I M
JF-Expert Member
- Dec 23, 2012
- 434
- 767
Tukio la kukamatwa kwa Deogratius Tarimo lililotokea katika eneo la Kiluvya linaonekana wazi kabisa kuwa alikuwa ana kamatwa na watu ambao walijitambulisha kuwa ni Askari, hakuwa anatekwa.
Mwenye akili hawezi kusema kuwa eti alikuwa anatekwa!!!! Utekaji hauwezi kufanyika vile.
waliomkamata walitumia nguvu ya wastani sana, hawakumjeruhi licha ya Deo kukaidi kwa nguvu zote, huo hakuwa utekaji bali ukamatqji halali.
Tuache uzushi, tuache uchunguzi ufanyike kisha ukweli utabainika.
Deo hakupigwa wala kujeruhiwa popote pale zaidi ya yeye mwenyewe kujirusha lkn wakamataji hawakumpiga ngumi wala teke.
Wangekuwa watekaji wangeweza kumpa kipigo cha kumtoa fahamu kisha kumtupia kwenye gari, lkn haikuwa hivyo... hii inaonyesha kama hao watu walikuwa wanamkamata sio kumteka.
Upumbavu kama huu ni mzigo kwa Taifa, Tukiwa na watu na viongozi kama nyie kuendelea ni ngumu sana.