Ndiyo!!! (uliuliza "Nasema uongo jamani?"). Chanjo ipi imetumiwa kuleta ugumba??? Wachina walipunguza idadi ya watoto kuliko kila nchi duniani lakini hawakutumia chanjo. Hakuna chanjo ya kuzuia watoto.
Marekani hawana shabaha kupunguza idadi ya watu wao 2.4% (wala %% yoyote). Kinyume wanaendelea kupokea wahamiaji kutoka nchi nyingine ili kujenga uchumi wao.
Kama sasa wameleta chanjo ya Johnson - kwa sababu walibaki nayo baada ya kuchanja watu wengi wengi tayari, na kwa sababu ile chanjo ya JJ ilichelewa kufika sokoni. Hapo sababu ya kufikia watu wachache huko. Lakini wamechanja mamilioni ya watu wao , na bila shaka SI KWA KUSUDI KUWAUA.
Kwa Astra Zeneca kama huko Kenya TZ imechelewa shauri ya kiburi cha mwenda zake. Itarudi baadaye.