Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
- Thread starter
-
- #121
Mkuu Tujitegemee, kwanza nisamehe, nilihisi hili nilijijibu kule kwenye main thread ya karma,Mkuu Pascal Mayalla nakumbuka ulijibu swali langu hili hapa chini. Lakini majibu yako siyaoni jamvini na kwenye uzi huu. Uliyafuta majibu yale!?
===
Mkuu Tujitegemee, majibu ya hili yako kwenye the main thread ya karma.Asante kwa uzi huu... Nina swali kidogo kuhusu Karma. Tumeelezwa kuwa Karma inatabia kama ya tukio la ' what goes around comes round' ...pia tumeelezwa kuwa karma ni sawa na sheria za Newton za Every action there is equal and opposite reaction. Swali lenyewe sasa....Mkuu, Ni wakati gani tunatambua kuwa Sasa Karma 'is going around' ama 'is coming around'....Na pia ni wakati gani tunaweza kusema sasa Karma is an ACTION na siyo REACTION?
Kwa kifupi, ni wakati gani ama ni vigezo vipi tunatumia kutambua kuwa sasa Karma inaanzisha duara na ama sasa KArma inafunga duara?
===
Kwa haraka haraka ninajua kabisa umelielewa swali langu barabara. Nasubiri majibu Mkuu.
Duh...!.View attachment 1472626
View attachment 1472650
Salaam,
Taarifa nilizozipata hivi punde toka chanzo changu kinanihabarisha kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman A. Mbowe amevamiwa na kikundi cha watu wasiojulikana akielekea nyumbani kwake usiku huu na kupigwa na wamemuumiza.
Tukio hili limetokea majira ya saa 6-7 usiku.
Mhe. Mbowe amekimbizwa Hospitali ya Ntyuka iliyopo jijini Dodoma.
Kamanda Muroto amesema wamepata taarifa kuwa kavunjwa mguu wa kulia na amelazwa Wodi namba 4 hospitalini hapo. Amesema taarifa zaidi zitafuata
MAONI YANGU:
Mhe. Mbowe kuvamiwa na kupigwa eneo la Area D, jijini Dodoma, Mtaa wa Sengia; linalotajwa kuwa na ulinzi wa kutosha, kama ilivyotokea kwa Lissu kunaacha maswali mengi, je, hili linaweza kuwa limechochewa na Lissu kutangaza nia ya kugombea Urais wa JMT October 2020? Ni hasira au kitu gani? No one knows.
Bado najiuliza; hivi kama Taifa kwa tabia hizi za kihuni tunaelekea wapi? Hawa wanaojichukulia sheria mikononi kila siku wanafanya hivyo kwa kutumwa na nani? Matendo haya yataendelea kwa viongozi wa upinzani mpaka lini?
We need to wake up, better late than never.
Dodoma ni mji wa kihalifuDuh...!.
Hii ni hatari sana!.
Hata shambulio hili la Mhe. Mbowe, limefanywa na watu wasiojulikana, hivyo nawaomba sana tusihujukumu, kwa kupiga ramli chonganishi ili na sisi tusihukumiwe!.
Pole sana Mhe. Mbowe,
Get well soon.
P
Ramli ni ubashiri, kuna ubashiri mzuri kama huuPascal Mayalla
Hivi huwa kuna ramli ambayo siyo chonganishi? Na kama ipo, ikoje?
Ubashiri peke yake bila nyongeza yoyote ya nguvu zilizo nje ya mamlaka ya Mungu siyo ramli bali ni utabiri! Ramli ni ubashiri unaoambatana na matumizi ya nguvu nyingine za nyongeza ambazo hazitokani na mamlaka ya Mungu. Kwenye utabiri Mungu huwa anashiriki 100% ila kwenye ubashiri mchango wa Mungu ni 0%Ramli ni ubashiri, kuna ubashiri mzuri kama huu
Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
P
Mwanzo wa Mungu ndio ule ule wa shetani, kabla ya kuwa ibilisi shetani, Lucifer was the 2nd in command baada ya Mungu, na hata baada ya usi alitimuliwa peponi na kutupwa Duniani with all the powers zikiwa intact.Ubashiri peke yake bila nyongeza yoyote ya nguvu zilizo nje ya mamlaka ya Mungu siyo ramli bali ni utabiri! Ramli ni ubashiri unaoambatana na matumizi ya nguvu nyingine za nyongeza ambazo hazitokani na mamlaka ya Mungu. Kwenye utabiri Mungu huwa anashiriki 100% ila kwenye ubashiri mchango wa Mungu ni 0%
How can you tell hata kilichomkuta Lissu sio sehemu ya karma?.pasco!acha kupoza hasira!!!Ya Lissu mbona hakuna Karma?watu wanadunda tu???!!!
Naunga mkono hojaUko sahihi kabisa. Nguvu za shetani kwa kuanzia unapewa bure uzitumie kwanza, na baada ya kuzitumia ndiyo unapewa bei na masharti yake. Za Mungu ukiona unazitumia, ujue tayari ulishazilipia kwa kufanya kazi kwenye kile ki-portion kidogo mno ambacho Mungu huwa anakitoa kama assignment kwako, kabla hajakuamini na kuchukua uamuzi wa kukutunuku mamlaka hayo. However, over 99.99% ya nguvu za Mungu ambazo huwa anawatunuku wanadamu ili wazitumie, zinatokana na neema ya Mungu tu na si vinginevyo. Huwa nawashangaa mno wale ambao huwa wanapenda kujiingiza kwenye mambo ya hatari ya ku-deal na shetani!
Huu sio muda wa ramli chonganishi!.Kwanza atujibu nani alimpiga risasi 38 Tundu Lisu? Nani aliwaua hao vijana wetu waliotekwa? Kwenda mbinguni lazima upitie Tohorani
PWanabodi,
Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, linapotokea jambo baya lolote, mtu unaruhusiwa kumhisi mtu yoyote kimawazo, ila huruhusiwi kumtaja wala kumuandika popote, huko ni kipiga ramli chonganishi. Ukimhisi mtu, usimtaje bali mfuatilie tuu nini kitamkuta, karma ndio itamshughulikia. Hivyo natoa wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".
Kwanza Tuendelee Kumuombea Lissu Uponyaji wa Haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.
Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.
Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.
Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.
Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...
Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...
Paskali
Mkuu,hujaonekana jukwaani mda mrefu! Karibu sana