Tuache kudanganyana hakuna gesi iliyowahi kuuzwa na kusafirishwa kwa bomba kwenda nje ya Tanzania

Tuache kudanganyana hakuna gesi iliyowahi kuuzwa na kusafirishwa kwa bomba kwenda nje ya Tanzania

Ni CNG, huko inakotoka mpaka kufika Kinyerezi inapitia kwenye compressor stations zinazofanya kazi hiyo ya kuigandamiza kuwa CNG
Pamoja na maelezo yako mazuri huko nyuma, hapa naongeza yafuatayo;
Kiasili gesi asilia Ina pressure kutoka ardhini (visima vina msukumo wa kutosha). Compressor hutumika tu pale ambapo gesi imepungua (kuelekea kuisha) na hivyo pressure iliyokusudiwa kuendesha mitambo kutoka kwenye kisima kutofikiwa.
 
Ila naomba tena usichanganye LNG na LPG.
LPG ni liquefied petroleum gas na imeundwa kwa kampaundi za propane na butane.
LPG huwa inazalishwa wakati wa kuchakata mafuta ghafi (crude oil) au wakati wa kuchakata gesi asilia yenye kiwango kikubwa cha butane na propane.
LPG haipo Tanzania, huagizwa kutoka nje ya nchi. LPG ndio gesi tunayotumia kupikia majumbani (Oryx, Mihani, Taifa n.k).

Ili kupata LPG tunazikandamiza butane na propane katika mgandamizo mdogo tu (low pressure). Baada ya hapo butane na, propane zinakua kimiminika.

Ili kupata CNG tunaikandamiza gesi asilia (methane) katika pressure kubwa.

Ili kuipata LNG tunaipoza gesi asilia (methane) katika joto la (-163 °C)
Ndio kusema LNG haina soko nje kutokana na gharama zake na uwepo wa LPG. LNG Mataifa ya nje hawaitaki coz ina gharama ya kuichakata na pia uwepo wa LPG ya kutosha kwahiyo Gas yetu haiwezi kutupatia pesa za kigeni na ndio maana hata JPM akaona aikaushie tu na hata mataifa ya nje kutokua na shobo nayo
 
Wabongo wameshazoea uongo uongo kudanganywa danganywa.

Huu uongo alianza nao Dr Slaa mwaka fulani kwenye kampeni eti kuna gas inaibiwa inapelekwa ulaya kwa bomba kupita baharini, toka siku hiyo nilimdharau sana Dr Slaa.

Yaani kwa akili ya kawaida kabisa, Project ya kujenga bomba baharini from mtwara to Europe inaweza kuwa project ya kitoto?
Na wewe umedanganya, Dr.Slaa alisema ni mafuta na siyo gesi na wala hakusema kuna bomba la gesi kwenda ulaya.
 
Hayati Magufuli aliposema gesi ya Mtwara tumeshapigwa alikuwa amekusudia nini ?? Je hakuwa well informed na watu wake. ?? Inawezekana Rais akadanganywa namna ile. ??
Alikuwa na maana ya kwamba mikataba tulioingia ya uchimbaji wa gesi hainufaishi nchi badala yake inawanufaisha zaidi waliowekeza kuchimba hiyo gesi maana wataendelea kutuuzia hiyo gesi kwa bei kubwa hadi warudishe gharama na faida kwa miaka mingi. Wakati wa JPM nia yake ilikuwa kuharakisha ujenzi wa bwawa la JNHPP ili ujenzi wake ukamilike mapema na kuua biashara ya kuiuzia nchi gesi na umeme unaozalishwa na gesi kwa bei kubwa. Kumbuka Serikali ina mkataba na Songas ya kutuuzia umeme unaozalishwa na gesi hadi 2024.
 
Unapo zungumzia gesi ni tofauti sana na mafuta katika swala zima la uhifadhi na usafirishaji.

Ili kuweza kuisafirisha gesi nje ya nchi unahitaji miundo mbinu ya kuweza kuibadilisha kuwa kimiminika.

Ikiwa katika hali ya kimiminika ndipo unaweza kuipakia kwenye meli ikiwa kwenye mitungi maalumu na kuisafirisha hadi nje ya nchi.

