Tuache upotoshaji; Deo Bonge alikuwa anakamatwa sio kutekwa

Alikuwa anakamatwa na nani?
Acha ujinga bro, niliishawahi kukamatwa mchana kweupe na makachero wa polisi,wawili, walifika nilipokuwa, wakanitajia kosa,na anayenishitaki, wakaniambia inabidi wanifunge pingu, wanipereke mtwara polisi kujibu mashitaka, wakanionyesha vitambulisho na hati ya mahakamani, wakanibeba kwenye boda, tukafika central, aliyenishiitaki nikamkuta, nikaingizwa ndani, nikahojiwa, nikakana, basi wakaniambia aliyenishiitaki inabidi alete ushahidi ndio kesi iendelee, nikaacha mawasiliano, nikaambiwa nipo huru kuondoka, mpaka ushahidi ukiletwa, wataniita, imepita miaka 12 sasa!
Kama wale night polisi walienda kumkamata,mpaka Leo, mbona hawajitokezi, hawa polisi wetu wakija kukukqmata, ukigoma watakuulia hapo hapo, tumeona kwa viongozi wa chadema,
Wale ni kikosi maalum cha kuteka na kuua wapinzani,
Polisi wametoa tamko, watafsnya uchunguzi! Wa nini?kama ni polisi wao?hapo, ni kukili tu, wale walikuwa wenzetu afande so and so!
Tuliwatuma, mpaka sasa hv, 60hrs hawajasema, wale ni watekaji, watesaji, wauaji, hz operations zina Baraka yq samia, period!
 
We Jamaa ni Bogus wa mwisho akili umepeleka wapi.
Kumkamata mtu ndio Mje na Gari private na Askari wavae kiraia na wamkamate mtu kwa kusema tu sisi ni Askari bila kuonyesha kibali cha kumkamata na vitambulisho.
 
Pumbavu kabisa... OK, kama alikuwa anakamatwa kama unavyotaka wewe tuamini, kwanini hao unaoita wakamataji, ambao wewe unatuthibitishia kuwa ni polisi.
Kwanini walikimbia wakati walikuwa wanafanya kazi yao kwa mujibu wa sheria?
Pumbavu tena.
 
Ni wazi wewe ni mmoja kati ya hao watekaji, utafutwe uunganishwe nao.
Baada ya tukio lile Deo alikwenda kuripoti polisi na polisi walifungua jarada la upelelezi, kama angekuwa anakamatwa na hao unaodai ni askari ambao na wahslifu wenzako, ni wazi Deo angeshikiliwa hapo kituoni, sasa hao walitumwa toka wapi?
 
Baada ya Tukio kuisha Bonge alikwenda kituoni Gogoni. Kutoa riport. Na kufunguliwa pingu.
Kama ulikua ukamataji wa kawaida mbona hawakumkata tena kumeweka ndan/Sero.
Kwa Tanzania ya Sasa hatutak tena mambo ya kutekana tena
 
Do you know the meaning and the differences between ARREST and ABDUCTION??
 
Kitendo cha kumwacha tu kinatosha kuthibitisha kuwa alikuwa anakamatwa kwa kutekwa kama sivyo wange fuata hata wajumbe wa nyumba 10 pia kungekuwa hata na polisi wenye uniform nk
 
Mwenye akili hawezi kusema kuwa eti alikuwa anatekwa!!!! Utekaji hauwezi kufanyika vile.

waliomkamata walitumia nguvu ya wastani sana, hawakumjeruhi licha ya Deo kukaidi kwa nguvu zote, huo hakuwa utekaji bali ukamatqji halali.
Na Kibao je?
 
Wewe ni yupi kati ya wale watekaji??

Umejifichia wapi kwanza?? Mtakamatwa tu
 
Hata Uwesu ilikuwa hivyo hivyo, wakamataji 'kisheria' huwa hawamshindwi individual ilibidi mawasiliano ya radio hutumika kuongeza nguvu. Police pia immediately wangetoa taarifa yao baada ya tukio kwenda viral ili public ifahamu mbivu na mbichi, wakamataji huwa hawakimbii eneo la tukio wakati hawakuwa wakishambuliwa.
Trying to spin this obvious truth naamini kuna kitu unafahamu kuhusu huu utekaji uliofeli, mafala wapuuzi wote waliohusika ni watekaji kwani ukamataji huwa una taratibu zake za kisheria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…