be transformed in different forms" - Law of Conservation of Mass

Ni kama vile tu unapoweza chemsha maji yakawa mvuke au ukayagandisha yakawa yabisi, lakini mwisho wa siku ni maji yale yale au ukaupooza mvuke na ukawa maji...(Hii ulifundishwa katika somo la Sayansi ukiwa darasa la tano)
 
Kivipi tena boss, mbona elimu ipo wazi kabisa.

Gesi inaweza uzwa Ulaya kabla hata haijachimbwa mkuu, kama vile dhahabu, almasi na tanzanite zinavyomilikiwa na makampuni ya nje zingali ardhini Tz.


Ufafanuzi wako wa hivyo vifupi
(LNG,CNG,LPG) ni sawa kabisa.

Lakini kuuza gesi iliyoko Tanzania Ulaya, America au China siyo lazima iwe physical.
 
Hiyo gesi ambayo tumekua tukiitumia kabla ya kugunduliwa gesi ya Mtwara inaitwa Liquefied Petroleum Gas (LPG). LPG imeundwa kwa kampaundi za propane na butane. LPG ndio gesi inayouzwa na akina Mihani, Oryx, Taifa, Lake n.k.
LPG unaweza kuihifadhi nyingi kwenye mtungi katika mgandamizo mdogo (low pressure) kisha ukaweza kuisafirisha popote duniani ikiwa kwenye mtungi.

Gesi yetu ya Mtwara imeundwa kwa kampaundi ya methane. Ili uweze kuisafirisha nje ya nchi katika mataifa ya mbali njia pekee yenye faida ni kuibadilisha kuwa kimiminika kwanza kwa kuipoza katika joto la (-163 °C) kisha iweke kwenye mitungi yenye kuweza kuhifadhi hilo joto pakia kwenye meli. Ila katika umbali mfupi njia pekee yenye faida ni kutumia bomba tu.
Na mbaya zaidi huwezi kupikia gesi asilia ikiwa kwenye mtungi. Ili uweze kupikia gesi asilia unatakiwa kupikia ikiwa ndani ya bomba. Hivyo kwa Tanzania ili tuweze kupikia gesi asilia tunatakiwa kusambaza mabomba kwenye nyumba zote zenye uhitaji.

Hivyo tatizo kubwa la gesi asilia lipo kwenye uhifadhi na usafirishaji.

Kwa umbali mrefu ukitumia bomba ni hasara. Maana yake ujenge bomba kutoka Mtwara mpaka ulaya (dhana potofu).
Otherwise ujenge kiwanda cha kuzalisha LNG (ambacho kama kingekuwepo tungekiona tu)
Shukrani.
Hiyo gesi inayotumika kuzalisha umeme Dar es Salaam ni gesi ipi na imefikishwaje Dar?
 
Ni hadithi tu hizo, iliwapasa wazungumzie kwa hali ya mkataba tulioingia production sharing agreement (PSA) ambao sisi hatuchangii hata shilingi kwenye uwekezaji.
Kawaida ya PSA humtaka mwekezaji azalishe gesi na kuuza mpaka atakapo rudisha gharama alizotumia kwenye uwekezaji ambayo huchukua muda fulani. Akisha rudisha ndipo mnaanza kugawana faida inayopatikana kutokana na mauzo ya gesi.

Na kiukweli mkataba tulioingia ndio mzuri zaidi ukilinganisha na mikataba mingine kama Joint Venture na Concession. Pia tunaangalia na hali ya uchumi wetu, mfano mkataba kama wa joint Venture ambao hutaka nawewe uchangie kwenye mtaji kiukweli kwa taifa lenye uchumi mdogo kama wakwetu ni risk endapo kama hatutoweza ipata gesi tuliyotarajia.

LNG plant pekee inahitaji Trillini 70 Tsh. Maana yake kama ukiamua kuingia moja kwa moja kushiriki join venture maana yake nawewe utoe Trillioni 30 au 20 kutoka kwenye bajeti yetu. Hapo ukiangalia ni risk kwa uchumi wetu.
Hayati Magufuli aliposema gesi ya Mtwara tumeshapigwa alikuwa amekusudia nini ?? Je hakuwa well informed na watu wake. ?? Inawezekana Rais akadanganywa namna ile. ??
 
Back
Top Bottom