Mbaya zaidi huwezi kujenga bomba la gesi kutoka Tanzania hadi ulaya. Pesa utakayotumia itakua kubwa sana kuliko faida utakayoipata.

Mara nyingi mabomba ya kuisafirisha gesi asilia hujengwa katika umbali mfupi mfano mkoa hadi mkoa au wilaya hadi wilaya.

Sasa unapomsikia mtu anasema bomba zimechimbwa kutoka Mtwara hadi Ulaya unawaza hivi inawezekanaje? Unakuja kugundua labda kunatatizo katika elimu hii ya mafuta na gesi.

Gesi ya Mtwara bado ipo zaidi itaanza kuzalishwa mpaka LNG plant itakapokua imejengwa.

Hii inayozalishwa sasa ni kiasi kidogo tu.

Karibuni kwa maswali sasa


Mengineyo:
Kwa ushauri kuhusu maswala ya gesi na mafuta pia karibuni.

Nakukumbusha nyumba yako itakua salama endapo kama mtungi wa gesi ya kupikia (LPG) utahifadhiwa mahali penye hewa ya kutosha nje ya nyumba yako, na kupitisha mpira wa gesi kupitia ukutani au dirishani mpaka kwenye jiko lako jikoni.

Pika salama lala kwa amani bila hofu.
Usichokijua ni kwamba maeneo au visima vyenye gesi vimeshauzwa kwa makampuni vya nje Enzi za kikwete ndo maana magufuli anasema hatuna chetu tumebakiwa na visima vichache.lakini maeneo yenye gesi nyingi yameshauzwa.
 
Unapo zungumzia gesi ni tofauti sana na mafuta katika swala zima la uhifadhi na usafirishaji.

Ili kuweza kuisafirisha gesi nje ya nchi unahitaji miundo mbinu ya kuweza kuibadilisha kuwa kimiminika.

Ikiwa katika hali ya kimiminika ndipo unaweza kuipakia kwenye meli ikiwa kwenye mitungi maalumu na kuisafirisha hadi nje ya nchi.

Mbaya zaidi huwezi kujenga bomba la gesi kutoka Tanzania hadi ulaya. Pesa utakayotumia itakua kubwa sana kuliko faida utakayoipata.

Mara nyingi mabomba ya kuisafirisha gesi asilia hujengwa katika umbali mfupi mfano mkoa hadi mkoa au wilaya hadi wilaya.

Sasa unapomsikia mtu anasema bomba zimechimbwa kutoka Mtwara hadi Ulaya unawaza hivi inawezekanaje? Unakuja kugundua labda kunatatizo katika elimu hii ya mafuta na gesi.

Gesi ya Mtwara bado ipo zaidi itaanza kuzalishwa mpaka LNG plant itakapokua imejengwa.

Hii inayozalishwa sasa ni kiasi kidogo tu.

Karibuni kwa maswali sasa


Mengineyo:
Kwa ushauri kuhusu maswala ya gesi na mafuta pia karibuni.

Nakukumbusha nyumba yako itakua salama endapo kama mtungi wa gesi ya kupikia (LPG) utahifadhiwa mahali penye hewa ya kutosha nje ya nyumba yako, na kupitisha mpira wa gesi kupitia ukutani au dirishani mpaka kwenye jiko lako jikoni.

Pika salama lala kwa amani bila hofu.
Kwa hiyo Kikwete ameshauza maeneo au visima vyenye gesi na inasemekana pia Katoa mengine kwa wachina ili amuokoe kijana wake alipokamatwa na madawa ya kulevya.
 
Alikuwa na maana ya kwamba mikataba tulioingia ya uchimbaji wa gesi hainufaishi nchi badala yake inawanufaisha zaidi waliowekeza kuchimba hiyo gesi maana wataendelea kutuuzia hiyo gesi kwa bei kubwa hadi warudishe gharama na faida kwa miaka mingi. Wakati wa JPM nia yake ilikuwa kuharakisha ujenzi wa bwawa la JNHPP ili ujenzi wake ukamilike mapema na kuua biashara ya kuiuzia nchi gesi na umeme unaozalishwa na gesi kwa bei kubwa. Kumbuka Serikali ina mkataba na Songas ya kutuuzia umeme unaozalishwa na gesi hadi 2024.
Kumbee !! Tunaumizana sisi kwa sisi halafu tunasema wengine ni wajanja wa mjini !! Salaaleeh !!
 
