Tuache kulalamikia TISS kwa majukumu yasiowahusu ya kudhibiti ufisadi au kuendesha uchumi wa nchi

Tuache kulalamikia TISS kwa majukumu yasiowahusu ya kudhibiti ufisadi au kuendesha uchumi wa nchi

Namaanisha, mtu kaingia nchini kakopa kwenye bank kadhaa na kaondoka na mzigo wa hela
Ndio Ila hio ya kutoa Pesa si hua wanawarushia mpira Katibu Mkuu sio hao Security sijasikia Mimi hao Security wakilaumiwa kwa kuacha wezi waibe kisha waondoke na wao wapo ikiwa wezi wameshirikiana na mtu wa ndani kwenye Wizara nyeti, wewe ukiwa km ndio Security utafanya nini ?
 
Likitengo la ovyo kabisa kuwahi kutokea Tanzania, hawana tofauti na chawa na kazi yake kubwa ni kulamba makalio ya CCM , wapinzani wakichukua nchi au Raisi anayejitambua kazi ya kwanza iwe ni kulifumua hili likitengo na kufukuza mbalagala wote mpaka mlinzi wao wa geti, naamini machinga wanaweza fanya kazi nzuri kuliko hili likitengo la sasa
 
Ndio Ila hio ya kutoa Pesa si hua wanawarushia mpira Katibu Mkuu sio hao Security sijasikia Mimi hao Security wakilaumiwa kwa kuacha wezi waibe kisha waondoke na wao wapo ikiwa wezi wameshirikiana na mtu wa ndani kwenye Wizara nyeti, wewe ukiwa km ndio Security utafanya nini ?
Neno security ni pana na inategemea tuna liangalia kwa picha ipi katika swala kama hilo.
 
Granda corruption ikifanyika kwenye sekta ya afya sio tishio kwa usalama, raia wanyonge wataumia tu, ila grand corruption ikifanyika kwenye jeshi inaweza kuwa tishio kwa usalama wa taifa.
Nisaidie kunielimisha, unaposema wanyonge wakipatashida sio tishio kwa taifa ira jeshi ndio tishio. Kwani Taifa ili liitwe taifa vitugani vinafanya kuwa taifa
 
TISS sio General services unity, ingekuwa general kusingekuwa na PCCB, CID, Financial Intelligence Unit ya BoT, Millitary Intelligence n.k
Mkuu huko kote PCCB,CID,Financial Intelligence unit,MI lazima wapandikize watu kututo Tiss nilikuwa nawaza tu mkuu
 
Taasisi inayoheshimika kwenye hii nchi kwa sasa ni JWTZ tu. Zingine zote 'ufisadi uendelee.'
 
Mkuu huko kote PCCB,CID,Financial Intelligence unit,MI lazima wapandikize watu kututo Tiss nilikuwa nawaza tu mkuu
Sio kupandikiza, wanaitwa liaison officers.
 
Tiss sio wa kuwalalamikia.

Hangaika na utawala ulipo.
 
Sijwahi kuona taifa lingine ambalo wizi/ufisadi wa mali za umma unatokea halafu Idara za ujasusi ndizo zinalaumiwa.

Ukosoma sheria ya kuundwa kwa TISS kazi ya inahusu usalama wa taifa "security". Kufuatilia rushwa, ufisadi katika ofisi za umma, kuendesha uchumi, kupambana na madawa ya kulevya sio kazi yao. Hayo ni majukumu ya vitengo vingine vingi vilivyoundwa mahususi kwa shughuli hizo.

Wao wanapaswa kuingia tu kwenye uchunguzi wa mambo hayo endapo yanahusisha usalama wa taifa, mfano mtu anauza dawa za kulevya kufadhili ugaidi au mtumishi amepewa rushwa kutoa classified information za nchi. Sio kila ufisadi, au biashara haramu ni jukumu la TISS.

Act yao inasema to obtain, correlate, and evaluate intelligence "relevant" to security.

Tuache kwapa TISS majukumu yasiyowahusu, hii ni slippery slope mbaya sana inatengenezwa kwa kufanya hivi. TISS wanapaswa kufanya kazi zao kulingana na Act yao iliyounda hiyo idara.
Wqnapewa majukumu yasiyowahusu na wanasiasa uchwara na sisi tunawamulika humo humo wanakotumwa.

Maslahi ya Nchi ni mapana sana na siyo ya kikundi cha wachache wanaomiliki funguo za hao tisi
 
Teeth Haina faida yoyote kwa sasa.

Military inteligence inatosha kufanya kazi.

Uvsisiem wanapeana mashavu ya huko teeth.

Sisiem imeharibu nchi

imagine mpka mwenye kiti anaondolewa kinyemela na hao teeth wapo kurndeshwa na kikundi cha watu.

R.I.P Jembe
 
Sijwahi kuona taifa lingine ambalo wizi/ufisadi wa mali za umma unatokea halafu Idara za ujasusi ndizo zinalaumiwa.

Ukosoma sheria ya kuundwa kwa TISS kazi ya inahusu usalama wa taifa "security". Kufuatilia rushwa, ufisadi katika ofisi za umma, kuendesha uchumi, kupambana na madawa ya kulevya sio kazi yao. Hayo ni majukumu ya vitengo vingine vingi vilivyoundwa mahususi kwa shughuli hizo.

Wao wanapaswa kuingia tu kwenye uchunguzi wa mambo hayo endapo yanahusisha usalama wa taifa, mfano mtu anauza dawa za kulevya kufadhili ugaidi au mtumishi amepewa rushwa kutoa classified information za nchi. Sio kila ufisadi, au biashara haramu ni jukumu la TISS.

Act yao inasema to obtain, correlate, and evaluate intelligence "relevant" to security.

Tuache kwapa TISS majukumu yasiyowahusu, hii ni slippery slope mbaya sana inatengenezwa kwa kufanya hivi. TISS wanapaswa kufanya kazi zao kulingana na Act yao iliyounda hiyo idara.
Kaka unapotosha, hivi unajua yote uliyotataja yanahusika na Usalama wa Taifa,,ndio maana unakuta head wa Pccb,ofisi ya CAG au madawa ya kulevya ni Mtu wao.Tiss wapo kila mahali,na wanafanya kila kitu,katika kuona namna bora ya kuendesha nchi.ule ni mkono wa Rais kufahamu kila linaloendelea. Na taarifa zote zipo sema wanaoenforce ni Taasisi zingine,na wafanya maamuzi ni taasisi nyingine.kwamfano taarifa za rushwa au jinai ili zikamilike,lazima mtu achunguzwe kijinai,afunguliwe mashtaka awe prosecuted mahakamani afungwe.so idara itakuwa ilishatimiza kazi yake.mf.CAG ameshatoa riport itabidi ijadiliwe bungeni yatoke maazimio etc due process ifanyike.so idara inafanya kazi zake kwa weledi, sema mifumo ya kuenforce inakuwa ya kirasimu na inatoa fursa ya haki kwa kila upande kwa mujibu wa katiba na sheria nyingine.
 
We ni chizi kweli et sio majukumu ya TISS mbona wanareport mambo machafu ya watu wa chini kwann hawareport ama kugundua huo uchafu wa watu wa juu tiss wapo kwenye mashirika halimashaur vyuoni makanisan msikitin masokon lkn wanagundua madudu ya watu wa chini tu
 
Back
Top Bottom