Tuache mazoea ya kuvumilia kila kitu kwenye ndoa

Tuache mazoea ya kuvumilia kila kitu kwenye ndoa

Bahati mbaya hakuna kanuni kwenye hilo wapo waliovumilia namwisho ikawa kicheko nawengine ikawa kilio kila mtu asikilize moyo wake usijaribu kumwambia mwanandoa hapo alipo hapastaili utapata aibu baadae
 
Kuna kuvumilia na kuna kupoteza muda,wengi wanapoteza muda.
 
Biashara ni ubepari haina kuoneana huruma.[emoji276]
 
Tuache upumbavu wa kusema "NDOA NI UVUMILIVU" .... Wanawake wengi wamepoteza kazi, ndoto zao na hata wengine wamelemazwa kabisa kwasababu ya huu upuuzi wa kusema "NDOA NI UVUMILIVU" ..... na kuna wale ambao wameuawa katika ndoa.

Ninyi wazazi ambao mnakimbilia kila mara kuwaambia binti zenu kuvumilia mambo ya kinyama katika ndoa, tafadhali acheni upuuzi huo.

Nanyi wanawake wapumbavu mnaonyanyaswa halafu mnaendelea kuvumilia ujinga kwa sababu mnaamini kuwa ndoa ni uvumilivu, ninaamuru mara moja kuacha ujinga huo.

NDOA NI FURAHA NA AMANI, NA SI VINGINEVYO. UNANIELEWA ??
Uvumilivu ni dhamana nzuri ya mwanadamu ambayo lazima iwepo katika mazingira yote ya wanadamu, ili kukabiliana vizuri na shida ambazo zinaweza kutokea kutafakari na kuchukua msimamo bora.

Hata hivyo hatupaswi kuvumilia mambo maovu yanayotendwa juu yetu, ikiwa Mungu Mwenyewe anasema yeye havumilii uovu, bilashaka hata sisi pia hatupaswi kuvumilia uovu lazima tuchukuwe hatua sahihi.
 
Usipovumilia basi hata mwezi hukai, sema tu kuna zile abusive behaviour hutakiwi kukaa nazo. Ila uvumilivu ni muhimu, uvumilie kutopewa utamu, uvumilie kununiwa... uvumilie... lakini sio kupigwa kama ng'ombe, mkishindwana peaneni nafasi!
 
Sasa wewe ndoa za wengine unazowapa ushauri zinakuhusu?

Umeamka na kisununu sana Asubuhi hii, au ndo Mambo ya mwezini?
ID yako inaashiria ni mtu mwenye akili ila mbona maandishi yako yanakusaliti?
 
Usipovumilia basi hata mwezi hukai, sema tu kuna zile abusive behaviour hutakiwi kukaa nazo. Ila uvumilivu ni muhimu, uvumilie kutopewa utamu, uvumilie kununiwa... uvumilie... lakini sio kupigwa kama ng'ombe, mkishindwana peaneni nafasi!
Mimi namaanisha huu unyama wa hadi wengine kuuana au kupeana vilema vya maisha. Na thread nimeanzisha baada ya mwaka huu kutokea visa vingi vya watu kuuana hapa nchini na nje ya TZ.
 
Ngapi huko? Ukiona hivo ujue kashavurugwa mtu.
 
Si mwanaume si mwanamke wote wakiwa kwenye ndoa,wanakutana na mabalaa

Ova
Mzee wa Kinondoni mbona hujatoa tamko kwa hii ishu ya afisa aliyekamata mzigo wa madawa ya kulevya kukamatwa na kushikiliwa pasipojulikana? Ina maana wazee wa Kinondoni ndo wanarudi kwenye enzi zao upya?
 
Mzee wa Kinondoni mbona hujatoa tamko kwa hii ishu ya afisa aliyekamata mzigo wa madawa ya kulevya kukamatwa na kushikiliwa pasipojulikana? Ina maana wazee wa Kinondoni ndo wanarudi kwenye enzi zao upya?
Hahaha hahaha
Mzee pm kunakuwaga na mushkeli sana

Nilipata hiyo code,wazee mbona wako kazini
Sana bado tena ukiisha moto ni ule ule
Si ulisikia ile issue ya tegeta+ununio+kino

Ova
 
Back
Top Bottom