Ila naomba tena usichanganye LNG na LPG.
LPG ni liquefied petroleum gas na imeundwa kwa kampaundi za propane na butane.
LPG huwa inazalishwa wakati wa kuchakata mafuta ghafi (crude oil) au wakati wa kuchakata gesi asilia yenye kiwango kikubwa cha butane na propane.
LPG haipo Tanzania, huagizwa kutoka nje ya nchi. LPG ndio gesi tunayotumia kupikia majumbani (Oryx, Mihani, Taifa n.k).

Ili kupata LPG tunazikandamiza butane na propane katika mgandamizo mdogo tu (low pressure). Baada ya hapo butane na, propane zinakua kimiminika.

Ili kupata CNG tunaikandamiza gesi asilia (methane) katika pressure kubwa.

Ili kuipata LNG tunaipoza gesi asilia (methane) katika joto la (-163 °C)
Lakini bandugu Kwa Mzungu akitaka jambo lake huwa hashindwi !!
 
Meli ngapi za kuvua samaki zinavua kiharamu huko bahari kuu nani anaziona ?? Kwani gesi ambayo tumekuwa tukiitumia miaka mingi kabla hata ya kugunduliwa hiyo ya mtwara ilikuwa inasafirishwa kwa kutumia njia zipi mpaka zitufikie hapa TZ ??
Unachozungumza kuhusu samaki ni kweli ila sio kwa gesi asilia. Ili uweze kusafirisha gesi asilia unahitaji kuwa na bomba kutoka mahali inapozalishwa gesi hadi huko ulaya. Kujenga bomba hadi ulaya ni gharama zaidi ya faida utakayoipata ukiuza hiyo gesi. Njia ya pili ni kuibadilisha hiyo gesi kuwa kimiminika (LNG) kisha unaiweka kwenye mitungi na kuisafirisha hadi nje ya nchi kuiuza. Kufanya hivyo lazima ujenge kiwanda cha kuipoza hiyo gesi ili iwe kimiminika. Hicho kiwanda ni ghali sana (70Trillion Tsh). Hapo inahitaji utafute wawekezaji wakubwa. Kwa serikali zetu zenye bajeti ndogo, kufanya uwekezaji wa 70T kwa mambo ya gesi na, mafuta inaweza kuwa ni risk. Kwa hiyo lazima uwaachie wazungu wajichange wenyewe.

Gesi ambayo huwa inatufikia hapa Tanzania inaitwa LPG, hiyo huwa sio kazi kuisafirisha. Kwasababu kwanza kuibadilisha kuwa kimiminika na kuiweka kwenye mitungi unahitaji mgandamizo (pressure) kidogo sana.
 
Kwa hiyo Kikwete ameshauza maeneo au visima vyenye gesi na inasemekana pia Katoa mengine kwa wachina ili amuokoe kijana wake alipokamatwa na madawa ya kulevya.
Usiwaseme viongozi kwa mambo usiyoyajua rafiki. Ni vyema tujikite kuelimishana tu na sio kusambaza taarifa tusizo zijua.
 
Hayati Magufuli aliposema gesi ya Mtwara tumeshapigwa alikuwa amekusudia nini ?? Je hakuwa well informed na watu wake. ?? Inawezekana Rais akadanganywa namna ile. ??

Mara tu gesi asilia inapochimbwa, huuzwa kwa serikali na hayo makampuni ya wazungu...

Mkataba uliopo ni huo wa manunuzi na bila shaka JPM alilenga kwenye mktaba huo...
 
Mara tu gesi asilia inapochimbwa, huuzwa kwa serikali na hayo makampuni ya wazungu...

Mkataba uliopo ni huo wa manunuzi na bila ahka JPM alilenga kwenye mktaba huo...
Na hiyo inafuatana na mkataba mlio ingia. Mwanzoni huwa hivyo mpaka mwekezaji arudishe gharama zake.
 
Back
Top Bottom